Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 614
Kuna habari kwamba watu wasiojulikana wanaodhaniwa kuwa majambazi wamemvamia mhariri na mmiliki wa Mwanahalisi, Saed Kubena na kumkata kwa mapanga. Habari zaidi baadaye.
===========
Mwanahabari Saed Kubenea akiwa hospitali baada ya kumwagiwa tindikali
Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Mwana Halisi na Mseto, Said Kubenea, amevamiwa ofisini kwake na watu wenye silaha na kumwagiwa tindikali usoni na kusababisha apoteze uwezo wa kuona.
Katika tukio hilo, vile vile mshauri na Mhariri wa Habari wa magazeti hayo, Ndimara Tegambwage, alijeruhiwa na kushonwa nyuzi 15 kichwani baada ya watu hao kumkatakata kwa mapanga.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jamal Rwambow, ambaye alikuwa kiongozi wa kwanza kwenda kumjulia hali Kubenea hospitalini juzi usiku, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Hadi jana mchana, Kubenea (37) ambaye alijeruhiwa kwa kupigwa na kitu kizito karibu na jicho la kulia, alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), huku taratibu za kumpeleka nchini India kwa matibabu zaidi zikiendelea kufanywa kutokana na hali yake kuwa mbaya.
Tukio hilo limetokea baada ya watu wasiojulikana kuchoma moto gari lake na kisha kumpigia simu na kumtumia ujumbe wa maandishi wa simu (sms) wakitishia kumuua.
Akisimulia mkasa wa kushambuliwa na kumwagiwa tindikali hospitalini hapo jana, Kubenea ambaye anaongea kwa tabu kutokana kuelemewa na maumivu, alisema wakiwa ofisini kwenye saa 3:00 za usiku wa kuamkia jana pamoja na Ndimara ambaye pia ni Mkurugenzi wa Shirika lisilo la Kiserikali linaloshughulikia masuala ya Kijamii la IDEA na vijana wake watatu, watu watatu walifika na gari na kugonga mlango.
Kubenea alisema baada ya mlango kugongwa, alikwenda na kuufungua ili kuwatambua wageni waliokuwa wakibisha hodi.
Alisema baada ya kufungua mlango, watu wale walimwambia kuwa ‘Tunakutaka wewe’ na baada ya kuwambia hivyo, wakamwamuru kukaa chini na kuanza kutoa mapanga, visu na nondo.
“Nilipotaka kufunga mlango, wakawahi kuingia ndani. Ndimara ambaye alikuwa anasafiri leo (jana) kwenda Darfur, Sudan, akawauliza kuna nini? Kuuliza hivyo, wakamvamia Ndimara na kuanza kumshambulia kwa mapanga,” alisema Kubenea.
Alisema hali hiyo ilizua mapambano makali ofisini kati yao na watu hao yaliyodumu kwa dakika kadhaa kabla ya watu hao kuzidiwa nguvu na kukimbia.
Kubenea alisema tukio la kumwagiwa tindikali lilikuja baada ya mmoja wa watu hao kuangusha chini panga alilokuwa akilitumia na yeye (Kubenea) kuliokota na kutaka kulitumia katika mapambano hayo.
“Baada ya mapambano kuchukua kama dakika mbili hivi, panga la mmoja wao likaanguka chini. Nikaliokota, nilipotaka kulitumia, ndio wakanimwagia tindikali,” alisema Kubenea.
Hata hivyo, alisema hakukata tamaa, badala yake, alijitahidi na kuingia kwenye moja ya vyumba vya ofisi hiyo kutafuta silaha kwa ajili ya kukabiliana na watu hao na kufanikiwa kupata chupa lakini aliporudi kwa ajili ya kuendelea na mapambano, alikuta watu hao wametoka nje ambako waliendelea kupambana na Ndimara.
Alisema baada ya kudhibitiwa na Ndimara huko nje, watu hao walijaribu kummwagia tindikali usoni, lakini haikumuathiri kwa vile alivaa miwani.
