Mhariri wa MWANANCHI ajeruhiwa na majambazi, aporwa TZS 1.5 Mil

Mdakuzi mkuu

JF-Expert Member
Dec 27, 2016
212
719
Alan+Pics.jpg


Mhariri wa Mafunzo wa kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), Allan Lawa amelazwa katika Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili (Moi) baada ya kujeruhiwa na majambazi waliomvamia nyumbani kwake usiku wa kuamkia leo (Alhamisi).

Mtoto wake, Isack Lawa amesema kwamba baba yake alivamiwa juzi saa saba usiku nyumbani kwake Tabata Bonyokwa na kumkatakata kwa mapanga na kisha kuchukua Sh1.5 milioni zilikuwapo.

“Jana usiku baba alivamiwa, mwenyewe anasema walikuwa ni vijana watatu waliovaa kininja. Walimkatakata kwa mapanga lakini mama yeye alipigwa kidogo hakuumizwa sana. Msichana wa kazi na wajukuu hawakuguswa kabisa,” amesema Isack.

Isack amesema baada ya tukio hilo, alipigiwa simu na majirani saa 8:30 usiku na akawahi nyumbani lakini alikuta baba yake ameshapelekwa Hospitali ya Amana.

Majirani waliripoti katika vituo vya polisi Buguruni na Stakishari.

“Nilifika ndani tu nikakuta vitu vimevunjikavunjika na damu zimetapakaa sebuleni, ikanibidi nielekee huko hospitali. Nilikuta bado yupo mapokezi baada ya muda kidogo akapatiwa huduma ya kwanza,” amesema Isack na kuongeza:

“Baada ya kupewa huduma ya kwanza, tulimhamisha na kumpeleka Hospitali ya Regency, ambako kutokana na hali aliyokuwa nayo, madaktari walishauri tumpeleke Muhimbili.”

Isack amesema, Lawa amejeruhiwa maeneo yote ya mwili lakini zaidi kichwani, kifuani na mikononi ambako kidole kidogo cha mkono wa kushoto kilikatwa kabisa, huku baadhi ya mishipa katika mikono nayo ilikatwa.

Hata hivyo, Isack amesema baada ya kipimo cha X-ray imeonekana hajapata majeraha ya fuvu ila sehemu ya kifua ndiyo iliyodhurika zaidi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni hakupatikana baada ya simu yake kuita bila kupokewa.

Chanzo: MWANANCHI
 
Pole.yake jamani kama wamemwachia.uhai afadhali coz hela inatafutwa siyo uhai
 
Dawa ya hawa jamaa ni polisi kutengeneza scene palepale kwenye crime scene....kama walivyowafanyia jana pale mikocheni
 
Hayo ndio madhara ya jobless ikiongezeka mitaani pamoja na ukata
 
Hayo ndio madhara ya jobless ikiongezeka mitaani pamoja na ukata
Kuna wakati gani kulikuwa hakuna ukata na ujambazi haukuwepo? Panya road wameibuka lini? Acha kuhusisha kila kitu na siasa. Wizi hauwezi kwisha sab ya wizi kubwa ni tamaa sio umaskini pekee kwa kuna wezi matajiri kuna mafisadi n.k wanapesa zao wasomi na wanaheshimika katika jamii.
 
Wememjerui baada ya kuleta ubishi au kuna kisasi nyuma ya pazia?
 
JPM majambazi yametamalaki ....kama doria za polisi hazitoshi ...ongeza na JWTZ ....hali mbaya ...
 
Kuna wakati gani kulikuwa hakuna ukata na ujambazi haukuwepo? Panya road wameibuka lini? Acha kuhusisha kila kitu na siasa. Wizi hauwezi kwisha sab ya wizi kubwa ni tamaa sio umaskini pekee kwa kuna wezi matajiri kuna mafisadi n.k wanapesa zao wasomi na wanaheshimika katika jamii.
Ndg yangu inaonekana we unajua hali ilivyo lkn unaamua kujisahurisha.
Bila kujali siasa madhara moja wapo la kuongezeka kwa ukosefu wa ajira nini?
Ukosefu wa ajira haukuanza kwa magufuri tu Bali ni zao LA ccm toka mwanzo hivyo magufuri huwezi kukwepa kwani ni kiongozi mwandamizi wa serikali za awamu zote za ccm.
Kila kitu nyie mnaleta ushabiki tu na kutetea hata ujinga ili mradi mnatimiza usemi wa ndiooooo kila kitu mtukufu anachofanya
 
Back
Top Bottom