Mh. Dada kamata, hakuna jambo lililo nishtua kama wewe kusema wimbo wa 'Mageuzi usiniguse nimeolewa' umeimbwa na wanawake WOTE Geita. Nipo mbali na geita ila nina jamaa wengi huko nimejipa muda kuwauliza kama kweli mliandika au kutunga pamoja wimbo huo. Wote nilioongea nao wamekataa kwa uchungu kuwa umewaongopea! Nimeongea na Ng'wanasabuni wa kijiji cha Lubanga amekataa na amesema hata hakujui ila aliwahi kusikia una hela nyingi wakati wa uchaguzi kuliko wanawake wote waliogombea na wewe, Balizukwa wa Shibalanga nae amekana kuhusika kutunga nawe wimbo huo, Katalina wa Nyarugusu Tologo nae amekataa kabisa kuhusika. Sikuchoka, nikamuuliza hata Diwani wa viti maalumu CCM Bi Stella wa Nyijundu amedai wimbo wako aliupenda ila alisema mahusiano yake na CCM ni ya kati ya chama na mwanachama na si ya ki-ndoa kama uivyodai. Nimezungumza pia na Roza wa Butundwe yeye amesema ukome kuwasingizia wanawake wa Geita. Nikajiuliza umepata wapi nguvu ya kusema hadharani ni wimbo wa wanawake wote wa Geita nikaona pengine UWT Geita ndio mliotunga wote wimbo huo, nikamuuliza M/kiti wa wa Jumuia hiyo Bi Zaituni nae amesema hajui na akaishia kukupongeza ulivyo cheza jukwaani.
Kwanafasi yako dadangu kusema uongo na hasa wa kusingizia ni hatari. Wengine Geita tuna mama zetu,dada zetu, shangazi zetu kutangaza hadharani kuwa wote wameolewa na CCM ni kuhatarisha ndoa zao bila sababu.
Ingetosha kama Ungesema tu 'wimbo huu ni wangu wenzangu na mimi nauimba kwa niaba ya wanawake tunaoolewa na CCM, isingeleta tabu zote hizi.
Kwanafasi yako dadangu kusema uongo na hasa wa kusingizia ni hatari. Wengine Geita tuna mama zetu,dada zetu, shangazi zetu kutangaza hadharani kuwa wote wameolewa na CCM ni kuhatarisha ndoa zao bila sababu.
Ingetosha kama Ungesema tu 'wimbo huu ni wangu wenzangu na mimi nauimba kwa niaba ya wanawake tunaoolewa na CCM, isingeleta tabu zote hizi.