Mh Rais Kikwete kauli zako zina utata

Exaud Mamuya

JF-Expert Member
Jul 26, 2011
403
242
Akiongea katika maadhimisho ya siku ya uhuru amemsifia mzee Mandela bila kukumbuka yanayofanyika kwenye serikali yake. Ambayo amesema yafuatayo.
1.Mzee Mandela aliwapigania watu wake dhidi ya serikali ya kibaguzi iliyokuwa akiongozwa na Makaburu.
2.Mzee Mandela alipoona kutafuta haki na usawa kwa njia ya AMANI ilibidi aanzishe chama cha siasa yaani ANC
3.Akiwa ndani ya ANC na kuona watawala bado hawako tayari kutenda HAKI ilibidi azunguke nchi mbalimbali kwa lengo la kuanzisha JESHI.
4.Lakini kabla ya kuanza kulitumia jeshi alikamatwa na kufungwa gerezani.
5.Amesema mzee Mandela alipokuja Tanzania alilala kwa mama Nsilo Swai na kusahau viatu vyake kwa mama Nsilo Swai.
Mh rais ameona mabaya ya makaburu na kumuona mzee Mandela alikuwa sahihi wakati rais Kikwete anajua dhuluma zinazofanywa na serikali yake kwa kukikandamiza Chadema na hata Chadema inapoona HAKI inashindikana kupatikana kwa njia ya AMANI na zaidi ya yote kutumia vyombo vya dola kuvuruga mikutano ya Chadema iliamua kutangaza kuanzisha makambi ya ukakamavu kwa vijana wa Chadema kwa lengo la kulinda mikutano na viongozi, wanachama na wasiokuwa wanachama bado serikali ya mh Kikwete ilileta ubabe katika swala hili.

Sasa serikali hii ya CCM inatofautianaje na serikali ya makaburu wa Afrika ya kusini?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
...if you can read between the lines, JK anaogopa CDM mkishika dola mtalipiza kisasi... Hivi huyo Nswilo Swai ni kabila gani? kwanini mandela alifikia nyumbani kwake?
 
mimi pamoja na kuwa mnazi wa CADEMA JK nampenda kwa tabia yake ya kurusu tutukanane na kumtukana yeye kwenye mitandao bila kutusumbua. Mapungufu yake mengine ni seemu ya maisa ya binadamu.
 
uko bias sana kwenye thread yako. umeona ya chadema tu. umesahau ya CUF yaliyoanza kabla na bado mpaka leo yanaendelea kote bara na visiwani. umesahau ya NCCR yaliyotufungulia mlango. kwa upumbav.u huu haya maccm will rule us forever.
 
Duh emphasis ilikuwa ni viatu vilivyosahaulika kwa Nsilo Swai huyu ni dada yake Mama Anna Mkapa
 
Akiwahutubia wananchi katika sherehe za miaka 52 ya uhuru wa Tanzania bara, kikwete pamoja na kutoa kauli nyingi za kejeli kimafumbo pia kaonyesha wasi wasi wa roho za kulipa kisasi miongoni mwa watu watakaoweza kupata fursa fulani.
My take:
je mheshimiwa ana wasi wasi gani na visasi? au ndo kwanza anaanza kujisalimisha ukilinganisha yanayofanywa na serikali yake na upepo wa kisiasa kwa sasa?
Nawasilisha.
 
Hii ni kauli ya Mh. Kikwete, rais wa JMT wakati akitoa speech yake muda mfupi uliopita uwanja wa uhuru Dar akielezea wasifu wa mtu ambaye binafsi ninayekubaliana na falsafa yake Mzee wetu MANDELA. Nimejiuliza nani hasa alikuwa mlengwa wa kauli ile.
1. uhasimu ndani ya ccm mfano kambi ya akina sita, mwakyembe et al na kambi ya akina lowasa? au membe au
2. alimaanisha uhasimu kati ya ccm na wapinzani kwa maana ya CUF, chadema au NCCR magauzi?
I am paranoid.
 
