MH MWIGULU, CHADEMA sio bahati mbaya ni Mpango wa Mungu huwezi kuihujumu ukashinda!!

sokoinei

JF-Expert Member
Feb 27, 2012
1,832
566
Kwako MWIGULU MCHEMBA Naibu katibu mkuu Ccm bara. Nikupongeze kwanza kwa hatua yako ya kukiri kuhusika na Video ya Kutengeneza dhidi ya Mkuu wa Usalama na ulinzi CDM ndugu WILFRED LWAKATARE.

Pili nikukumbushe tu machache uliyoyafanya dhidi ya CDM na viongozi wake ktk "JITIHADA" zako za Kuihujumu chama hiki Kikuu cha Upinzani ktk Kukipaka matope na Kuitakia mabaya.
Baada ya Uchaguzi wa Igunga 2011 wewe na wenzio mlimuua na kumtupa porini mfuasi na mwanachama wa CDM mkazi wa Dar es salaam.
Mwaka 2012 baada ya uchaguzi wa Arumeru mashariki ulishiriki mipango ya kumuua mwenyekiti wa CDM kata ya Usa riva. Mwaka huohuo 2012 mwishoni ukiwa ktk kituo cha STAR TV kinachorusha matangazo yake jijini mwanza ulidai kwamba unao Mkanda wa Video unaowaonyesha Viongozi wa CDM wakipanga kuteka na kuuwa watu.

Miezi michache baadae Mwenyekiti wa Wahariri Absalom Kibanda alitekwa na kupigwa na kuumizwa vibaya hadi kupoteza jicho lake moja.
Baada ya Mpango wako kukamilika ndipo ikaibuka na Video yako ya Lwakatare,na Polisi bila kukuhoji wewe kama Mtuhumiwa wa kwanza wakakurupuka na LWAKATARE na kumpa Kesi ya UGAIDI.ukachekelea sana na Majuha wenzako.
Kumbuka ulisema unao ushahidi na hata kama ni MBINGUNI upo tayari kuutoa.Tunasubiri maana MUNGU ni wa haki

Lwakatare alikaa Mahabusu kwa zaidi ya miezi 3 hadi alipofutiwa mashtaka matatu ya Ugaidi na kubakiwa na moja na hatimae kupewa dhamana..Cha ajabu wewe unaehusika na uliesema una mkanda na ukauweka mitandaoni upo huru ukiendelea kuhujumu CDM na kupoteza maisha ya watu wasio kua na hatia.

Ktk Vikao vya Bunge vilivyopita na vinavyoendelea sasa umekua ukiendelea na Harakati na hujuma zako dhidi ya CDM hali iliyosababisha wabunge 6 wa CDM kusimamishwa kuhudhuria vikao vitano vya bunge.

Ktk uchaguzi mdogo wa Madiwani uliokua unafanyika ktk kata 26 uliendelea na Mbinu zako chafu na siasa za Maji Taka dhidi ya CDM kwa kumtembeza Majukwaani MUSA KIJANA "TAAHIRA"alie athirika Kisaikolojia baadaya kumwagiwa Tindikali kwa Mipango yako kule Igunga, na kuelezea watu kuwa waliomfanyia vile ni CDM.

Haikuishia hapo siku mbili kabla ya Uchaguzi wa Madiwani ukiwa Ktk kata ya Kimandolu moja ya kata nne zilizokua zikifanya ichaguzi jijini Arusha uliwaambia watu kuwa wasipoichagua CCM wataendelea kufa kwani CDM ni chama cha Vurugu.

Siku moja kabla ya Uchaguzi,baada ya kuona mmezidiwa na CDM pamoja na Ccm kuwatumia baadhi ya Mawaziri ktk mikutano yao bila mafanikio ndipo tena chini ya Mipango yako mkaamua kupiga Bomu ktk hitimisho la mkutano wa CDM ili tu uchaguzi uahirishwe kwa kile kinachodaiwa kua hadi Amani itakapo rejea.
Tangia juzi ilipotokea tukio hilo sio watu wa kawaida sio polisi wanakuhusisha na tukio hilo. Yamkini ktk hili la Bomu huusiki moja kwa moja lakini Mtiririko wa Mauaji ya Igunga,Usa riva,Ndago Singida, Video ya Lwakatare na sasa Bomu Arusha yananifanya nikuhusishe.

