Mh. Rais, Wizara ya Afya ni ka "Empire" ka Madaktari, Kuna "Mfumo Daktari" Ulioota Mizizi

Nobunaga

JF-Expert Member
Mar 22, 2019
1,169
4,985
Kwanza kwa heshima na taadhima nakusalimu na kukupa pole Mh. Rais kwa kazi nzito ya kuwaongoza Watanzania na taifa kwa ujumla.

Mimi sio mwandishi mzuri sana Mh. lakini naomba nikupe hints chache tu ili ujue na watu wajue ni kwa jinsi gani humo wizara ya afya kuna ki empire kimejengwa ambapo kwa namna moja ama nyingine kina negative impacts kwa jamii.

Kwanza kwenye wizara, nafasi za juu pale, yani top layer karibia yote wameshikilia Madaktari, hakuna kada nyingine japokuwa wana vigezo sawa na hao Madaktari.

Tukiachana na waziri pamoja na naibu wake ambazo ni nafasi za kisiasa (lakini wote ni Madaktari), nafasi zingine za juu pale wizarani zimekaliwa na Madaktari pia. Directors karibu wote ni Madaktari.

Ukija kwenye hospitali zote pia wakuu wake wanakuwa ni Madaktari. Sidhani kama kuna hospitali hapa nchini mkuu wake ni kada tofauti na udaktari. Mh. tukumbuke uongozi ni nafasi ya kuteuliwa haihitaji uwe umesomea kada fulani bali uwe na ujuzi na uwezo wa kuongoza. Lakini huko mahospitalini automaticaly Madaktari wameshajiwekea dhana kwamba wao ndio wanapaswa kuongoza hospitali. Hakuna cha muuguzi, mfamasia wala mtaalamu wa maabara anayeruhusiwa kuongoza hospitali hata awe na sifa sawa na daktari.

Sio kwamba napinga wao kuwepo hapo, hapana. Ila najaribu kuwaza tuu ina maana kada zingine hamna wenye vigezo vya kushika hizo nafasi mpaka wao tuu washike.

Huu mfumo umepelekea maamuzi mengi sana yanafanyika kwa upendeleo na Madaktari wanapeana favor zaidi kupita kada zingine. Angalia hata nafasi za kusoma level za juu wanaopata ufadhili wengi ni Madaktari.

Pili, kutokana na "mfumo daktari" huu hapo wizarani, umepelekea wao kujiamulia mambo wanavyotaka bila kuogopa sababu wanajua hapo juu yupo wa kuwatetea hivyo hawagusiki.

Mathalani, ukienda hospitali nyingi za umma kwenye inpatients wards Madaktari hawakai kabisa. Wakishapita ward rounds ile asubuhi kufika saa sita wanakuwa wameshapotea wanabaki wauguzi tu. Hata ikitokea dharura yeyote wanaohangaika na mgonjwa ni wauguzi, na wagonjwa wengi sana wanafariki bila daktari kuwepo, mgonjwa akishafariki ndio daktari anaitwa kuja kuidhinisha kifo na sio kumuokoa mgonjwa. Mida ya usiku ndio hali ni mbaya zaidi kwani hata daktari akiitwa kuja ni mpaka asubuhi.

Tukija kwenye scenario ya huyo daktari aliyekimbia hapo Tabora na kwenda Dar, kwanza kwa upande wangu Mh. naona kama amefanya fair kuweka wazi kaacha kazi. Mh. Rais naomba utambue 80% ya Madaktari wa hospitali za umma wana vijiwe.

Na hivi vijiwe ndiyo wanavipa priority zaidi kuliko vituo vyao rasmi vya kazi. Asubuhi wakishapita round huko vituo vyao vya kazi basi kuanzia mida ya saa nne/tano wanaenda huko vijiweni (private hospitals) ambako wanakaa full-time. Sasa mimi naona bora huyu aliyeacha kabisa kuliko hawa wanaoendelea kula kodi zetu kwa geresha tuu huku muda mwingi wakiutumia huko private.

Pia hawa Madaktari kingine kibaya zaidi wanachofanya huwa ni kuhama na wagonjwa kutoka hospitali za umma na kwenda nao huko vijiweni kwao. Mfano anaweza kuja mgonjwa kwenye hospitali ya umma akaonwa na daktari, lkn ataambiwa kwa vipimo na huduma kamili tuonane siku fulani kwenye hospitali fulani. Wakati anachoenda kufanyiwa huko private hospital pia kinafanyika kwenye hiyohiyo hospitali ya umma. Wanachoahidiwa huko private ni kwamba ukileta mgonjwa basi unakuwa na "cha juu".