“Ndimara alinisaidia sana. Kwani kama ningekuwa peke yangu, wangeniua au kuniteka,” alisema Kubenea.
Kubenea alisema baada ya hali kutulia, walikodi teksi na kukimbizwa katika hospitali binafsi ya Dk Mvungi iliyoko Kinondoni ambako walipatiwa huduma ya kwanza kabla ya usiku huo kuhamishiwa Muhimbili.
Alisema madaktari wanaomtibu wameshauri akatibiwe haraka nchini India kutokana na kutojua aina ya tindikali iliyotumika kumdhuru.
“Madaktari wanasema ingekuwa ni tindikali ya kawaida, ingekuwa rahisi kwao kunitibu, lakini hii inaweza kuendelea kutafuna kwa muda mrefu na kuathiri macho kabisa. Hivyo, wameshauri kama upo uwezekano ni vizuri nikaenda India haraka, ikiwezekana kesho (leo),” alisema Kubenea ambaye anaona kwa tabu.
Alisema anaamini watu waliotekeleza tukio hilo, wametumwa kumshughulikia kutokana na waliowatuma kuchukizwa na msimamo wake wa kuweka hadharani maovu ya baadhi ya vigogo serikalini kupitia magazeti yake.
Kubenea alisema dhana hiyo inapewa nguvu kutokana na kuwa tangu Juni 13, mwaka jana, amekuwa akitumiwa sms za vitisho ambapo miezi miwili badaye watu wasiojulikana walichoma moto gari lake na kutamba kupitia sms kuwa wametimiza jambo hilo na kwamba kilichobaki ni kuuondoa uhai wake.
Alisema baada gari lake kuchomwa moto, aliendelea kupokea sms zinazomweleza kuwa:
“Kiburi chako kitakuponza, jiandae kwa shughuli nzito itakayokupata”, “Kifo chako kitakuwa cha aina yake, mzoga wako hautaonekana”, “Dawa ya kushughulikia maiti kama wewe imepatikana, jiandae”, “Maandalizi ya mauti yako yameiva, watangazie mabwana zako wanaokutuma. Unanuka uvundo wa kufa”, “Vuta pumzi zako za mwisho, hatuko mbali, yamebaki masaa machache kabla hatujakupeleka panapostahili”.
Alisema awali, alidhani watu wanaomtumia sms hizo ni waandishi wenzake wanamtania. Lakini kadri matukio ya kutisha yalivyozidi kutokea, akaamini kuwa watu hao ni maadui zake.
Mamia ya watu wakiongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Zanzibar, Juma Duni Haji na Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Halima Mdee, waliokwenda kumjulia hali Kubenea, jana asubuhi walifurika katika Wodi ya Sewahaji chumba namba 19 alikolazwa mwandishi huyo kabla ya kuhamishiwa katika chumba maalum hospitalini hapo.
Akizungumza hospitalini hapo jana, Duni alisema Kubenea amekuwa mhanga wa kusimamia ukweli na kuwashutumu waliomtishia kumuua kwa sms.
Kamanda Rwambow, alisema polisi wanaendelea na upelelezi na kwamba leo watatoa taarifa rasmi kuhusiana na tukio hilo.
PIA, SOMA:
===========
Mwanahabari Saed Kubenea akiwa hospitali baada ya kumwagiwa tindikali
Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Mwana Halisi na Mseto, Said Kubenea, amevamiwa ofisini kwake na watu wenye silaha na kumwagiwa tindikali usoni na kusababisha apoteze uwezo wa kuona.
Katika tukio hilo, vile vile mshauri na Mhariri wa Habari wa magazeti hayo, Ndimara Tegambwage, alijeruhiwa na kushonwa nyuzi 15 kichwani baada ya watu hao kumkatakata kwa mapanga.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jamal Rwambow, ambaye alikuwa kiongozi wa kwanza kwenda kumjulia hali Kubenea hospitalini juzi usiku, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Hadi jana mchana, Kubenea (37) ambaye alijeruhiwa kwa kupigwa na kitu kizito karibu na jicho la kulia, alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), huku taratibu za kumpeleka nchini India kwa matibabu zaidi zikiendelea kufanywa kutokana na hali yake kuwa mbaya.
