Mh. Suleiman Ali Bungala Mbunge wa Kilwa Kusini (CUF)

MWILI NYUMBA

JF-Expert Member
Jun 18, 2012
817
255
Kwa wale tuliobahatika kutazama kipindi za jioni cha Bunge la Bajeti leo basi mtaungana na mimi kutaka kumfahamu huyu Muheshimiwa hasa kutokana na mbwembwe zilizopita kiasi anazotumia Mbunge huyu katika kuwasilisha hoja. Kwakweli amewachana vya kutosha CCM juu ya kusuasua kwa ujenzi wa Barabara kuu ya kusini na hoja zake nzito.

Ningependa kumfahamu zaidi huyu Muheshimiwa kama uwajibikaji wake kwenye jimbo analolitumikia, maoni juu ya kuendelea kwake kuwepo kwenye bunge kwa awamu ijayo ya kuanzia 2015, CV yake, jinsi alivyopenya kwenye uchaguzi wa mkuu wa mwaka 2010 nakadharika. Kwa mwenye kumfahamu huyu kwa undani please hebu tupashe kidogo na sisi.
 
Ooyooo naona hiyo si tena barabara ni barabara ya kwenda ahera hiyo ni toka lini barabara ikajengwa toka awamu ya kwanza hadi laana ya leo bado tu
 
Inasikitisha sana mkuu, gesi kutoka mtwara wameweza kuisafirisha mpaka dar kwa mwaka mmoja tu lakini hiyo barabara nasikia huu ni mwaka wa sita km 60 hazijakamilika.Hebu ccm muone haya jamani duh
 
...kwa taarifa nilizonazo juu ya huyo Mh Bungala,alipita kwa nguvu ya umma,baada ya CCM kumpitisha Mzee Madabida kama mgombea wao,ili hali wananchi walikuwa wakimuhitaji mbunge aliyekuwepo, ambaye walikuwa wanaimani nae kwa namna alivyokuwa akiwapigania.

Filimbi ilipopulizwa wananchi wakaonyesha nguvu yao,..ni kama ilivyokuwa Iringa mjini kwa Mh Msigwa na Bukombe kwa Prof Kahigi,...Bungala huyooo bungeni,,,Kiukweli hata mimi huwa ananivutia sana
 
Elimu yake ni darasa la saba ,jimboni kwake hakuna kinachofanyika ,pia inasemekana alishawahi kurukwa na akiri
...kwa taarifa nilizonazo juu ya huyo Mh Bungala,alipita kwa nguvu ya umma,baada ya CCM kumpitisha Mzee Madabida kama mgombea wao,ili hali wananchi walikuwa wakimuhitaji mbunge aliyekuwepo, ambaye walikuwa wanaimani nae kwa namna alivyokuwa akiwapigania.

Filimbi ilipopulizwa wananchi wakaonyesha nguvu yao,..ni kama ilivyokuwa Iringa mjini kwa Mh Msigwa na Bukombe kwa Prof Kahigi,...Bungala huyooo bungeni,,,Kiukweli hata mimi huwa ananivutia sana
 
Back
Top Bottom