Lakini haya yote hakuna wa kuyachukulia hatua madhubuti sababu kwenye uongozi mzima wameshikilia wao kuanzia wizarani mpaka huku chini kabisa. Hawa kada zingine hata wakijaribu kupeleka malalamiko wanaishia kuzimwa maana kote kuna "mfumo daktari".

Hivyo Mh ukitaka kuiponya hii sekta ya afya anza na kuvunja vunja huu "mfumo daktari" kwanza ndio tutapiga hatua kwenye hii sekta.

Ni hayo tuu kwa sasa Mh. Rais.

________________________

1. Sina 'farasi' kwenye mtifuano huu.

2. "Nasikia" zamani Madaktari walikuwa wakipenda Waziri wa Afya awe mtu ambaye "siyo" daktari (MD) kwa vile huwa "mnyumbufu" zaidi katika kushughulikia masuala yanayohusu madaktari. Sijui siku hizi kukoje.

3. "Nasikia" hospitali fulani iliwahi kuleta mkuu wa hospitali Mzungu. Ukazuka mjadala wa kwanini/kwinini ;) . Wakaambiwa tunataka mtu mwenye digilii ya "Hospital Management". Hakuwapo kwa wakati huo, na Mzungu akapeta!

4. "Mfumo-Daktari" kwenye afya; "Mfumo-Wahadhiri" kwenye taasisi za elimu ya juu; "Mfumo-Mwanasheria-Msomi" kwenye kada za kisheria; "Mfumo-Wahandisi" kwenye baadhi ya kada, pengine ni vitu ambavyo vipo. Tatizo kubwa Afrika ni "Menejimenti". "Menejimenti" haijaweza bado kuonekana ni fani inayojitegemea, na kwamba mtu yoyote aliyeweza kufikia viwango vya vigezo na masharti ya "Menejimenti" angeweza kuonekana sawa na mwenzie aliyetimiza vigezo na masharti --- bila kujali ilmu zao za awali. Pana taasisi mashuhuri iliwahi kuletewa "Menejimenti" nzima ya kukodishwa ili kuboreshwa. Hili ni jambo la kawaida kutokea baadhi ya taasisi, hasa nchi za mbali. "Management-For-Hire".

Hitimisho: "Kasungura" kenyewe kadogo :( ... kila mmoja anataka aweko "jikoni" kwenye kazi ya "kutenga" kwenye "sahani" nani apate nini, lini na kwa nini. Menejimenti kama utaalam (Profession) iheshimiwe -- nafasi za menejimenti zisijali kwanza kuhusu usuli wa taaluma ya mtu, kabla ya kuangalia Utaalam wa Menejimenti.
Mkuu kwanza neno MEDICAL halina maana ya "Udaktari"

Mwanafunzi aliyehitimu masomo yake ya "Udaktari" ambaye ana degree yake moja huyo kiufasaha kabisa katika kada ya afya anatambulika kama GENERAL PHYSICIAN (GP)

GP ndo title sahihi kabisa ya madaktari wetu ambao wana wamemaliza masomo yao ya degree ya kwanza na jukumu lao kubwa ambalo linawatofautisha na kada zingine ni ubobezi katika kufanya diagnosis.

Kiufupi Kada za afya zina compliment to each other.. Yaani kila kada inamtegemea mwenzake kwa huduma bora zaidi za afya.. Ndo maana kuna term inayoitwa MEDICAL PERSONNEL ikimaanisha mjumuiko wa wataalamu katika mfumo Tiba.

Ukisema medical officer lazima awe daktari kwa kigezo cha uwepo wa neno medical katika iko cheo haupo sahihi 100%

Medical officer can be any medical personnel ambaye ana qualifications za hiyo post kwa mujibu wa taratibu ambazo wahusika wataona inafaa ila hauwezi kuipa hiyo post by default kwenda kwa madaktari kisa tu kuna neno medical ndani yake.
wale wahuni Hadi idara za preventive services wanajustify kuwa wao ndio wanafaa kuongoza kwa hoja ya kuwa huwezi kuzuia kitu ambacho kikitokea huwezi kukiondoa

Hadi idara ya epidemiolojia wanajustify kuwa huwezi kuongoza idara ya namna ya kudhibiti kuenea kwa magonjwa wakati hujui magonjwa