Tukio hilo limetokea baada ya watu wasiojulikana kuchoma moto gari lake na kisha kumpigia simu na kumtumia ujumbe wa maandishi wa simu (sms) wakitishia kumuua.
Akisimulia mkasa wa kushambuliwa na kumwagiwa tindikali hospitalini hapo jana, Kubenea ambaye anaongea kwa tabu kutokana kuelemewa na maumivu, alisema wakiwa ofisini kwenye saa 3:00 za usiku wa kuamkia jana pamoja na Ndimara ambaye pia ni Mkurugenzi wa Shirika lisilo la Kiserikali linaloshughulikia masuala ya Kijamii la IDEA na vijana wake watatu, watu watatu walifika na gari na kugonga mlango.
Kubenea alisema baada ya mlango kugongwa, alikwenda na kuufungua ili kuwatambua wageni waliokuwa wakibisha hodi.
Alisema baada ya kufungua mlango, watu wale walimwambia kuwa ‘Tunakutaka wewe’ na baada ya kuwambia hivyo, wakamwamuru kukaa chini na kuanza kutoa mapanga, visu na nondo.
“Nilipotaka kufunga mlango, wakawahi kuingia ndani. Ndimara ambaye alikuwa anasafiri leo (jana) kwenda Darfur, Sudan, akawauliza kuna nini? Kuuliza hivyo, wakamvamia Ndimara na kuanza kumshambulia kwa mapanga,” alisema Kubenea.
Alisema hali hiyo ilizua mapambano makali ofisini kati yao na watu hao yaliyodumu kwa dakika kadhaa kabla ya watu hao kuzidiwa nguvu na kukimbia.
Kubenea alisema tukio la kumwagiwa tindikali lilikuja baada ya mmoja wa watu hao kuangusha chini panga alilokuwa akilitumia na yeye (Kubenea) kuliokota na kutaka kulitumia katika mapambano hayo.
“Baada ya mapambano kuchukua kama dakika mbili hivi, panga la mmoja wao likaanguka chini. Nikaliokota, nilipotaka kulitumia, ndio wakanimwagia tindikali,” alisema Kubenea.
Hata hivyo, alisema hakukata tamaa, badala yake, alijitahidi na kuingia kwenye moja ya vyumba vya ofisi hiyo kutafuta silaha kwa ajili ya kukabiliana na watu hao na kufanikiwa kupata chupa lakini aliporudi kwa ajili ya kuendelea na mapambano, alikuta watu hao wametoka nje ambako waliendelea kupambana na Ndimara.
Alisema baada ya kudhibitiwa na Ndimara huko nje, watu hao walijaribu kummwagia tindikali usoni, lakini haikumuathiri kwa vile alivaa miwani.
“Ndimara alinisaidia sana. Kwani kama ningekuwa peke yangu, wangeniua au kuniteka,” alisema Kubenea.
Kubenea alisema baada ya hali kutulia, walikodi teksi na kukimbizwa katika hospitali binafsi ya Dk Mvungi iliyoko Kinondoni ambako walipatiwa huduma ya kwanza kabla ya usiku huo kuhamishiwa Muhimbili.
Alisema madaktari wanaomtibu wameshauri akatibiwe haraka nchini India kutokana na kutojua aina ya tindikali iliyotumika kumdhuru.
“Madaktari wanasema ingekuwa ni tindikali ya kawaida, ingekuwa rahisi kwao kunitibu, lakini hii inaweza kuendelea kutafuna kwa muda mrefu na kuathiri macho kabisa. Hivyo, wameshauri kama upo uwezekano ni vizuri nikaenda India haraka, ikiwezekana kesho (leo),” alisema Kubenea ambaye anaona kwa tabu.