Mh Mwigulu CDM ni mpango wa MUNGU na wewe kujitahidi kwa Hila kuzuia Mipango ya Mungu matokeo yake yatakua mabaya sana kwako. Leo hii ninaamini kwamba baada ya uchaguzi huu kusimamishwa na kuwa utafanyika tena tar 30,huna tena hamu wala Ujasiri wa Kusimama ktk jukwaa la siasa hapa Arusha na kuihusisha CDM na Upuuzi uliouzoea.
Wana Arusha wa CCM,CUF,TLP,NCCR na CDM hawataki hata kusikia jina lako.kwa Mtaji huu ndio kabisa UMEIZIKA CCM Jijini Arusha.
Kumbuka kuwa SIKU ZOTE MWISHO WA UBAYA NI AIBU.
Chadema ni mpango wa Mungu kuizuia hutaweza.
 
Mwigulu asipothibitiwa, atasababisha nchi nzima iingie kwenye machafuko. Huyu jamaa hafai kuwa kiongozi kwenye nchi zenye amani kama Tanzania. Kwanini CCM mnaenedelea kumkumbatia wakati anazidisha hasira za wananchi dhidi yenu?

Damu zote za watu anao endelea kuzimwaga HAKIKA HAZITAPOTEA BURE!
 
wakitoka lumumba watakuja hapa kumtetea.subiri wamalize kuchukua posho yao ya leo.
 
Pia ulisahau mauji yaliyo tokea tarafa ya Ndago,Iramba yalihaririwa na Mwigulu
 
Mbn mnatafuta ubaya Mwigulu haipiti siku mnalete mada juu yake hamna jipya mmedoda
 
Mwigilu una kazi kubwa sasa ya kujisafisha ; inavyoonekana wewe ndiye muasisi wa mbinu chafu za kuidhoofisha CDM; umeleta siasa za chuki, unawagombaisha watanzania kwa udini na ukabila; jisafishe hizi tuhuma zinazoelekezwa kwako na watanzania ni nzito sana.
 
Kama raisi wa nchi anaangaliga huku nathani sasa mwigulu atakuwa kwenye wakati mgumu sana.na inasemekana mipango yote ya arusha yeye ndiye aliiratibu na mwanamke mmoja wa ccm.kwa nini police hawasemi zile risasi walipiga za nini na mabomu ya machozi wakati watu walikuwa wanakimbia kujiokoa na wengine kumfuatilia aliyerusha bomu ambaye inasemekana aliingia kwenye cruza ya polisi akalala chini?
 
Siku zote nasema Mwigulu ni Janga kwa CCM zaidi ya CHADEMA, anapaka matope uwezo wa IGP, MKuu wa Upeleelezi na vyombo vyote vya dola vinaonekana haviwezi tena kurinda RAIA wake.

Anasahau kwamba RAIS wake ameapa kurinda maisha ya Watanzania wote siyo CCM peke yake.

IGP Kazi kwako chukua MWIGULU asaidie polisi au ENDELEA Kufedheheshwa!
 
Mwigulu namfananisha na Shetani ambaye siku zote hupenda kuona watu wakipata tabu.. Alikuja na apology yake ili kutuchota akili kuwa yeye ni msafi na ameshakiri madhaifu yake. Lengo ni kuwa likitokea tukio lingine tusimhusishe.. Ile apology aliitoa makusudi kabisa kucheza na akili zetu, and he failed big time!!!

Stupid Monger!!!
 
Kweli Mwigulu ni vizuri ukatafakari haya yote watu wanayokutuhumu.Tambua kwamba nje ya CCM,wewe ni mwananchi wa kawaida,unayetakiwa kujichanganya na jamii katika mambo mbalimbali.Kwa namna watu wanavyokuzungumzia,unaweka hata maisha yako hatarini.Hebu MUNGU akupe moyo wa huruma ili uweze kujitambua.Wenzako watakutumia,wao watabaki safi,wewe utabaki na lawama.MUNGU ibariki Tanzania,MUNGU ibariki Africa.
 
