Mhadhiri TUDARCo ashtaki na Kudai fidia kwa kutengenezewa mazingira magumu ili aache kazi

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,005
9,872
Mmoja wa waanzilishi wa kitivo cha Sheria kutoka Chuo Kikuu cha Tumaini, Dar Es Salaam (Tudarco), Dk Lucas Kamanija anakidai chuo hicho fidia ya Sh130milioni, akidai kutengenezewa mazingira magumu yaliyomsababishia aachishwe kazi chuoni hapo.

Dk Kamanija amedai fidia hiyo, baada ya kufungua kesi ya madai katika Baraza la Usuluhishi wa Migogoro ya Kazi (CMA) akidai kulipwa fidia hiyo.

Chuo hicho kimekiri kuyatambua madai hayo, ambapo Naibu Mkuu wa chuo Utawala, Mchungaji Ipiana Mwamugobole aliyezungumza na Mwananchi kwa simu amesema wanaamini kuwa watalimaliza suala hilo nje ya kwa amani nje ya baraza hilo.

“Mambo haya ya mikwaruzano wala si mazuri kabisa, sisi kama chuo tunaendelea kuamini kuwa jambo hili linaweza kumalizika kwa amani na hilo likifanyika faida itakuwa ni kwa pande zote mbili,” amesema Mchungaji Mwamugobole.

Amesema migogoro mingi ambayo haimalizwi kwa njia ya amani imekuwa na athari na haiwezi kuwa na faida sio tu kwa chuo hata kwa mtu binafsi ambaye analalamika.

Hata hivyo, madai ya Dk Kamanija yanayosikilizwa mbele ya msuluhishi, Edgar Fungo yameshindwa kufikia mwafaka na hivyo kupelekwa ngazi nyingine.

Hivi karibuni, shauri hilo liliitishwa kwa ajili ya kutolea uamuzi, lakini uamuzi huo haukufikia mwafaka, hali iliyosababisha msuluhishi wa shauri hilo kulipeleka ngazi za juu.

Mlalamikaji anatetewa na Wakili Nicholus Kashililika na Cheba Kameya huku upande wa chuo ambao ni walalamikiwa wakitetewa na wakili George Masoud.

Akiwasilisha hoja ya mteja wake, Wakili Kashililika alisema kuwa, Dk Kamanija amefungua madai hayo katika baraza hilo akiomba kulipwa fidia ya kiasi hicho cha fedha kutokana na kutengenezewa mazingira magumu ya ufanyaji kazi yaliyosababisha aache kazi.

Baada ya mabishano ya kisheria ambayo yalishindwa kufikia muafaka, msuluhishi Fungo aliamua shauri hilo liende kwenye hatua zingine za juu.

Chanzo: Mwananchi
 
Hii kitaalamu yaitwa constructive termination, yaani mwajiri anafanya mambo ambayo yatamfanya mwajiriwa kuacha kazi, kuna wigo mpana sana kwenye hili.

Mfano; Mwajiriwa anafika ofisini na hapangiwi majukumu yake kama inavyoanishwa kwenye mkataba wa ajira yaani anafika halafu anakaa tu n.k
 
Jaribu kufungua hilo boksi la hayo mazingira magumu aliyopewa huyo Daktari wa Falsafa.
 
Hii kitaalamu yaitwa constructive termination, yaani mwajiri anafanya mambo ambayo yatamfanya mwajiriwa kuacha kazi, kuna wigo mpana sana kwenye hili...

Mfano; Mwajiriwa anafika ofisini na apangiwi majukumu yake kama inavyoanishwa kwenye mkataba wa ajira yaani anafika halafu anakaa tu n.k
Au unaweza kupangiwa majukumu yaliyoshindikana au nje ya fani yako!
 
TUDARCO imekula kwao walikua wanamtegemea Dkt. Masumbuko Lamwai saizi kafa wanaisoma namba
 
Mimi nilifanyiwa mambo hayo ili niache kazi mwenyewe mwisho wakanipa redundancy.

Pia swala langu lipo CMA, Ila kwa sasa namtafuta mwanasaikolojia ili anisaidie juu madhara niliyoyapata kutokana madhila ya hiyo Kampuni
Hebu funguka kidogo, ilikuwaje? Sasa ukienda kazini halafu hupangiwi majukumu ya kazi si ni jambo la heri tu! Unatumia muda huo kwa mambo mengine!

Muhimu mshahara unaingia mwisho wa mwezi.
 
Hii kitaalamu yaitwa constructive termination, yaani mwajiri anafanya mambo ambayo yatamfanya mwajiriwa kuacha kazi, kuna wigo mpana sana kwenye hili.

Mfano; Mwajiriwa anafika ofisini na hapangiwi majukumu yake kama inavyoanishwa kwenye mkataba wa ajira yaani anafika halafu anakaa tu n.k
Hii hapa anafanya sana mama mmoja ambaye ni Katibu Mtendaji wa Taasisi moja ya Uwezeshaji chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Huyu Katibu Mtendaji akiona wewe ni mwiba anaku frustrate mpaka uone kazi chungu. Yaaani toka aingie kwenye hiyo taasisi miaka 6 iliyopita ametesa sana watumishi. Wengi walijiondokea kimya kimya kwa kuomba uhamisho wenyewe kutoka Utumishi. Kuna ambaye bado hajafanikiwa kupata uhamisho hivyo anateseka mno maana kazi hampi.

