Mh Rais Nikukumbushe Tena, Amani ni Tunda la Haki, Rehearse this well!

mcfm40

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
4,452
3,150
Katika vyombo vya habari leo umesikika ukihimiza watanzania watunze amani na mshikamano ulipokuwa makanisani na misikitini huko Chato.

Lakini Mh pamoja na umuhimu wa kusisitiza swala amani, usisahau kuwa amani ni tunda la haki! Bila haki amani ya kweli ni ndoto. Haki na Amani ni maneno pacha. Huwexi kuzungumzia amani bila kuzungumzia na kusisitiza haki.

Watawala mnaogopa sana kutaja neno haki katika hotuba zenu kwa sababu mnajua haki ni gjarama na wengi hampo tayari kuongoza kwa haki!

Mh ni contradiction na unafiq kuhubiri amani kanisani na misikitini huku unabinya haki na uhuru wetu wa kidemokrasia.

Wewe unajipendelea kufanya mikutano na kuimarisha chama chako nchi nzima huku ukitumia vibaya vyombo vya dola kuwazuia washindani wako nao wafanye mikutano ya kuimarisha vyama vyao. Kumbuka hii ni nchi inayofuata misingi ya demokradia ya vyama vingi.

Kwa mtindo huu Mh ujue unapandikiza mbegu ya uasi katika nchi. Ukiminya haki za kikatiba za washindani wako watazitafuta kwa njia nyingine ambazo zinaweza kuwa na madhara! Na kuhubiri amani misikitini na makanisani haitasaidia km wewe mwenyewe hufuati misingi ya amani ambayo ni kuiheshimu katiba na sheria tulizojiwekea katika kuendesha nchi!

Hivyo mh nakusihi urudie mara kwa mara hii sentensi na uikariri na kuiishi katika uongozi wako (si utawala) kama kweli unataka kuliongoza hili taifa kwa mafanikio. "Amani ni tunda la haki." Hii iwe sala na dua yako kila ulalapo na uamkapo! Asante!
 
anajua hata asipotenda haki likanukishwa atasepa zake kwa mbest wake Kagame au m7 kwahiyo haoni tabu
 
Mungu ana technique nyingi sana anaweza kukutumia kama mlango wa kuangalia adui bila wewe kujua ili atimize kusudi lake.

Inaitaji busara itokayo kwake kuweza kumudu kuongoza Taifa

Mfano alipandikiza roho ya uadui kwa ndugu zake Yusuph wakamchukia kiasi cha kutaka kumuua but wakamuuza kumbe Ile ndio njia ya Yusuph kuwa Waziri Mkuu.

Nawasikia viongozi wa dini wakisema mara kwa mara huyu ni chaguo la Mungu katika awamu zote but badaye wanazikana kauli zao.

Nini nataka kusema kuna kusudi la Mungu kuweka utawala huu na sii kwa yale maombi mlikuwa mnakesha ilo kusudi liwe zuri au baya kwako Mungu ndio dhamira yake nasi tunapaswa kujifunza kwa hilo.

Kama alisema Yes kwako haitabadilika ingawa utakutana na No nyingi au gharama b4 kuifikia iyo Yes aliyokupangia
 
Dawa ya mnywa kiroba ni maji ya washawasha.
Tutaendelea kumhubiria Mh rais kwamba Amani ni tunda la haki kwa ssbsbu huko makanisani na misikitini anakokwenda hawadhubutu kumwambia ukweli, wasije wakakosa michango anayowapelekea! Fikiria pale Mnazi Mmoja siku ya Idd, wangempa mahusia kuhusu umuhimu wa haki katika nchi angewapa yale mafweza kweli?
 
Katika vyombo vya habari leo umesikika ukihimiza watanzania watunze amani na mshikamano ulipokuwa makanisani na misikitini huko Chato.

Lakini Mh pamoja na umuhimu wa kusisitiza swala amani, usisahau kuwa amani ni tunda la haki! Bila haki amani ya kweli ni ndoto. Haki na Amani ni maneno pacha. Huwexi kuzungumzia amani bila kuzungumzia na kusisitiza haki.

Watawala mnaogopa sana kutaja neno haki katika hotuba zenu kwa sababu mnajua haki ni gjarama na wengi hampo tayari kuongoza kwa haki!

Mh ni contradiction na unafiq kuhubiri amani kanisani na misikitini huku unabinya haki na uhuru wetu wa kidemokrasia.

Wewe unajipendelea kufanya mikutano na kuimarisha chama chako nchi nzima huku ukitumia vibaya vyombo vya dola kuwazuia washindani wako nao wafanye mikutano ya kuimarisha vyama vyao. Kumbuka hii ni nchi inayofuata misingi ya demokradia ya vyama vingi.

