Mh Rais sikia kilio cha vijana hawa wasomi waliojiajiri na kujenga kiwanda cha kuchenjua dhahabu

adb

Member
Sep 4, 2016
17
17


Ni vijana watano wahitimu wa vyuo vikuu waliojiajiri.

Safari yao ya ujasiriamali ilianzia kwenye kilimo. Mwaka 2015 walafanikiwa kusajili kikundi cha Nzega Agribusiness Association(NAA) wilayani Nzega. Walianza kwa kulima mtama mwekundu katika wilaya ya Igunga ambapo walilima jumla ya ekari 70 za zao hilo.
Wakiwa wameshatafuta soko tayari huku mtama ukiwa katika hatua za mwisho kuweza kuvunwa,walikutana na changamoto ya wafugaji kulisha shamba lao lote na hivyo kusababisha hasara kubwa kwa vijana hao. Pamoja na kuwakamata wahusika na kufungua kesi ya madai katika mahakama ya wilaya Igunga vijana hao walishindwa kesi kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao!!
Hii haikuwakatisha tamaa,na wala haikua mwisho wa safari yao ya ujasiriamali kwani mwaka 2016 waliamua kujiingiza katika sekata ya madini kama wachimbaji wadogo wa dhahabu wilayani Nzega. Msukumo huu waliupata baada ya serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mh Rais John Pombe Magufuli kuhakikisha rasilimali za nchi hasa madini zinawanufaisha watanzania kwanza.Walifanikiwa kuanza uchimbaji huo katika leseni ya watu wengine katika eneo la Mwanshina maarufu kama namba saba wilayani Nzega.
Kupitia uchimbaji huo,licha ya wao kua wamejiajiri,vijana hao pia waliweza kutoa ajira kwa vijana wenzao wapatao 19!Kwa uwezo wa Mungu walianza kuona mwanga katika uwekezaji huo kwa kuanza kupata mali. Kutokana na malengo yao na ufanyaji kazi wao kutokua wa "kimazoea" kidogo kilichokua kinapatikana waliamua kurudisha katika uwekezaji zaidi na hatimaye waliweza kufanikiwa kujenga mwalo(sehem maalum ya kuchenjua dhahabu kwa kutumia zebaki).
Hiyo iliwafungua zaidi na kufanya tafiti zaidi katika sekta ya madini na hatimaye waligundua kua uwezo wa zebaki(mercury) kuchukua dhahabu katika mchanga ni mdogo na hivo waliona kuna fursa zaidi endapo watawekeza katika kujenga kiwanda kidogo cha kuchenjua dhahabu(Vat Leaching Plant).
Ilipofika mwaka November 2017 ujenzi wa kiwanda hicho ambacho kipo katika kijiji cha undomo wilayani nzega ulikua umekamilika. Uwezo wa kiwanda chao ni kuchenjua tani 2000 za mchanga wa dhahabu kwa mwezi. Licha kiwanda chao kukamilika kwa takriban miezi 5 sasa vijana hao wameshindwa kuanza kazi ya uchenjuaji kutokana na changamoto ya mtaji wa kuanzia kazi.
Endapo kiwanda chao kitaanza kazi,kitakua na uwezo wa kutoa ajira kwa vibarua wasiopungua 120 na waajiriwa wasiopungua 15.
Lakini pia kiwanda hicho kitatoa fursa kwa wachimbaji wengine wa migodi midogo ya karibu kuweza kuuza mabaki ya mchanga wao na kuwahakikishia soko la uhakika.
Pia ni fursa kwa serikali kuweza kukusanya kodi kupitia mapato yatokanayo na kiwanda hicho.

Mpaka sasa vijana hao wamefanikiwa kusajili kampuni yao inayoitwa JADAN GOLD MINES LTD

Ni wakati sasa serikali na wadau kuweza kuwaunga mkono vijana kama hawa wenye UTHUBUTU kwa manufaa ya mwananchi mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Chini hapa ni link ya video inayoonyesha changamoto waliyokutana nayo kwenye safari yao ya kilimo
 
Kama vijana wetu wamefika hapo ni jambo la kufurahia sana wanaosema wa Africa tumelogwa na nani wakae pembeni

Nimesikitishwa sana na changamoto zilizowakuta kwani nilipokuwa nasoma wazo likaniijia nikajisemea laiti wangezungusha mpaka wa miti kwenye shamba
Lakini limetokea na kama wameingia kwenye biashara ya dhahabu watafanikiwa wasizidiane akili tu
Hawana website huenda wakahitaji vifaa baadae
 
Hongereni sana!
Ishu ya kushika jembe sio mchezo halafu mtu aje alishe mifugo kizembe kabisa!
Unaweza ukatoka na roho ya mtu
 