Kwa haya yanayotokea watakuja kuumbuka mchana kweupe tu mkuu!

Mwigulu soma Biblia uone jinsi ambavyo Mfalme SAULI alivyohangaika kumtafuta kijana Daudi lakini Baraka za Mungu zilisha hama kwake. CCM yapaswa kujua kwamba tayari Mungu ameshawapiga kisogo hivyo tmbueni kwamba kwa sasa mnaishi kwa huo ujanja ujanja tu lakini Baraka na mkono wa Mungu haupo tena pamoja nanyi, tafakari
 
natafakari tatizo la mwigulu liko wapi nadhani halipo ila kilichopo kwa mwigulu ni zile hoja zake nzito akiwa bungeni na nje ya bunge na amekuwa mkosoaji wa kwanza wa siasa dhaifu za chadema ikiwa ni pamoja na kuzichambua bajeti za chadema na kuonesha upungufu wake.

Ni ukweli usiopingika mwigulu hawezi kupendwa na chadema hata kama angekuwa padri au shehe,binafsi nahofia sana za siku hizi kwa sababu wako tayari kuuwa ili wao wapate sifa huu ni upuuzi lakini wanasiasa wakae wakijua kwamba uasi wanaofanya hautaishia duniani hata mungu anawamulika vema.
 
tafakari nyingine ambayo inanifanya niamini kuwa mwigulu anachukiwa kwa sababu za kisiasa tu hasa kwa wanachadema ambao wanaona chama chao kinaumizwa na mwigulu.

Hata wale wanaompinga mwigulu kwenye mitandao ya kijamii ni walewale wadau ambao wanaonekana ni wanachama wa chadema kutaka kuthibitisha hili ni vema kuwa msomaji wa post kwa za watu kwa mda mrefu utajua kuwa wanaompinga mwigulu ni walewale wapenzi wa chadema.
 
Mwigulu ni kama Ruge vile,kila mtu lawama kwake,ukiona unalalamikiwa na kila mtu ujue ww ni tatizo.
 
hakika Mungu ameona, mwigulu damu iliyo mwagika bila hatia ipo siku...........
 
kwa CHADEMA, mwingulu ni mume wenu na yeyote kati yenu anafyata mkia kila jina la huyu mtu likitajwa. nampongeza sana MWINGULU na kama ni mkuki, basi mkuki huu umewaingia moyoni swadakataa.
by the way!!! mungu ni tungo tata. mungu unaemuengelea wewe huenda ukawa unamaanisha ''THE SUPREME BEING"" Mungu wa FREEMASONS. na kwa ishara zenu za kichama, mavazi yenu, na mikutano yenu inavyoambatana na umwagaji damu ni wazi kuwa huyo ndie mungu unaemuamini na kumuongelea.
kwa watanzania wazalendo,wapenda amani, wanaowapenda watu na vizazi vyao,,,,, tunaamini katika mungu wa kweli, wa amani na upendo, asiyependa machafuko na umwagaji damu, asiyependa dharau na matusi na aliye wa kweli na hakika. mungu wetu ni ALPHA NA OMEGA na hashindwi na lolote.
mungu wetu anaichukia CHADEMA na ndio maana anaiua taratiiiiiiibuu huku mkishuhudia.Endeleeni kuegama katika mungu asiye na mashiko, apendaye damu za watu kama makafara na mwisho wa siku mtagundua mkiwa mmeshachelewa saaaana.
 
Nchemba ni muuaji ila wakuu wake wanajua kinachofanyika. Halafu Mbunge kama Cheyo naye ashughulikiwe kwani hana maana Bungeni ni mchumia tumbo tuu. Eti Spika anasema hana taarifa rasmi ya Taarifa ya Bajeti ya Upinzania kutosomwa hii ni aibu kweli kwa mwanamama huyu hata hana huruma kwa wafiwa, hivi ana watoto huyu jamani?
 
Back
Top Bottom