Mh. Waziri Mkuu Usikwepe Majukumu

Amanikwenu

Senior Member
Dec 1, 2009
187
0
Wiki iliyopita wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam walifikisha ujumbe maalum kwa njia ya mabango kwa Waziri Mkuu kuwa wanalala nje. Hii ilitokea wakati Waziri Mkuu akishiriki katika ufunguzi wa sherehe za miaka 50 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambazo zitafikia kilele chake siku ya tarehe 25.10.2011. Cha ajabu wakati wa hotuba yake WM hakuongelea tatizo hili na nini ufumbuzi wake.

Hali ya Malazi katika chuo hiki inatisha kwani zaidi ya wanafunzi 10,000 hawana uhakika wa kupata malazi hapo chuoni au katika hosteli zake nyngine kama vile Mabibo. Mbaya zaidi ni kuwa vyuo vyote vikuu hapa nchini, ukiachilia UDOM, havina nafasi za malazi za kutosha kwa ajili ya wanafunzi.

Ukiangalia suala la malazi katika chuo kikuu cha Dar es Salaam utaona kuwa ukiacha Mabibo Hosteli, Hall la mwisho kujengwa hapo chuoni ni Hall 7 ambalo lilijengwa miaka ya 80 mwanzoni.

Kinachotakiwa kutatua tatizo hili ni kwa Serikali kutenga bajeti kila mwaka kwa ajili ya ujenzi wa Hosteli za Wanafunzi kila mwaka katika vyuo vyetu. Serikali inaweza kupata fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hosteli za Wanafunzi kwa kukopa toka katika mifuko yetu ya hifadhi ya jamii na pesheni. Kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam chini ya usimamizi mzuri na matumizi mazuri ya fedha shilingi bilioni 50 zinatosha kabisa kutatua tatizo hili. Ukitumia kiwango hiki cha fedha una uhakika wa kupata vyumba visivyopungua 10,000 vyenye ukubwa wa mita za mraba 10 kwa kila chumba kimoja na kila chumba kikiwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi wanne kama ilivyo kwa chuo kikuu cha Dodoma. Kama kwa Chuo Kikuu cha Dodoma imewezekana kwa nini isiwezekane kwa vyuo vingine.
 
Hawataki kujenga vingine ili kutoa mwanya kwa wenye nafasi kuuza vyumba kwa bei ghali kweli!
 
Naogopa kusema ukweli atalia, unafiki sio mzuri unakataa shangingi eti ni matumizi mabaya yet unaruhusu mtendaji wako alitumie si unafiki huo??? Pinda alitakiwa atoe tamko wambie huu ni ubadhilifu rudisheni yalikotoka yote sio lake tu, 280million mara 50 ministers, bado makatibu wakuu, bado wakurugenzi, bado wakuu wa mikoa, hii kweli nchi tajiri
 
Hali ya Malazi katika chuo hiki inatisha kwani zaidi ya wanafunzi 10,000 hawana uhakika wa kupata malazi hapo chuoni au katika hosteli zake nyngine kama vile Mabibo.

Malazi chuoni (hasa UDSM) ni time bomb. Watu wanalala wawili-wawili (almaarufu kubebana). Yaani chumba kimoja kina-accomodate MARA MBILI ya idadi ya watu waliopaswa kukaa mle. Many thanks to Engineers kwa kuweka ''safety factor'' wakati wa kudesign maana yale majengo yangeshaporomoka siku nyingi sana!!

Sintoshangaa lakini siku hall 5 likianguka!
 
sina la kusema mimi,sitaki kulia bureee ila najua wanataka tuki graduate tuwe watu wa namna gani kazini/serikalini
 
Pinda hana ubavu wa kuwabana watendaji serikalini ameshadhihirisha mara nyingi..
Nadhani wanasubiri Hall 2 lianguke ndo waje na mipango ya zimamoto...
 
Malazi chuoni (hasa UDSM) ni time bomb. Watu wanalala wawili-wawili (almaarufu kubebana). Yaani chumba kimoja kina-accomodate MARA MBILI ya idadi ya watu waliopaswa kukaa mle. Many thanks to Engineers kwa kuweka ''safety factor'' wakati wa kudesign maana yale majengo yangeshaporomoka siku nyingi sana!!

Sintoshangaa lakini siku hall 5 likianguka!

Ni kweli usemayo. Naona kama vile Serikali imekata tamaa baada ya kura kupungua kupita kiasi.
 
Hivi kuna watu bado mnamwona Pinda kuwa ni waziri mkuu? huku sumbawanga tulishafuta, Tanzania hatuna waziri mkuu, hata yeye mwenyewe analijua hilo. Huyo jamaa ni boya tu, ni kipaza sauti cha mafisadi.
 
Kama una ubavu mhe. Pinda yarudishe magari yote na upige marufuku kununua magari!!!!!!!!!!!!hapo nitakuona mwanaume!!!!!!!!!!!!!!!! Tena wa shoka na mtoto wa mkulima kweli.
 
Kama una ubavu mhe. Pinda yarudishe magari yote na upige marufuku kununua magari!!!!!!!!!!!!hapo nitakuona mwanaume!!!!!!!!!!!!!!!! Tena wa shoka na mtoto wa mkulima kweli.

Pinda hana ubavu huo,usipoteze nguvu zako bure.Yeye kazi yake ni kutoa ushauri tu, which you can take or leave.Halafu do you know, uwaziri mkuu wa Tanzania ni ceremonial!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom