Papaa Mobimba
JF-Expert Member
- Jan 27, 2018
- 746
- 3,055
Mhadhiri wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Samsoni Mahimbo (68), amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na kesi ya kuomba rushwa ya ngono kwa mwanafunzi wake ili amfaulishe ktk mitihani wa marudio (Supplement), Kesi imeahirishwa hadi September 17.
Mshtakiwa anadaiwa ametenda kosa hilo Januari 12 , 2017 huko katika nyumba ya kulala wageni ya Camp David iliyoko Mlalakuwa Mwenge.
Inadaiwa siku ya tukio, mshtakiwa akiwa muajiriwa wa chuo hicho cha NIT kama Mhadhiri kwa muhula wa kwanza wa masomo wa mwaka 2015/2016 wa somo la usimamizi wa barabara na usafirishaji (road transport management), lenye kodi namba 07101 alitumia mamlaka yake kutokana na nafasi yake chuoni hapo na kuomba rushwa ya ngono kutoka kwa mwanafunzi, Victoria Faustine ambae ni mwanafunzi wa chuo hicho anayosomea mafunzo hayo ya road transport management.
Inadaiwakuwa, mshtakiwa aliomba rushwa hiyo kama sharti kwa mwanafunzi huyo kuwa atamfaulisha katika mtihani wa marudio (Supplement) wa somo hilo uliokuwa ukifanyika January 5, 2017.
Hata hivyo mshtakiwa amekana kutenda kosa hilo ambapo ameachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya kuwa na mdhamini mmoja atakayesaini bondi ya Sh. Milioni 4.
Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi katika kesi hiyo umekamilika. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 17,2019 mshtakiwa atakaposomewa maelezo ya awali.
Pia soma
Mshtakiwa anadaiwa ametenda kosa hilo Januari 12 , 2017 huko katika nyumba ya kulala wageni ya Camp David iliyoko Mlalakuwa Mwenge.
Inadaiwa siku ya tukio, mshtakiwa akiwa muajiriwa wa chuo hicho cha NIT kama Mhadhiri kwa muhula wa kwanza wa masomo wa mwaka 2015/2016 wa somo la usimamizi wa barabara na usafirishaji (road transport management), lenye kodi namba 07101 alitumia mamlaka yake kutokana na nafasi yake chuoni hapo na kuomba rushwa ya ngono kutoka kwa mwanafunzi, Victoria Faustine ambae ni mwanafunzi wa chuo hicho anayosomea mafunzo hayo ya road transport management.
Inadaiwakuwa, mshtakiwa aliomba rushwa hiyo kama sharti kwa mwanafunzi huyo kuwa atamfaulisha katika mtihani wa marudio (Supplement) wa somo hilo uliokuwa ukifanyika January 5, 2017.
Hata hivyo mshtakiwa amekana kutenda kosa hilo ambapo ameachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya kuwa na mdhamini mmoja atakayesaini bondi ya Sh. Milioni 4.
Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi katika kesi hiyo umekamilika. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 17,2019 mshtakiwa atakaposomewa maelezo ya awali.
Pia soma
Mtego wa TAKUKURU wamnasa Mhadhiri NIT akiomba rushwa ya ngono
Mhadhiri Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Samson Mahimbo (66yrs) akamatwa na TAKUKURU Wilaya ya Kinondoni baada ya kunaswa katika mtego wa rushwa ya ngono kwa mwanafunzi. Kwa mujibu wa taarifa ya Kaimu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Kinondoni, Denis Manumbu ameeleza kuwa mtuhumiwa huyo...
www.jamiiforums.com