Anamsema Membe , ambaye alisema Ana maadui 11akiwa Rais lazima wahame nchi wanaishi Kenya ..........
 
makundi ndani ya chama chake hasa kambi ya Lowassa yenye nguvu zaidi
hakuna ubishi watateuliwa kugombania urais ingawa hawatashinda.
JK ameshaogopa CCM kutokurudi madarakani alikuwa kama anatoa wosi kwa chadema wasilipize kisasi
 
Hapa Jk kapiga umbea,"jasiri haachi asili".Mpaka kutuambia alikolala na kusahau viatu?what was the reason behind this?
 
Hii ni kauli ya Mh. Kikwete, rais wa JMT wakati akitoa speech yake muda mfupi uliopita uwanja wa uhuru Dar akielezea wasifu wa mtu binafsi ninayekubaliana na falsafa yake. Nimejiuliza nani hasa alikuwa mlingwa wakauli ile.
1. uhasimu ndani ya ccm mfano kambi ya akina sita, mwakyembe et al na kambi ya akina lowasa? au membe au
2. alimaanisha uhasimu kati ya ccm na wapinzani kwa maana ya CUF, chadema au NCCR magauzi?
I am paranoid.

aache kuogopa kivuli chake. Kama anajua kuna visasi kwa nini asiongoze katika njia ambayo haitampa maadui?
UKIUA KWA UPANGA NAWE UTAUWAWA KWA UPANGA
 
makundi ndani ya chama chake hasa kambi ya Lowassa yenye nguvu zaidi
hakuna ubishi watateuliwa kugombania urais ingawa hawatashinda.
JK ameshaogopa CCM kutokurudi madarakani alikuwa kama anatoa wosi kwa chadema wasilipize kisasi

lazima wote waliotawala kifisadi ile kwao CDM ikichukua nchi 2015.
 
apa sitii neno JK namkubali ila CCM siipendi ndo maana wana CCM wenyewe wanamcukia.
 
Anaanza kuweweseka kwa mabaya aliyofanya, mshahara wa mwenye kutenda dhambi ni Mungu, lakini Mungu ana njia nyingi za kuadhibu na mara nyingi kuanzia hapa hapa duniani mtu angali na uhai. Tenda mema, kwani kutenda mabaya kwa kinga ya kutendewa mema kwa kivuli cha Mandela ni kuweweseka, wasiwasi na woga kwa mabaya tuliyowatendea wengine.
 
Akiongea katika maadhimisho ya siku ya uhuru amemsifia mzee Mandela bila kukumbuka yanayofanyika kwenye serikali yake. Ambayo amesema yafuatayo.
1.Mzee Mandela aliwapigania watu wake dhidi ya serikali ya kibaguzi iliyokuwa akiongozwa na Makaburu.
2.Mzee Mandela alipoona kutafuta haki na usawa kwa njia ya AMANI ilibidi aanzishe chama cha siasa yaani ANC
3.Akiwa ndani ya ANC na kuona watawala bado hawako tayari kutenda HAKI ilibidi azunguke nchi mbalimbali kwa lengo la kuanzisha JESHI.
4.Lakini kabla ya kuanza kulitumia jeshi alikamatwa na kufungwa gerezani.
5.Amesema mzee Mandela alipokuja Tanzania alilala kwa mama Nsilo Swai na kusahau viatu vyake kwa mama Nsilo Swai.
Mh rais ameona mabaya ya makaburu na kumuona mzee Mandela alikuwa sahihi wakati rais Kikwete anajua dhuluma zinazofanywa na serikali yake kwa kukikandamiza Chadema na hata Chadema inapoona HAKI inashindikana kupatikana kwa njia ya AMANI na zaidi ya yote kutumia vyombo vya dola kuvuruga mikutano ya Chadema iliamua kutangaza kuanzisha makambi ya ukakamavu kwa vijana wa Chadema kwa lengo la kulinda mikutano na viongozi, wanachama na wasiokuwa wanachama bado serikali ya mh Kikwete ilileta ubabe katika swala hili.

Sasa serikali hii ya CCM inatofautianaje na serikali ya makaburu wa Afrika ya kusini?



Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

Ni ajabu kuifananisha Serikali ya Kikwete na Serikali ya Kikaburu, Halafu wakati huo huo unamuita kiongozi wa serikali hiyo Mheshimiwa. Mimi nadhani kaburu hana heshima au?
 
Asiogope kuachia nchi watanzania kutoka chama kingine kwani vyote vyama na wanachama wake ni watanzania
 
Back
Top Bottom