Alisema anaamini watu waliotekeleza tukio hilo, wametumwa kumshughulikia kutokana na waliowatuma kuchukizwa na msimamo wake wa kuweka hadharani maovu ya baadhi ya vigogo serikalini kupitia magazeti yake.
Kubenea alisema dhana hiyo inapewa nguvu kutokana na kuwa tangu Juni 13, mwaka jana, amekuwa akitumiwa sms za vitisho ambapo miezi miwili badaye watu wasiojulikana walichoma moto gari lake na kutamba kupitia sms kuwa wametimiza jambo hilo na kwamba kilichobaki ni kuuondoa uhai wake.
Alisema baada gari lake kuchomwa moto, aliendelea kupokea sms zinazomweleza kuwa:
“Kiburi chako kitakuponza, jiandae kwa shughuli nzito itakayokupata”, “Kifo chako kitakuwa cha aina yake, mzoga wako hautaonekana”, “Dawa ya kushughulikia maiti kama wewe imepatikana, jiandae”, “Maandalizi ya mauti yako yameiva, watangazie mabwana zako wanaokutuma. Unanuka uvundo wa kufa”, “Vuta pumzi zako za mwisho, hatuko mbali, yamebaki masaa machache kabla hatujakupeleka panapostahili”.
Alisema awali, alidhani watu wanaomtumia sms hizo ni waandishi wenzake wanamtania. Lakini kadri matukio ya kutisha yalivyozidi kutokea, akaamini kuwa watu hao ni maadui zake.
Mamia ya watu wakiongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Zanzibar, Juma Duni Haji na Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Halima Mdee, waliokwenda kumjulia hali Kubenea, jana asubuhi walifurika katika Wodi ya Sewahaji chumba namba 19 alikolazwa mwandishi huyo kabla ya kuhamishiwa katika chumba maalum hospitalini hapo.
Akizungumza hospitalini hapo jana, Duni alisema Kubenea amekuwa mhanga wa kusimamia ukweli na kuwashutumu waliomtishia kumuua kwa sms.
Kamanda Rwambow, alisema polisi wanaendelea na upelelezi na kwamba leo watatoa taarifa rasmi kuhusiana na tukio hilo.
PIA, SOMA:
- Kubenea kumwagiwa tindikali: Nini chanzo?
- Saed Kubenea atiwa mbaroni. Afikishwa Mahakamani kwa kuingia nchini kinyume na Sheria, utakatishaji fedha na kupelekwa rumande
- Saed Kubenea aachiwa kwa dhamana
- Kubenea amwaga chozi
- Saed Kubenea amburuza Paul Makonda Mahakamani, kupanda kizimbani Desemba 3, 2021 kwa makosa ya jinai
- Miaka 16 imepita haijajulikana nani alimmwagia tindikali Saed Kubenea
- Saed Kubenea afika Wizara ya Habari Kuonana na Waziri Bashungwa kuitikia wito wa Rais wa kufungulia vyombo vya habari vilivyofungiwa kibabe
- Mwandishi wa kampuni ya Mwananchi Communications (MCL), Azory Gwanda apotea siku 10 na hajulikani alipo
- Absalom Kibanda (Mwenyekiti wa Jukwa la Wahariri) avamiwa na watu wasiojulikana na kujeruhiwa
- Mwandishi Mwangosi auawa katika vurugu kati ya Polisi na CHADEMA
- Mwanahabari Erick Kabendera akamatwa na Polisi nyumbani kwake; yadaiwa anaendelea na Mahojiano
- Mwandishi wa Mwananchi Jesse Mikofu ashambuliwa na askari akitekeleza majukumu yake
- Mchora katuni Opptertus John Fwema ashikiliwa na Polisi kwa Makosa ya Mtandao
- Mwandishi wa Watetezi TV mbaroni kwa madai ya kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni juu ya watuhumiwa kulazimishwa kulawitiana Kituo cha Polisi
- Mwandishi wa Habari, Kazimbaya Makwega ashikiliwa na Polisi, asafirishwa kutoka Mwanza hadi Dodoma