Hadi idara ya Tiba ya asili wanakuambia huwezi kuongoza idara ya Tiba ya asili wakati hujui Tiba

Hadi idara ya mafunzo watakuambia huwezi kuongoza idara ya mafunzo yenye mafunzo ya udaktari ndani yake wakati wewe hujausoma wakati wao wanasoma vyote vya Afya

Hadi idara ya elimu kwa umma wanakuambia huwezi kuongoza idara ya elimu ya Afya kwa umma wakati hujui afya ya binadamu vizuri kama wao

Hence

Idara zote wanaongoza wao isipokuwa zile ambazo zipo specific Kama idara ya uuguzi na ukunga,Idara ya madawa na vifaa tiba na idara ya rasilimali watu
 
'Wabena' wanasema "Well said" !

Wafamasia nadhani ndio kundi la wataalam wa Afya wasiotambulika kabisa Tanzania licha ya kuwa ni kada muhimu sana! Nchi kama USA Wafamasia wanawapiku Madaktari kwa kukubalika kwa wananchi! Tz muulize mtu kuwa Mfamasia anafanya nini hajui!
 
Hali ya kiuchumi ni tete kwa mtu binafsi ndio maana inakuwa hivyo na wakisema waanze hivyo kumbuka kuna madaktari bingwa mara nyingi hawana kituo maalamu lakini pia kuna maprofesa wanafundisha vyuo zaidi ya kimoja tusiwakandamize madaktari ata ungekua wewe ungefata masilahi.
 
Kuna Dr alikua na duka la dawa sasa alimweka muuzaja wa dawa hana elim ya dawa kiasi kwenye duka lake aliweka ad huduma ya sindano. Kuna mgonjwa alimwambia aende duka la dawa akachome sindano. Sasa yule mhudum hana elimu yoyote alimchoma mgonjwa akaanza kuishiwa nguvu ad akapoteza fahamu.
 
Unajisumbua bure kumpigia mbuzi gitaa.

Huyo Unayependa akusikiluze hajui chochote na hataki kujua, kuna siku MAT walikuwa na mkutano akaalikwa.

Akaishia kusema wataajiri madaktari 1,000 kwasababu wanasoma miaka 5, utafikiri madaktari watafanya kila kitu huko kwenye sekta ya afya.
 
Unajisumbua bure kumpigia mbuzi gitaa.

Huyo Unayependa akusikiluze hajui chochote na hataki kujua, kuna siku MAT walikuwa na mkutano akaalikwa.
Hivi vitu vinauma sana, ukisikiliza speech yake ya ile siku utadhani madaktari ndio wafanyakazi wa hospital pekee, na yote hayo ni mfumo ndio umepelekea hivyo, mwisho wa siku wasipofanyia marekebisho mambo yalivyo hovyo kwenye huo mfumo daktari watu watakuja kupigaba huko mahospitalini sababu ya ujinga uliopo.
 
'Wabena' wanasema "Well said"!

Wafamasia nadhani ndio kundi la wataalam wa Afya wasiotambulika kabisa Tanzania licha ya kuwa ni kada muhimu sana! Nchi kama USA Wafamasia wanawapiku Madaktari kwa kukubalika kwa wananchi! Tz muulize mtu kuwa Mfamasia anafanya nini hajui!
Yani hierrachy nzima ya wizara wameshika madaktari ndio matokeo yake haya.

Ukienda India kila hospitali ina kiwanda chake kidogo cha kutengeneza dawa, hakuna hospitali wananunua dawa nje na hapo. Hizi dripu na vizagavizaga vingine ni simple sana kutengeneza lkn nashangaa sijui tunakwama wapi.

Dripu nyingi tunazotumia hapa Tanzania zinatoka hapo Uganda tuu, pia niliwahi kuona Tumbi Hospital ya pale Kibaya mkoani Pwani wanatengeneza dripu zao.
 
'Wabena' wanasema "Well said"!

Wafamasia nadhani ndio kundi la wataalam wa Afya wasiotambulika kabisa Tanzania licha ya kuwa ni kada muhimu sana! Nchi kama USA Wafamasia wanawapiku Madaktari kwa kukubalika kwa wananchi! Tz muulize mtu kuwa Mfamasia anafanya nini hajui!
Mfamasia na doctor of medicine ni watu wawili tofaut doctor of medicine hawa ndio wanaobun madawa wana priority zaid hao mafamasia wanaklemishwa tu majina ya madawa tu nipe asprin ndio anachojua yeye.
 
