TANZIA Mh. Regina Rweyemamu, Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania afariki Dunia

Moja wapo ya majaji waliokua na mchango mkubwa katika mahakama kwa kutoa maamuzi mbali mbali ambayo yalitumika katika kutoa maamuzi mengine (precedent)

Mchango wake katika mahakama kuu divisheni ya kazi unatambulika.
 
View attachment 1701387
Mahakama ya Tanzania inasikitika kutangaza kifo cha Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Regina Rweyemamu aliyefariki dunia leo asubuhi katika hospitali ya Kitengule iliyopo Tegeta jijini Dar es salaam.

Msiba wa Jaji Mstaafu Rweyemamu uko nyumbani kwake Mbweni jijini Dar es salaam.

Mahakama ya Tanzania inatoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki kufuatia msiba huu.

Taarifa Zaidi kuhusiana na msiba huu zitapatikana baadaye.

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA, JINA LAKE LIHIMIDIWE.
Mama si aliwahi kuwa Kamishna wa kazi huyu....Kama Ni yeye kwa life style yake kifua hakikuwa na Afya...msisinguzie mengine!
 
Mama si aliwahi kuwa Kamishna wa kazi huyu....Kama Ni yeye kwa life style yake kifua hakikuwa na Afya...msisinguzie mengine!
Naona unatafuta mazingira uweke umbeya, life style gani tena na ya nini hapa!
 
Kaazi kweli kweli. Jinsi tunayo angamia kwa kukosa maarifa.
Yaani Mungu asitimize yake,eti tunaangamia kwa kukosa maarifa! Alipangalo Mungu hakuna wakulitenguwa hata ukiwa na maarifa bakuli tele!!
 
sasa kwanini unachukia watu wakitangaza vifo vya wapendwa wao. kama hutaki kusikia au kuona matangazo kama hayo basi jitoe kwenye mitandao ya kijamii
Sasa si mpeleke matangazo yenu kule Redio one kwa Marehemu Mengi!!
 
Back
Top Bottom