Kama vijana wetu wamefika hapo ni jambo la kufurahia sana wanaosema wa Africa tumelogwa na nani wakae pembeni

Nimesikitishwa sana na changamoto zilizowakuta kwani nilipokuwa nasoma wazo likaniijia nikajisemea laiti wangezungusha mpaka wa miti kwenye shamba
Lakini limetokea na kama wameingia kwenye biashara ya dhahabu watafanikiwa wasizidiane akili tu
Hawana website huenda wakahitaji vifaa baadae

Ni jambo jema kwakweli kuona vijana wetu wanajituma na kujiongeza namna hii,biashara ya dhahabu ni nzuri hasa uchenjuaji kwani tayari unakua umepunguza risks nyingi sana...
 
Ni jambo jema kwakweli kuona vijana wetu wanajituma na kujiongeza namna hii,biashara ya dhahabu ni nzuri hasa uchenjuaji kwani tayari unakua umepunguza risks nyingi sana...
Hii ni fursa kubwa sana ambapo zamani ilikuwa hata huwezi kusogea hapo
Wajitahidi madini yanalipa sana
 
Ebu kuweni specific, mmekwama wapi hasa,

Changamoto kubwa ni mtaji wa kuanzia uzalishaji kwani ujenzi umekamilika,mtaji wanaohitaji ni kwa ajili ya ununuzi wa mabaki ya mchanga kwa wachimbaji wadogo(takribani tani 2,000),usafirishaji kwenda kiwandani,kemikali zinazotumika kuchenjulia na gharama za uendeshaji kama chakula,mafuta ya mitambo,malipo ya vibarua n.k. Wanauhitaji wa takriban shilingi milioni 126(asilimia 70 ya pesa hii inakwenda kwenye ununuzi wa mabaki ya mchanga)
 
Wamuone kamishna wa madini wa iyo kanda atawasaidia au tv station iwarushie harakati zao kwenye tarifa ya habari mkuu wa nchi atawapa sapoti
 
  • Thanks
Reactions: adb
Kwanza kabisa hongereni sana..kwa vijana wasomi kuweza kujiajiri maana changamoto za ajira ni nyingi..vilevile polen kwa kulishiwa mashamba yenu..
 
  • Thanks
Reactions: adb
Ila nilikua nataka kujua mlengo wenu kwenye uchimbaji..je ni kama hawa wachimbaji wadogo wadogo tunaowajua wanachimba kwa local tools..
 
  • Thanks
Reactions: adb
Ila nilikua nataka kujua mlengo wenu kwenye uchimbaji..je ni kama hawa wachimbaji wadogo wadogo tunaowajua wanachimba kwa local tools..

Hapana hawa vijana wame advance kutoka huko kwenye kuchimba kwa zana duni hadi kujenga hicho kiwanda cha kuchenjua dhahabu,hawa vijana wao wananunua michanga kutoka kwa wachimbaji wadogo naku-process kwenye kiwanda chao so hawa vijana kwa namna moja au nyingine wana-suport pia juhudi za wachimbaji wadogo!
 
Hapana hawa vijana wame advance kutoka huko kwenye kuchimba kwa zana duni hadi kujenga hicho kiwanda cha kuchenjua dhahabu,hawa vijana wao wananunua michanga kutoka kwa wachimbaji wadogo naku-process kwenye kiwanda chao so hawa vijana kwa namna moja au nyingine wana-suport pia juhudi za wachimbaji wadogo!
Ok..nimekuelewa ila je mlishaonana na taasisi zezote zile za kifedha na uongoz wenu wa wilaya..
 
  • Thanks
Reactions: adb
Ok..nimekuelewa ila je mlishaonana na taasisi zezote zile za kifedha na uongoz wenu wa wilaya..

Ndio,uongozi wa wilaya ya Nzega unafaham jitahada na changamoto za vijana hawa,pia wamekwenda taasisi nyingi sana za fedha bila mafanikio kwani bank nyingi za hapa nchini hazitoi mikopo sekta ya madini hasa katika level hii ya SME
 
Hongereni sana kwa uthubutu wenu,naiona picha kubwa hapo badae kama mtaendelea hivo,mara nyingi tumeskia viongozi wa kisiasa pamoja na serikali wakisisitiza suala la kujiajiri kwa vijana,ni ukweli uliowazi kua pesa zinazotengwa kwenye halmashauri zetu(10%) kwa ajili ya vijana na akina mama bado ni ndogo na mikopo yake ni midogo midogo sana,ni wakati sasa serikali iandae mazingira ya kusaidia vijana kama hawa wenye mawazo makubwa na uhitaji wa mikopo mikubwa.
 
  • Thanks
Reactions: adb
Back
Top Bottom