Mh Sumaye tunakukumbuka

zumbemkulu

Member
Dec 6, 2013
52
5
Kwa hali ilivyosasa tunakukumbuka waziri mkuu mstaafu Mh Sumaye katika kipindi chako kizima kuanzia 1995-2005 katika kuweza kusimamia vizuri serikali kama mtendaji mkuu na kuhakikisha nidhamu na maadili ya viongozi kama mtendaji mkuu wa shughuli za serikali .
 
Mafanikio ya kiongozi yeyote yule ni kuwa na msaidizi mchapakazi,mkweli na muwajibikaji hivyo utendaji wa Mh Sumaye ndio ulimfanya aweze kumsaidia mh Mkapa katika kipindi chote cha utawala wao
 
Utendaji wake na uimara wake katika serikiali pindi akiwa mtendaji mkuu wa serikali ndio unaweza kimpa nafasi kama atayangaza kuwania nafasi nyingine,kwasababu watanzania waliweza kimwamini katika nafasi ya PM na kuweza kufanya kazi hivyo sina shaka na utendaji wake wa kazi
 
sema namkumbuka siyo tunakukumbuka maana mi sioni cha kumkumbuka zaidi ya ufisadi tu
 
wengi humkumbuka kwa juhudi zake na utendaji mahiri wa kazi yake wakati wa uongozi wake kuwa na askari wa mwamvuli wenye weledi na wachapakazi ndio humpa zaidi nafasi ya kukumbukwa na watanzania walio wengi
 
Binafsi sioni la maana alilofanya na alipoteza mwelekeo kwa kumshauri Mkapa auze viwanda vyote na nyumba za serikali tulizojenga kwa kodi zetu kwa ushirikiano na Mwalimu Nyerere kwa bei ya toilet-paper. Leo hii vijana wetu wasingehangaika kutafuta ajira kama siyo yeye na akili zake fupi. Shame on him huyu bwana- shamba!
Ipo wapi kiwira coal mining na mashamba ya Nafco alojigawia na kuyageuza mapori? Angalia, tulikuwa wa kwanza duniani kusafirisha na kuuza mkonge, leo hii yako wapi?
Usiwe unamsifia tu mtu eti kwa kuwa aliwanyima habari na uwazi wa yalikuwa yanatendeka serikalini. Kwangu mie ni shetani tu anajivika sura ya malaika! Hana na hatopata nafasi ya kutuongoza tena nchi hii kwani hayajamtosha aliyotufanyia?
Sidanganyiki!
 
Yapo mengi amefanya kama uwanzishwaji wa mfuko wa maendeleo wa TASAF vijijini yeye ndio aliyeshauriana na wenzake pindi akiwa mtendaji mkuu wa serikali na leo hii tunaona matunda yake juu ya mpango huu
 
yapo mengi amefanya kama uwanzishwaji wa mfuko wa maendeleo wa tasaf vijijini yeye ndio aliyeshauriana na wenzake pindi akiwa mtendaji mkuu wa serikali na leo hii tunaona matunda yake juu ya mpango huu

mkapa ndiye wa kukumbukwa kwa utendaji si fsadi sumaye
 
Mh sumaye hajaliibia Taifa hili,utumishi wake na utendaji wake ndio ishara ya kuwa alikuwa na hofu ya mwenyezi mungu juu ya mali za umma angaliweza kujilimbikizia mali katka kipindi chote cha utawala wake lakini hakuwa na sababu ya kuliibia Taifa hili
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom