Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo abeza marufuku ya uuzaji mazao nje

streetwiser

Member
Jul 11, 2008
30
3
SOURCE: Alasiri [Accessed 2008-08-11 19:25:26]

Mhadhiri wa Chuo cha Kilimo cha Sokoine, SUA, Dk. Damian Gabagambi amedai kuwa marufuku ya kuwazuia wakulima kuuza mazao yao ndani na nje ya nchi ni kuwasababishia umaskini usiokuwa wa lazima.

Pia akawataka wanaharakati kuwasaidia wakulima kuifikisha mahakamani serikali kupigania haki yao dhidi ya katazo hilo la serikali linalosimamiwa na wakuu wa wilaya na mikoa nchini na kuwafanya wakulima wasinufaike na kazi zao.

Dk Gabagambi, amesema kuwa katazo la serikali la kuzuia wakulima kuuza mazao yao inasababisha umaskini kwa kuwa inawafanya wahusika kushindwa kupata fedha na kujiendeshea maisha yao ikiwemo kulipia gharama za elimu.

Mhadhiri huyo amedai kuwa si tu linakwamisha mipango ya maendeleo ya kuinua sekta na uchumi kwa ujumla, lakini pia ni unyanyasaji uliovuka mipaka kwa kuwakataza wakulima wanamenyeka kuzalisha kwa dhiki na tabu kubwa na kuja kupangiwa wapi na mahali gani pa kuuza.

``Wanaharakati wasaidie kuwaongoza wakulima ambao asilimia kubwa hawajui haki zao kuifungulia mashtaka serikali kwa unyanyasaji huo ili kukomesha jambo hilo,`` akasema.

Akiongea kwa uchungu Dk. Gabagambi, amesema kuwa ingekuwa vema kama serikali ingekuwa inawawezesha wakulima katika uzalishaji na sio kuibuka pale mazao yaliyowasumbua wakulima yakiwa yameshavunwa na kuwabana.

Juu ya hofu ya serikali kukabiliana na uhaba wa chakula, mhadhiri huyo amesema ni wajibu serikali ikatoa mkusuko kwa kuweka mipango madhubuti wakulima wakazalisha kwa wingi mazao na kupata akiba katika ghala la taifa na ziada ikauzwa nje kuwafanya wakulima wapate moyo wa kuendelea na kilimo.
 
If I can say nothing about the arguments raised, I will say that the mere positing of such arguments, so open, the person so exposed and vulnerable, so uneiquivocal and unambiguously formed, singles out this person for his independence of mind, courageous conviction and a pioneering spirit that is so lacking in our intellectuals.

GT would do well to note there is hope on this after all, too bad he is banned (or so I hear).
 
Kwa kweli hili jambo limekuwa liki nisumbua saana, kwa sababu kwa uapande mmoja serekali yetu inazungumzia biashara huria, kwa upande mwingine inawazui wakulima kuuza bidha zao watakapo pata pato zuri, hii si haki na si sawa, pili hakuzi uzalishaji na utaalamu wa utunzaji wa bidha na kujielekeza katika kuboresha mazao yetu.
fikiria huyu mkulima hapewi mkopo, pembejeo ananunua at competitive price, lakini bidhaa yake ikiwa tayari anapewa bei na serekali au soko na serekali.
Kwa mfano mkulima wa kahawa kagera anaweza kupata bei ya juu uganda au rwanda wakati wote hawa soko lao la kimataifa ni moja, au wakulima wa mahindi arusha/moshi/bariadi/tarime wanaweza pata bei nzuri kenya, au ndugu zangu wa mbeya/rukwa kuuza mahindi/maharage nk zambia/malawi au drc.
 
.......hivi wabunge wetu kwa nini wasiitake serikali iwalipe tofauti ya bei kama kweli serikali inayataka mazao hayo ya wakulima? badala ya kuwazuia kuuza kwa faida mazao yao?
 
Kingine cha kusikitisha ni kuwa serikali yetu inamkataza mkulilma kuuza mahindi kwa mfano Uganda au Kenya lakini mfanyabiashara anaruhusiwa kuuza sembe huko sasa huu niuonevu wa hali ya juu.
 
Kwa kuongezea, wakulima wanachukuliwa kama watu wasiokuwa na malengo wanapofanya shughuli zao! Nadhani hakuna anayewekeza nguvu na muda wake katika kazi au shughuli yeyote bila kuwa na matarajio.Matarajio ya wakulima wanapolima ni kuvuna na kuuza wapate fedha kujikimu.
Sasa` serikali inapoingilia katika utaratibu wa maisha ya mkulima wanatarajia nini?? Wamewahi kushiriki kupanga na wakulima ili kujua matarajio yao na iwapo hayatafikiwa kwa sababu mathalani njaa inazuia wasiuze mazao yao nje watafidiwa vipi?
Wahusika wanapaswa kuwaheshimu wakulima badala ya kuwaingilia na kuwasababishia hasara!
 
Mkulima ni mtu wa kupewa amri. Hana mamlaka na jasho lake na wala serikali haimpi ulinzi wowote kimaslahi au kimaisha.

Haruhusiwi kuuza mahindi mabichi - ma-RC na ma-DC wanao uwezo (!) wa kupiga marufuku sio uuzaji wa jumla tu, hata biashara ya mahindi ya kuchoma barabarani. Yeye anatakiwa kukaa miezi 6 mpaka 9 kusubiri yakauke na pia asubiri kama SGR watapewa pesa na serikali kununulia mahindi yao.

Huu ni ugandamizaji wa hali ya juu kwa mtu ambaye mbolea ya ruzuku haimfikii, anatakiwa alipe 20,000/= ya ujenzi wa shule, hana njia nyingine ya kuyakimu maisha yake na wala serikali haina mpango wa kuhakikisha kuna value-added kwenye mazao yake.
 
mhadhiri nakushauri ipeleke serikali mahakamani............si unajua yule jamaa kasema hana shamba asiulizwe habari ya njaa km utauza ughaibuni.
pia wasomi wa SUA kwa nn msiwasaidie wakulima kuunda vikundi na kampuni za kulima na ku process ili waongeza mnyororo wa thamani wa mazao?mnajua Phd zenu sisi walalahoi hatuoni umuhim wenu zaidi ya kuandika pepa za kupanda vyeo vyenu........
Sua kuna shahada za agro econimics na agrobusness na za kilimo km horticulture,agriculture general msipo saidia serikali na wananchi na nyie mkawa watu wa majukwaani km ma DC naRC mnatupa utata sisi wakulima kuwatofautisha nyinyi na akina Mlisho
 
Back
Top Bottom