Hakuna shaka juu ya huo msemo, mwananchi mwenyewe ndio mwenye uwezo wa kuijenga na kuiharibu nchi. Hata kukitokea mgeni kutaka kuharibu nchi ni lazima apitie kwa mwananchi mwenyewe
Nimeona bandiko la Mjomba Paskali kuhusu alichokiita Security Alert. Alichoandika Paskali kilitakiwa kuonwa na wenye mamlaka ya nchi ambao kila siku ya Mungu hawalali kuhakikisha Taifa liko salama na naamini kabisa wanajua mengi zaidi. Wanasema kazi yao ni kushauri tu japo inapobidi wanaweza kwenda hatua zaidi.
Adui hawezi kujaribu kuharibu nchi kabla uzalendo haujapotea kwa kiasi kikubwa miongoni mwa wananchi. Suala la Uzalendo limepungua sana kwa kiasi kikubwa kwa mtazamo wangu, na hilo limesababishwa na wanasiasa, uonevu na ubaguzi kwa minajili ya vyama, kesi za kukomoana, utekaji, utesaji HUKU tukiwa tunaangalia tu jinsi taifa linavyomeguka. Ikifikia asilimia 96 ya wagombea wa vyama vya upinzani wanatolewa kwa figisu kwenye chaguzi za serikali za mitaa ni jambo la hatari. Wananchi kususia kujiandikisha na kushiriki Chaguzi lilitakiwa kutushtua. Lakini tumefumba macho hatujui tunatengeneza bomu
Leo hii kuna wenye hisia kuwa wanaonewa na wanaona hawana pa kukimbilia, kwamba kila unapoenda unakutana na maagizo. Kama mbunge anaweza kupigwa risasi, akafungwa jela kwa kesi za kubambikiwa na kuvuliwa ubunge kwa njama za kisiasa na akakosa pa kwenda kutafuta haki vipi kuhusu mwanachama wa kawaida?
Ndio maana leo hii Marekani akitoa tamko linaloonekana kutetea haki anapata sapoti nyingi ya kundi kubwa la watanzania ambao wengine hufurahia maamuzi yanayochukuliwa hata kama yatakuja kutuathiri wote kama taifa. Marekani siku zote anapita humo humo mlikotengeneza nyufa zenu. Nyufa tunatengeneza wenyewe mgeni anakuja kupita humo humo kwenye nyufa kisha tunaanza kulaumu. Lawama ni kwetu wenyewe.
Haya ya mganyiko katika Taifa watu walikuwa wanaonya lakini wanapuuziwa. Majuto ni mjukuu.
Mfano aliotoa Paskali, watu kama Saddam na Gadhaffi hawa walitawala kwa mkono wa chuma, walikandamiza watu kupitia vyombo vya dola matokeo yake nyufa zikatengenezwa ( ndio ni kweli Marekani kuna maslahi yake hivyo hivyo pia bila nyufa hawezi kuingia).
Tuache masuala ya uonevu kwa misingi ya vyama, mikutano ya kisiasa iruhusiwe, watu watoe wa moyoni, tuache mihimili iwe huru, tugawane keki ya taifa kwa usawa. Ukipitia mitandaoni humo utagundua mapenzi kwa nchi yameanza kupungua, inafikia watu wanatoa dhihaka hadi kwenye kurasa za viongozi wa kitaifa, sio jambo lenye afya. Watu washasahau Cybercrime hawaigopi tena.
Nikumbushie kile kilichoitwa 'maandamano ya Mange na kuiweka nchi katika security level ya hali ya juu ( nchi ilikuwa katika tension). Klichotokea ni kwamba watu walitamani, wakaweka nia ila wakawa waoga tu hawakutokea barabarani. Huo uoga siku ukiwatoka adui anapenya humo humo.
HATUJACHELEWA
Pascal Mayalla
Nimeona bandiko la Mjomba Paskali kuhusu alichokiita Security Alert. Alichoandika Paskali kilitakiwa kuonwa na wenye mamlaka ya nchi ambao kila siku ya Mungu hawalali kuhakikisha Taifa liko salama na naamini kabisa wanajua mengi zaidi. Wanasema kazi yao ni kushauri tu japo inapobidi wanaweza kwenda hatua zaidi.
Adui hawezi kujaribu kuharibu nchi kabla uzalendo haujapotea kwa kiasi kikubwa miongoni mwa wananchi. Suala la Uzalendo limepungua sana kwa kiasi kikubwa kwa mtazamo wangu, na hilo limesababishwa na wanasiasa, uonevu na ubaguzi kwa minajili ya vyama, kesi za kukomoana, utekaji, utesaji HUKU tukiwa tunaangalia tu jinsi taifa linavyomeguka. Ikifikia asilimia 96 ya wagombea wa vyama vya upinzani wanatolewa kwa figisu kwenye chaguzi za serikali za mitaa ni jambo la hatari. Wananchi kususia kujiandikisha na kushiriki Chaguzi lilitakiwa kutushtua. Lakini tumefumba macho hatujui tunatengeneza bomu
Leo hii kuna wenye hisia kuwa wanaonewa na wanaona hawana pa kukimbilia, kwamba kila unapoenda unakutana na maagizo. Kama mbunge anaweza kupigwa risasi, akafungwa jela kwa kesi za kubambikiwa na kuvuliwa ubunge kwa njama za kisiasa na akakosa pa kwenda kutafuta haki vipi kuhusu mwanachama wa kawaida?
Ndio maana leo hii Marekani akitoa tamko linaloonekana kutetea haki anapata sapoti nyingi ya kundi kubwa la watanzania ambao wengine hufurahia maamuzi yanayochukuliwa hata kama yatakuja kutuathiri wote kama taifa. Marekani siku zote anapita humo humo mlikotengeneza nyufa zenu. Nyufa tunatengeneza wenyewe mgeni anakuja kupita humo humo kwenye nyufa kisha tunaanza kulaumu. Lawama ni kwetu wenyewe.
Haya ya mganyiko katika Taifa watu walikuwa wanaonya lakini wanapuuziwa. Majuto ni mjukuu.
Mfano aliotoa Paskali, watu kama Saddam na Gadhaffi hawa walitawala kwa mkono wa chuma, walikandamiza watu kupitia vyombo vya dola matokeo yake nyufa zikatengenezwa ( ndio ni kweli Marekani kuna maslahi yake hivyo hivyo pia bila nyufa hawezi kuingia).
Tuache masuala ya uonevu kwa misingi ya vyama, mikutano ya kisiasa iruhusiwe, watu watoe wa moyoni, tuache mihimili iwe huru, tugawane keki ya taifa kwa usawa. Ukipitia mitandaoni humo utagundua mapenzi kwa nchi yameanza kupungua, inafikia watu wanatoa dhihaka hadi kwenye kurasa za viongozi wa kitaifa, sio jambo lenye afya. Watu washasahau Cybercrime hawaigopi tena.
Nikumbushie kile kilichoitwa 'maandamano ya Mange na kuiweka nchi katika security level ya hali ya juu ( nchi ilikuwa katika tension). Klichotokea ni kwamba watu walitamani, wakaweka nia ila wakawa waoga tu hawakutokea barabarani. Huo uoga siku ukiwatoka adui anapenya humo humo.
HATUJACHELEWA
Pascal Mayalla