Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,898
Mhadhiri wa Chuo kikuu cha Dodoma, Dkt. Paul Luisilie amesema ziara na mahojiano anayoyafanya Tundu Lissu huko Ulaya na Marekani yatakuwa na athari kubwa katika siasa za Tanzania, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2020 na kuna uwezekano wa mataifa makubwa kufanya uamuzi mgumu dhidi ya Tanzania.
Amesema ziara hizo zinaliweka taifa katika wakati mgumu kiuchumi kwa kuwa anazifanya katika nchi zinazotoa misaada kwa Tanzania.
"Mpaka sasa athari za ziara ya Lissu zimeshaanza kuonekana, kwa kuwa mjadala ni mkubwa. Ndani ya CCM kwenyewe wanajadiliana. Hiyo ni impact.
Lissu alishapata huruma kubwa ya wananchi, matusi mengi anayotukanwa yanamjenga. Tumesikia spika akisema watakatisha mshahara wake, huku nako ni kumjenga maana watu wanajadili mshahara huo. Yani hatapata taabu kupigiwa kura kwa kuwa ameshajijenga wakati huu" - Alisema Dkt. Luisilie.
Mhadhiri huyo amesema tayari mitaani watu hasa vijana washaanza kuvutiwa na ujasiri wa Lissu na kutokata tamaa.
Amesema ziara hizo zinaliweka taifa katika wakati mgumu kiuchumi kwa kuwa anazifanya katika nchi zinazotoa misaada kwa Tanzania.
"Mpaka sasa athari za ziara ya Lissu zimeshaanza kuonekana, kwa kuwa mjadala ni mkubwa. Ndani ya CCM kwenyewe wanajadiliana. Hiyo ni impact.
Lissu alishapata huruma kubwa ya wananchi, matusi mengi anayotukanwa yanamjenga. Tumesikia spika akisema watakatisha mshahara wake, huku nako ni kumjenga maana watu wanajadili mshahara huo. Yani hatapata taabu kupigiwa kura kwa kuwa ameshajijenga wakati huu" - Alisema Dkt. Luisilie.
Mhadhiri huyo amesema tayari mitaani watu hasa vijana washaanza kuvutiwa na ujasiri wa Lissu na kutokata tamaa.