Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Habari nilizopata mchana huu kutoka kwa mwandishi mmoja mwandamizi wa gazeti la Serikali la Daily News zinasema kwamba kaimu Mhariri Mkuu wa gazeti hilo, Mkumbwa Alli anang'olewa kutoka wadhifa huo na badala yake kuwekwa mwingine ambaye atatangazwa si muda mrefu.
Huyu mpya atakauwa Mhariri Mtendaji moja kwa moja, na si kaimu tena kama alivyokuwa Mkumbwa Alli.
Habari zinasema Mkumbwa Alli atapangiwa kazi nyingine katika idara/taasisi nyingine ya serikali.
Wenye habari zaidi kuhusu tetesi hii watujuze.