Kwa mtindo huu Mh ujue unapandikiza mbegu ya uasi katika nchi. Ukiminya haki za kikatiba za washindani wako watazitafuta kwa njia nyingine ambazo zinaweza kuwa na madhara! Na kuhubiri amani misikitini na makanisani haitasaidia km wewe mwenyewe hufuati misingi ya amani ambayo ni kuiheshimu katiba na sheria tulizojiwekea katika kuendesha nchi!

Hivyo mh nakusihi urudie mara kwa mara hii sentensi na uikariri na kuiishi katika uongozi wako (si utawala) kama kweli unataka kuliongoza hili taifa kwa mafanikio. "Amani ni tunda la haki." Hii iwe sala na dua yako kila ulalapo na uamkapo! Asante!
It is very true.

Haiwezekani kila siku unasisitiza watanzania wadumishe amani na huku ukiwaomba wananchi wakuombee kwa Mungu, wakati wewe mwenyewe ndiye unayetaka kuivunja amani kwa kuminya demokrasia na huku unaisigina Katiba ya nchi ambayo inabainisha kuwa nchi hii ni ya mfumo wa vyama vingi, lakini wawe unatoa 'likizo' ya lazima kwa vyama vya siasa vya upinzani hadi mwaka 2020, wakati chama chako ukikiruhusu kufanya siasa kwa nguvu zake zote bila kuzuiwa na Polisi.......

Na anapotokea mtu jasiri na shujaa kama Tundu Lissu anapousema ukweli kuwa Mkuu wa nchi 'unapotea''' njia, Jeshi lako kwa 'kujipendekeza' kwako linamfunngulia kesi lukuki zisizo na kichwa wala miguu..........

Vyama vya upinzani vinapotaka kutumia haki yao ya kikatiba ya kufanya mikutano na maandamano, unaabuse 'power yako kwa kuviamuru vyombo hivyo 'unavyovimiliki' kuwashughulikia hao wananchi kwa kile unachikiita kuwa wewe hujaribiwi.........

Hakika wananchi wote tuna wajibu wa kupaza sauti zetu kwa nguvu zetu zote kumwambia Rais wetu kuwa njia ya uhakika ya kipekee ya kudumisha amani ya nchi hii ni kwa yeye kuongoza nchi hii kwa mujibu wa Katiba ya nchi hii ambayo Kabla ya kushika madaraka aliapa kuitii na kiiheshimu.......

Iwapo Rais wetu atapuuza ushauri unaotolewa na wananchi wengi kuwa anapaswa kuongoza nchi kwa mujibu wa Katiba ya nchi, na akaamua kuendelea kuendesha nchi hii kwa njia aliyoochagua ya ubabe na vitisho, hakika nchi hii atakuwa ameamua kwa makusudi kabisa kuitumbukiza kwenye machafuko.
 
Katika vyombo vya habari leo umesikika ukihimiza watanzania watunze amani na mshikamano ulipokuwa makanisani na misikitini huko Chato.

Lakini Mh pamoja na umuhimu wa kusisitiza swala amani, usisahau kuwa amani ni tunda la haki! Bila haki amani ya kweli ni ndoto. Haki na Amani ni maneno pacha. Huwexi kuzungumzia amani bila kuzungumzia na kusisitiza haki.

Watawala mnaogopa sana kutaja neno haki katika hotuba zenu kwa sababu mnajua haki ni gjarama na wengi hampo tayari kuongoza kwa haki!

Mh ni contradiction na unafiq kuhubiri amani kanisani na misikitini huku unabinya haki na uhuru wetu wa kidemokrasia.

Wewe unajipendelea kufanya mikutano na kuimarisha chama chako nchi nzima huku ukitumia vibaya vyombo vya dola kuwazuia washindani wako nao wafanye mikutano ya kuimarisha vyama vyao. Kumbuka hii ni nchi inayofuata misingi ya demokradia ya vyama vingi.

Kwa mtindo huu Mh ujue unapandikiza mbegu ya uasi katika nchi. Ukiminya haki za kikatiba za washindani wako watazitafuta kwa njia nyingine ambazo zinaweza kuwa na madhara! Na kuhubiri amani misikitini na makanisani haitasaidia km wewe mwenyewe hufuati misingi ya amani ambayo ni kuiheshimu katiba na sheria tulizojiwekea katika kuendesha nchi!