Huyu mama alimnyanyasa sana ndugu yangu mpaka Karibu apate mental tukamshauri aache kazi. Lakini alivyokuwa na Mungu akamtoa pale. Sote kwenye familia tulifurahia sana na kumshukuru Mungu. Yaani kifupi tuiitana tukamshukuru Mungu.

Ila tunachojua Malipo ni hapa hapa DUNIANI. Ipo siku kama hayatamkuta huyo Mtendaji lakini yatakikuta kizazi chake.

Ametesa sana watu na inaelekea ndiyo tabia yake maana hata huko alikokuwa anafanya kazi kabla alitesa sana wale watumishi waliogusa maslahi yake.

Serikali iwe inachunguza sana taasisi zake kuna viongozi ambao hawafai kabisa.
Ninashukuru Mungu niliamua kujiajiri miaka mingi maana viongozi kama hao nisingewavumilia kabisa.
 
Kazi uache mwenyewe,na katika mazingira hayo magumu mshahara nilikuwa nakulipa bila wasiwasi halafu nikulipe fidia ya 130 milioni???

Sasa hapo huyo Hakimu alishindwaje kutoa maamuzi wakati kazi umeacha mwenyewe sijakusitishia mkataba?
 
Mzee wa paradox za Jurisprudence akianza wataja wakina John Austin, Bentham, Prof. Hat, St. Thomas Acqunas, St. Augustine, Socrates, Plato et al utafurahia lecture.
 
Kazi uache mwenyewe,na katika mazingira hayo magumu mshahara nilikuwa nakulipa bila wasiwasi halafu nikulipe fidia ya 130 milioni???

Sasa hapo huyo Hakimu alishindwaje kutoa maamuzi wakati kazi umeacha mwenyewe sijakusitishia mkataba?
Mkuu haya ni masuala ya kisheria na sio mtazamo wa nje. Nadhani kwa kuwa ni la kisheria ungepata mwongozo wa kisheria.
 
Mmoja wa waanzilishi wa kitivo cha Sheria kutoka Chuo Kikuu cha Tumaini, Dar Es Salaam (Tudarco), Dk Lucas Kamanija anakidai chuo hicho fidia ya Sh130milioni, akidai kutengenezewa mazingira magumu yaliyomsababishia aachishwe kazi chuoni hapo.

Dk Kamanija amedai fidia hiyo, baada ya kufungua kesi ya madai katika Baraza la Usuluhishi wa Migogoro ya Kazi (CMA) akidai kulipwa fidia hiyo.

Chuo hicho kimekiri kuyatambua madai hayo, ambapo Naibu Mkuu wa chuo Utawala, Mchungaji Ipiana Mwamugobole aliyezungumza na Mwananchi kwa simu amesema wanaamini kuwa watalimaliza suala hilo nje ya kwa amani nje ya baraza hilo.

“Mambo haya ya mikwaruzano wala si mazuri kabisa, sisi kama chuo tunaendelea kuamini kuwa jambo hili linaweza kumalizika kwa amani na hilo likifanyika faida itakuwa ni kwa pande zote mbili,” amesema Mchungaji Mwamugobole.

Amesema migogoro mingi ambayo haimalizwi kwa njia ya amani imekuwa na athari na haiwezi kuwa na faida sio tu kwa chuo hata kwa mtu binafsi ambaye analalamika.

Hata hivyo, madai ya Dk Kamanija yanayosikilizwa mbele ya msuluhishi, Edgar Fungo yameshindwa kufikia mwafaka na hivyo kupelekwa ngazi nyingine.

Hivi karibuni, shauri hilo liliitishwa kwa ajili ya kutolea uamuzi, lakini uamuzi huo haukufikia mwafaka, hali iliyosababisha msuluhishi wa shauri hilo kulipeleka ngazi za juu.

Mlalamikaji anatetewa na Wakili Nicholus Kashililika na Cheba Kameya huku upande wa chuo ambao ni walalamikiwa wakitetewa na wakili George Masoud.

Akiwasilisha hoja ya mteja wake, Wakili Kashililika alisema kuwa, Dk Kamanija amefungua madai hayo katika baraza hilo akiomba kulipwa fidia ya kiasi hicho cha fedha kutokana na kutengenezewa mazingira magumu ya ufanyaji kazi yaliyosababisha aache kazi.

Baada ya mabishano ya kisheria ambayo yalishindwa kufikia muafaka, msuluhishi Fungo aliamua shauri hilo liende kwenye hatua zingine za juu.

Chanzo: Mwananchi
Nilichoshangaa zaidi,huyo aliyefanyiwa hayo ni MWANZILISHI wa Kitivo cha SHERIA hapo chuoni

kama wamefanya hivyo kwa mti mbichi vipi kwa mti mkavu?
 
Ajira ya taasisi binafsi ni changamoto mno dakika sifuri huna kazi
Nilichoshangaa zaidi,huyo aliyefanyiwa hayo ni MWANZILISHI wa Kitivo cha SHERIA hapo chuoni

kama wamefanya hivyo kwa mti mbichi vipi kwa mti mkavu?
 
Back
Top Bottom