Hivi vitu vinauma sana, ukisikiliza speech yake ya ile siku utadhani madaktari ndio wafanyakazi wa hospital pekee, na yote hayo ni mfumo ndio umepelekea hivyo, mwisho wa siku wasipofanyia marekebisho mambo yalivyo hovyo kwenye huo mfumo daktari watu watakuja kupigaba huko mahospitalini sababu ya ujinga uliopo
Mfano mimi nimesoma Environmental health sciences.

Sasa wewe unaelalamika kuwa Pharmacy inapuuzwa nikwambie hakuna kada sekta ya afya iliyopuuzwa kama hii.

Madaktari kwa kawaida huhusika na tiba, walivyokuja kugundua pesa nyingi za wafadhili huwa zinatarget kinga wakaamua kuhodhi mpaka huku.

Na kama hilo halitoshi wakaamua kumfanya daktari mkúu wa mkoa (RMO ) awe Daktari aliyesoma MPH ili akontrol kote.

Yaani Ukitaka kuona upuuzi, ukiwa nurse au pharmacist hata kama ni degree holder na daktari ni C.O yeye ndio boss wako na anakuelekeza cha kufanya
 
Mfamasia na doctor of medicine ni watu wawili tofaut doctor of medicine jawa ndio wanaobun madawa wana priority zaid hao mafamasia wanaklemishwa tu majina ya madawa tu nipe asprin ndio anachojua yeye
Hivi daktari na hao wafamasia ni nani wanabuni dawa? Au huyo doctor of medicine ni tofauti na daktari?
 
Mfamasia na doctor of medicine ni watu wawili tofaut doctor of medicine jawa ndio wanaobun madawa wana priority zaid hao mafamasia wanaklemishwa tu majina ya madawa tu nipe asprin ndio anachojua yeye

Uwezo wako wa kuandika unaonyesha wazi kiasi gani akili yako isivyoweza kujua hata nani anayetengeneza dawa na nani anahusika magonjwa kwa undani (In details).

Uliza uelimishwe.
 
Kuna vitu ni vigumu mno kuvibadili kimfumo, maana chimbuko lake lina mzizi mrefu kiutamaduni. Madaktari wana some sort of Superiority complex dhidi ya kada zingine za afya. Na kada zingine za afya zina inferiority complex mbele ya madaktari. Nahisi ni kitu kilichojijenga kijamii na kukuzwa darasani wakati wahusika wakiwa masomo.

Ni kama ilivyo kazi ya Askari jeshi (JWTZ) dhidi ya askari wengine kama Polisi, Magereza, Uhamiaji, wanyamapori nk.

Mtu wa kada nyingine yoyote ya afya(tofauti na udaktari) ni vigumu sana kuwaongoza madaktari, lakini ukiwa daktari (hata kama huna upeo, hekima wala ujuzi wa kiuongozi) ni rahisi sana kuwaongoza watu wengine wote katika sekta ya afya. Na popote hapa Tanzania walipogeuza hii hali, hali haikwenda vizuri, migogoro ya kiuongozi na kiutawala ilishamiri mnoo.

Ni rahisi mnoo kuitoa CCM madarakani kuliko kuwatoa madaktari katika mfumo wa utawala katika sekta ya Afya.
 
Mfano mimi nimesoma Environmental health sciences.

Sasa wewe unaelalamika kuwa Pharmacy inapuuzwa nikwambie hakuna kada sekta ya afya iliyopuuzwa kama hii...
Nchi za wenzetu kwenye hii sekta kuna boundaries za kazi zao, lkn hapa kwetu "mfumo daktari" umeshaimeza nchi kitu ambacho kina negative impacts kubwa sana hata kwenye maendeleo ya nchi.

Mfano tunaletewa chanjo na madawa yenye madhara kwetu sababu ya kushindwa kuwatumia wafamasia kutengeneza dawa na chanjo zetu.

Fedha nyingi zimeelekezwa kwenye kuwahudumia madaktari tuu, kwenye kusoma wanapewa priority wao tuu wakati kwa dunia ya sasa watu wameshatoka huko.

Kwa dunia ya sasa ilipaswa pesa nyingi zielekezwe kwenye viwanda vya uzalishaji dawa.
 