Hivyo mh nakusihi urudie mara kwa mara hii sentensi na uikariri na kuiishi katika uongozi wako (si utawala) kama kweli unataka kuliongoza hili taifa kwa mafanikio. "Amani ni tunda la haki." Hii iwe sala na dua yako kila ulalapo na uamkapo! Asante!
Hivi inawezekanaje Jeshi letu la Polisi liendelee kuabuse power yake kwa kuzuia almost mikutano yote ya vyama vya siasa vya upinzani kwa 'kisingizio' cha taarifa za kiintelijensia kuwa mikutano hiyo itasababisha uvunjifu wa amani, wakati cha kushangaza kupita kiasi ni kuwa haitokei hata siku moja intelejensia hiyo ya Policcm haijawahi kuzuia hata mkutano mmoja wa CCM kwa sababu hizo za kiintelijensia!

Ni dhahiri wananchi wanapolalamikia Jeshi letu la Polisi kuwa ni proCCM wanakuwa na ushahidi usio na shaka yoyote kuhusu madai yao hayo........
 
Katika vyombo vya habari leo umesikika ukihimiza watanzania watunze amani na mshikamano ulipokuwa makanisani na misikitini huko Chato.

Lakini Mh pamoja na umuhimu wa kusisitiza swala amani, usisahau kuwa amani ni tunda la haki! Bila haki amani ya kweli ni ndoto. Haki na Amani ni maneno pacha. Huwexi kuzungumzia amani bila kuzungumzia na kusisitiza haki.

Watawala mnaogopa sana kutaja neno haki katika hotuba zenu kwa sababu mnajua haki ni gjarama na wengi hampo tayari kuongoza kwa haki!

Mh ni contradiction na unafiq kuhubiri amani kanisani na misikitini huku unabinya haki na uhuru wetu wa kidemokrasia.

Wewe unajipendelea kufanya mikutano na kuimarisha chama chako nchi nzima huku ukitumia vibaya vyombo vya dola kuwazuia washindani wako nao wafanye mikutano ya kuimarisha vyama vyao. Kumbuka hii ni nchi inayofuata misingi ya demokradia ya vyama vingi.

Kwa mtindo huu Mh ujue unapandikiza mbegu ya uasi katika nchi. Ukiminya haki za kikatiba za washindani wako watazitafuta kwa njia nyingine ambazo zinaweza kuwa na madhara! Na kuhubiri amani misikitini na makanisani haitasaidia km wewe mwenyewe hufuati misingi ya amani ambayo ni kuiheshimu katiba na sheria tulizojiwekea katika kuendesha nchi!

Hivyo mh nakusihi urudie mara kwa mara hii sentensi na uikariri na kuiishi katika uongozi wako (si utawala) kama kweli unataka kuliongoza hili taifa kwa mafanikio. "Amani ni tunda la haki." Hii iwe sala na dua yako kila ulalapo na uamkapo! Asante!
Hivi inawezekanaje nchi hii tukajiaminisha kuwa tutaendeleza amani iliyodumu tokea tupate uhuru, wakati msingi mkuu wa kudumisha amani ambao ni pacha ya HAKI na AMANI ukipuuzwa waziwazi kabisa bila kukemewa na watu wanaosimamia dhamana ya kuwaongoza kondoo wao kwa misingi ya imani viongozi wetu wa dini wakiwa kimya kabisa bila kukemea mtindo huu wa uendeshaji wa nchi bila kufuata Katiba ya nchi na Sheria nyingine mbalimbali za nchi?
 
Hilo ndilo linalonishangaza Mkuu. Kama kweli rais hataki mambo ya mavyams ilikuwaje akakubali kuwa mwenyekti wa ccm taifa? Hakuona kwamba hili litamletea mgongano wa kimaslahi! Halafu viongozi wa dini wapo kimya, wenye busara huko ccm nao wapo kimya. Je wanzsubiri maafa ndio waibuke?
Hivi inawezekanaje nchi hii tukajiaminisha kuwa tutaendeleza amani iliyodumu tokea tupate uhuru, wakati msingi mkuu wa kudumisha amani ambao ni pacha ya HAKI na AMANI ukipuuzwa waziwazi kabisa bila kukemewa na watu wanaosimamia dhamana ya kuwaongoza kondoo wao kwa misingi ya imani viongozi wetu wa dini wakiwa kimya kabisa bila kukemea mtindo huu wa uendeshaji wa nchi bila kufuata Katiba ya nchi na Sheria nyingine mbalimbali za nchi?
 
anajua hata asipotenda haki likanukishwa atasepa zake kwa mbest wake Kagame au m7 kwahiyo haoni tabu
Hahaha. Rais wetu huyu naye buana, eti Kagame ndio role model wake! Ni shida_!
 
Back
Top Bottom