Jumbe Brown
JF-Expert Member
- Jun 23, 2020
- 12,078
- 12,756
Comment ina MADINI haswaa......Huu ni utumbo tu ambao biashara yake mwisho saa 6. Mbowe anakabiliwa na tuhuma zilizotokea Magufuli akiwa Rais na Mahakama ndiyo yenye jukumu la kumuachia, ndiyo utawala wa sheria huo.
Kuhusu Mbowe kumsaidia Samia nakataa kabisa. Mbowe hana hekima hata kidogo.
Haina ubishi wanufaika wakubwa wa siku 100 za kwanza za Rais SSH ni CDM, Mbowe na Mdude kwa maelekezo, falsafa na haiba ya Samia. Mpaka tukaandika threads nyingi za kusema "Mama anaupiga mwingi".
Ningetegemea Mbowe na Lissu watumie busara katika madai yao kwa kuwa wasikivu na wavumilivu pale Samia aliposema suala la Katiba lisubiri ajenge uchumi.
On the contrary Mbowe na Lissu wakaanza kumfokea Rais kama vile ni mbunge wa BAWACHA?? Na Mdude akasema " nitamnyoa mama yenu kwa wembe uleule nilio mnyolea mtangulizi wake"
Nini kikiwapata hawa watu ambao kwa Mwendazake waliufyata miaka 5. Mwendazake kawapiga risasi, kavunja Bilicanas na kavunja na mashamba yake, kamchukulia na fedha kwenye akaunti. Hajawahi hata kulalamika.
Samia kamrudishia akaunti, kesi zao za kubambika zikapigwa chini pamoja na ya MDUDE. Halafu wao ndiyo wa kwanza kusema HATUWEZI KUMBEMBELEZA Samia.