Kuna vitu ni vigumu mnoo kuvibadili kimfumo, maana chimbuko lake lina mzizi mrefu kiutamaduni. Madaktari wana some sort of Superiority complex dhidi ya kada zingine za afya. Na kada zingine za afya zina inferiority complex mbele ya madaktari. Nahisi ni kitu kilichojijenga kijamii na kukuzwa darasani wakati wahusika wakiwa masomo....
Sio kweli kada zingine wanashindwa kuongoza bali hawapewi support na wanakwamishwa makusudi ili "waonekani hawawezi".

Kumbuka from top to bottom wapo wao tuu hivyo kukukwamisha ni jambo la dakika sifuri tuu.
 
Mtoa mada pole sana, najua maumivu unayopitia hasa kwenye huo mfumo.

Doctor of medicine ni moja ya degree kongwe ambapo mtu akiwa tu na degree ya kwanza huitwa doctor,ambapo ni tofauti na degree nyingine nyingi sana ambapo hadi uwe na degree tatu ndio huitwa doctor,pia MD anauwezo wa kusoma master of science yeyote ile uliyowahi isiskia hapa duniani.

Miaka 5+,MD hufundishwa vitu vingi sana, yaani MD husoma kazi za nesi,za mfamasia,za maabara,na hadi za afisa afya.
MD unaweza muweka popote pale na akafanya kazi vizuri tu, lakini mtu wa maabara ukimpeleka theater utahitaji umfundishe kila kitu upya.

So pamoja na p MD anakua na degree sawa na wenzake lakini ki "academic"jua amewazidi sana,maana wenzako ni bado bachelor wakati yeye ni doctor.

Hata vigezo vya TCU MD haitaji kuwa na GPA ya 4 master ili kuwa lecturer,anahitaji tu kua na MMED baaasi,tofauti na degree zingine.
Halafu specialization za MD haziingiliani na zingine popote pale duniani,yaani ili uwe na higher medical education level/specialization ni lazima uwe MD.

Huu ni utaratibu tu wa dunia nzima ndio mana hata marekani among higher paying job ni MD ,hata Tanzania MD anaanza na mshahara mara mbili ya mwalimu mwenye masters.

Yaani pesa ambayo serikali inamkopesha MD kusoma kwa mwaka mmoja tu, unasoma degree ya environmental science miaka 3 hadi unamaliza na chenji inabaki.

Hawa watu hawawezi kua sawa. MD ana advantage ya kuziba nafasi za kada nyingine ya sayansi sababu yeye anaweza soma vitu vingi/master kwenye elimu yake ya juu.

Hata wewe uwe rais kati ya pharmacist mwenye PhD na MD mwenye PhD yupi utamchagua kua waziri wa afya?,kua mkweli hapa?
Kati ya environmental scientist mwenye PhD na MD mwenye PhD huku master ana MPH yupi utamchagua kua mkurugenzi wa Tiba pale wizara ya afya?

Yaani mfumo wa kidunia una mfavor zaidi MD kuliko kada ingine,haya mambo ni vema wanafunzi wangeyajua hata kabla ya kuanza shule.

MD ndio anamsababishi nesi,mtu wa maabara na famasia wafanye kazi.....yaani yeye ndio anainitiate matibabu,

MD anaweza toa huduma ya afya/kujikinga na magonjwa,wakati mtu wa environmental health hawezi toa huduma ya tiba
 
Chuki zako dhidi ya madaktari hazitakusaidia,nenda kasome na wewe kama unaona ni rahisi,iko miongozo inayoongoza...kwa hiyo ulitaka wewe uwe MOI,DMO au RMO...hujui unachoongea,narudia tena nenda kasome miaka 5,then 4 kama unafikiri ni kazi rahisi.
Sababu zenu ni zilezile miaka na miaka. Utasikia sisi tunasoma miaka mingi, sisi ndio tunatibu, sisi ndio wenye wagonjwa na blaah blaah nyingine nyingi zisizo na mashiko. Lkn naomba nikuambie dunia ya sasa imeshabadilika na hizo sababu zilikuwa za mwaka 90 kwa sasa zinapingwa kwa hoja nzito nzito.

Nilitegemea watu kama nyie mtajitokeza tuu.

Hatuwezi piga hatua kwa kuogopa kusema ukweli, ukweli utatuweka huru na tutapiga hatua.

Lkn huo "mfumo daktari" usipotolewa hii sekta haiwezi piga hatua.
 
Back
Top Bottom