MH.Utawala Umekushinda?Tulipe Tshs100 Kwa Kipi Mlichoboresha?Kiama Chenu 2010!

Kevo

JF-Expert Member
Jun 12, 2008
1,333
52
WATOTO wetu wamefanya kile ambacho sisi wazazi wao tumeshindwa, na badala yake tumeishia kufanya kile watoto hao wanachoweza kusema ni kukalia politiki tu.

Watoto wetu hawa wanaosoma shule za msingi na za sekondari za Dar es Salaam wameandamana kupinga wanachoona si halali kwao. Kitu hicho ni ongezeko la nauli ya mwanafunzi kutoka Shilingi 50 hadi Shilingi 100 kwa safari moja.

Wameweza kujiratibu na kuandamana siku mbili tu baada ya ongezeko hilo kutangazwa. Ukilinganisha na idadi ya wanafunzi wote wa jiji la Dar es Salaam, walioandamana hawakuwa wengi lakini wamefikisha ujumbe kwa watawala.

Najiuliza mno, na kuogopa, ingekuwaje iwapo wangepata mwezi mzima wa kujiandaa.

Ni 'Mene mene tekeli na peresi', maandishi ukutani ambayo kwa hakika watawala wetu wanapaswa kuyasoma na kuyatafutia ufumbuzi haraka iwezekanavyo.

Walichothubutu kufanya watoto wetu ni ushahidi kamili na wa wazi kabisa kwamba hiki ni kizazi ambacho hakitakuwa na ukondoo uliowakuta wazazi wao uliobatizwa jina refu la 'amani, uvumilivu na mshikamano wetu'.

Kuna somo hapa. Watoto wetu wamethubutu kuandamana wakati walimu wao wameipa serikali siku sitini kukamilisha madai yao ama sivyo wataitisha mgomo wa walimu nchi nzima. Tumeambiwa kuwa wanajazishana fomu ili kujua idadi ya watakaokuwa tayari kujiunga na mgomo.

Hii sio mara ya kwanza walimu kutishia kugoma. Wameshafanya hivyo mara nyingi tu huko nyuma; lakini kila mara maneno mazuri ya viongozi wa Serikali yameweza kuwashawishi 'warudishe majeshi nyuma'. Labda safari hii wamepania kikweli kweli. Pengine ndio maana wanajazishana fomu ili kupembua mchele na pumba miongoni mwao.

Watoto wetu wameandamana kuonyesha kutokubaliana kwao na nauli mpya waliyotangaziwa. Wamepigana vita inayopaswa kuwa ya wazazi wao. Ni bahati mbaya tu kwamba wamepata jibu lile lile ambalo wazazi wao walio wafanyakazi na kaka na dada zao wa vyuo vya elimu ya juu wamekuwa wakipewa na watawala kila walipotishia kugoma ama kuandamana.

Tusifike huko. Ni vyema watawala wakasoma alama za nyakati 'zinazoandikwa' na watoto wa shule na wananchi wengine wa kada mbalimbali na kufanya kile jamii inachotegemea kutoka kwao badala ya visingizio hafifu vya 'kuna watu wanawatumia'.
 
Kama Wanafunzi wamejimobilize ndani ya siku mbili na kuitikisa Serikali hii inaonyesha kizazi cha leo kimeshaachana na ubwege tuliobaki kuamka ni sisi wazazi na kufanya mabadiliko maana tumekuwa so immobile and actually done nothing.
Kama walimu wanadangywa kidogo tuu wanatulia eti kisa Kikwete shemeji yao huo ushemeji uekwe pembeni watu wafanye kazi!
 
The Driving Force For A Revolution Is Underway!The Whole Nation Is About To Get Into The Streets And Demand For Their Rights................!
 
Haya ndio yaliyotokea!

attachment.php


attachment.php


attachment.php


Picha kwa hisani ya Father Kidevu - (http://mrokim.blogspot.com)!

Serikali hii ina kazi kweli kweli!
 
The Driving Force For A Revolution Is Underway!The Whole Nation Is About To Get Into The Streets And Demand For Their Rights................!

Absolutely!! I fully agree, these students are the voters in 2010 general election....
 
Absolutely!! I fully agree, these students are the voters in 2010 general election....

Lets hope and pray that for sure 2010 ndio kiama cha CCM maana it is easier said than done kabla takrima haijapewa jina jipya na watu waanzae kugawiwa kanga,pilau na soda maana nchi hii kweli kichwa cha mwendawazimu!
 
WATOTO wetu wamefanya kile ambacho sisi wazazi wao tumeshindwa, na badala yake tumeishia kufanya kile watoto hao wanachoweza kusema ni kukalia politiki tu.

Watoto wetu hawa wanaosoma shule za msingi na za sekondari za Dar es Salaam wameandamana kupinga wanachoona si halali kwao. Kitu hicho ni ongezeko la nauli ya mwanafunzi kutoka Shilingi 50 hadi Shilingi 100 kwa safari moja.

Wameweza kujiratibu na kuandamana siku mbili tu baada ya ongezeko hilo kutangazwa. Ukilinganisha na idadi ya wanafunzi wote wa jiji la Dar es Salaam, walioandamana hawakuwa wengi lakini wamefikisha ujumbe kwa watawala.

Najiuliza mno, na kuogopa, ingekuwaje iwapo wangepata mwezi mzima wa kujiandaa.

