Zitto: Hata kesi ya Mbowe ni jumba bovu kwa awamu ya 6. IFUTWE!

Sexless

JF-Expert Member
Mar 11, 2017
21,563
50,407
Screenshot_20211204-161416.png
 
Mi_shakata_tamaa_kutoa_ushauri_%F0%9F%98%91_uongo_mbaya_-_maana_ninachoona_ni_ka_Shangazi_Fatm...jpg


Utukufu wa Mungu ni wa ajabu sana ! Leo Mtukufu Rais kwa kinywa chake mwenyewe ametamka kwamba ameona mambo ya hovyo ambayo amebambikiwa na awamu zilizopita , ameongea mengi na kukemea vikali kundi la watu waliomuangushia gari bovu kwenye awamu yake kwa lengo la kumchafua .

Mh Samia hakuwataja wapinzani , bali amewataja wanaccm wenzake na viongozi waliomo kwenye serikali yake mwenyewe , hawa watu wa hovyo ndio walewale waliokuwemo kwenye awamu ya 5 , hawa ndio waliomuangushia gari bovu mama na kumlisha maneno ya uongo ya kwamba Freeman Mbowe ni Gaidi , Njama zote za kumbambika kesi ya Uongo ya Ugaidi Mbowe zilipangwa kwenye awamu ya 5 na hawa hawa watu wa hovyo waliotajwa leo

Kesi ya uongo iliyofunguliwa kishamba sana bila hata ushahidi wa kuthibitisha ugaidi wa Mbowe , sasa inadhalilisha Nchi kila mahali duniani , mliyoyasikia huko EU ni ushahidi wa kwamba hili ni gari bovu aliloangushiwa mama na utawala uliopita kwa msaada wa vyombo vya dola , ANAPASWA KUTOONA AIBU KUIFUTA KESI HII ILI KULINDA HESHIMA YA UTAWALA WAKE , na baada ya kufuta uchafu huu unaoleta harufu kali na mbaya duniani kote , tunaamini atafanya mabadiliko kwenye uongozi wa vyombo vya dola nchini , Ili kuondoa watu wa hovyo wanamuangushia gari bovu

KUANZA UPYA SI UJINGA .
 
Back
Top Bottom