Mh. Waziri mwenye dhamana, Wanafunzi wa Mitihani(secondary) na Vyuo warudi vyuoni kuendelea na masomo yao

Wewe una mtoto?

Sisi wenye watoto tunaona Bora watoto wetu tukae nao wenyewe kwa maana ya kujikinga na kuwakinga.

Jukumu la mwanao ni la kwako usitake kuitwika serikali mzigo.

Kila mtu abebe mzigo wake.

Mitihani na masomo vimebuniwa na wanadamu. Uhai wa watu sio wa kufanyiwa majaribio.

Halafu nyie ndio wakiachwa mashuleni badae wakapata maambukizi mnaanza kulaumu serikali.

Hebu waswahili acheni ujuaji usio na maana kwenye maswala nyeti. Serikali wanahaha kujaribu kuona ni hatua gani wananchi wake watapata ahueni wewe unaletamasihala.

Hongera serikali kwa kutanguliza uhai wa raia kwanza, mengine yataangaliwa baadae Akilitime,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukishatoa uamuzi wa kufunga tayari ni gharama ambayo huwezi kuifidia mpaka tatizo liishe.Kwa ufupi kanuni iliyotumika ipo sawa, kusogea kwa ratiba ni bora kuliko maafa.Ni rahisi kumudu kuelekeza familia ila sio watu waliopo shule au chuo hususan kwa tatizo kama hili..
 
Duh, umewaza vizuri ila walishafanya maamuzi ukisema watengue tena itakuwa balaa, usambazaji utaongezeka coz watatoa huko na kupelek kule. Tutulie tu tuone muafaka,.
 
Kabisa
Kidato cha sita wapo mtaani na wanapepa mei,warudi darasani
Kweli kabisa.
Kidato cha sita ratiba ifatwe kama ilivyopangwa.wapewe wiki moja warudi shuleni,kwakuwa taharuki ya hao wagonjwa 6 ilipekekea serikali act immediatelly.
 
Back
Top Bottom