Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Mh Ndugai pamoja na wenzako fulani inaonekana uliumia sana wabunge wetu walipotoka nje wakati rais anahutubia. Leo naibu spika amesema eti wananchi waliowatuma wabunge hao kuwawakilisha bungeni walikerwa pia kwa wabunge hao kutoka bungeni. Napenda nimuambie Ndugai kuwa kwa usahihi kabisa hicho ndicho tulichowatuma wabunge wetu hawa wapendwa kukifanya. Tena kwangu ningewakilishwa vizuri zaidi kama mmoja angemrushia kiatu.