Ni 'Mene mene tekeli na peresi', maandishi ukutani ambayo kwa hakika watawala wetu wanapaswa kuyasoma na kuyatafutia ufumbuzi haraka iwezekanavyo.

Walichothubutu kufanya watoto wetu ni ushahidi kamili na wa wazi kabisa kwamba hiki ni kizazi ambacho hakitakuwa na ukondoo uliowakuta wazazi wao uliobatizwa jina refu la 'amani, uvumilivu na mshikamano wetu'.

Kuna somo hapa. Watoto wetu wamethubutu kuandamana wakati walimu wao wameipa serikali siku sitini kukamilisha madai yao ama sivyo wataitisha mgomo wa walimu nchi nzima. Tumeambiwa kuwa wanajazishana fomu ili kujua idadi ya watakaokuwa tayari kujiunga na mgomo.

Hii sio mara ya kwanza walimu kutishia kugoma. Wameshafanya hivyo mara nyingi tu huko nyuma; lakini kila mara maneno mazuri ya viongozi wa Serikali yameweza kuwashawishi 'warudishe majeshi nyuma'. Labda safari hii wamepania kikweli kweli. Pengine ndio maana wanajazishana fomu ili kupembua mchele na pumba miongoni mwao.

Watoto wetu wameandamana kuonyesha kutokubaliana kwao na nauli mpya waliyotangaziwa. Wamepigana vita inayopaswa kuwa ya wazazi wao. Ni bahati mbaya tu kwamba wamepata jibu lile lile ambalo wazazi wao walio wafanyakazi na kaka na dada zao wa vyuo vya elimu ya juu wamekuwa wakipewa na watawala kila walipotishia kugoma ama kuandamana.

Tusifike huko. Ni vyema watawala wakasoma alama za nyakati 'zinazoandikwa' na watoto wa shule na wananchi wengine wa kada mbalimbali na kufanya kile jamii inachotegemea kutoka kwao badala ya visingizio hafifu vya 'kuna watu wanawatumia'.


Kevo, Good! Lakini nadhani unatakiwa kumpa credit mtoa hoja hiyo ambayo kama sikosei ipo kwenye current issue ya gazeti la RAIA MWEMA!
 
Kevo nimeipenda hiyo... naomba kuitumia kwenye kijarida attribute to JF na Kevo of course.


Mkuu, heshima yako! Kama nilivyomuambia kevo hapo juu. Hiyo kauli imo kwenye makala iliyoandikwa na muandishi mmoja kwenye current issue ya gazeti la RAIA MWEMA word by word. Aren't you supposed to give credit to someone when you use his/her work?? just a though.
 
Hivi kwa nini wanafunzi wa skuli za Zenj hulipa nauli ya mtu mzima kwenye daladala, huku Tz Bara wanafunzi hulipa chini ya robo ya nauli ya mtu mzima?
 
Naona Kuna Watu Wanahalalisha Maandamano Ya Wanafunzi Yale Siku Zile , Napenda Kuwahakikishia Kwamba Watoto Hao Na Jamaa Zao Wengine Waliowashauri Waandamane Wamevunja Sheria Za Nchi , Wakati Mwingine Itatumika Nguvu Zaidi Kuwanyamazisha Wao Na Wengine Wote Ambao Wanafikiri Kwamba Sasa Ni Wakati Wao Wa Kuitukana Na Kuitusi Serikali Iliyochaguliwa Na Wananchi Kidemocrasia
 
Naona Kuna Watu Wanahalalisha Maandamano Ya Wanafunzi Yale Siku Zile , Napenda Kuwahakikishia Kwamba Watoto Hao Na Jamaa Zao Wengine Waliowashauri Waandamane Wamevunja Sheria Za Nchi , Wakati Mwingine Itatumika Nguvu Zaidi Kuwanyamazisha Wao Na Wengine Wote Ambao Wanafikiri Kwamba Sasa Ni Wakati Wao Wa Kuitukana Na Kuitusi Serikali Iliyochaguliwa Na Wananchi Kidemocrasia

hapana that is so unmerited of you!Mind you hawa waliondamana na hao waliowa support ni walalahoi ambao wanauchungu na nchi hii!serikali iliona na kuheshimu maandamano yao no wonder wakapunguza nauli yao sasa kama wewe unaona whatever they did was claptrap I guess you are mistaken and out of line!
 
Lazima walipe kwa sababu shule zipo kila kata sasa kwa nini unapeleka watoto wako shule ya mbali????umependa mwenyewe kumtesa mwanao.
 
Naona Kuna Watu Wanahalalisha Maandamano Ya Wanafunzi Yale Siku Zile , Napenda Kuwahakikishia Kwamba Watoto Hao Na Jamaa Zao Wengine Waliowashauri Waandamane Wamevunja Sheria Za Nchi.

Nadhani ifike wakati kila mzazi awajibike na malezi ya mwanae, mzazi asiyeweza kupata 4000/= kwa mwezi ya nauli ya mwanae anawezaje kumpa mtoto huyu malezi bora!

Mkapa alifanya makosa kuondoa karo za shule, sasa inaonekana wajibu wa kulea watoto nilaserikali nasio la mzazi husika.

Kama watoto hawaoni umuhimu wa elimu hadi kumuua mwalimu wanidhamu, wanakunywa pombe za kienyeji na kupiga watu. Hakuna haja ya kutoa elimu yabure! acha kila mzazi amhangaikie mwanae.
 
Back
Top Bottom