NusuMutu
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 421
- 87
Salaam ewe mheshimiwa! Pole kwa majukumu (yako pamoja na ya wale wanaolala na kukusubiri ufikirie badala yao). Treni la mjini aka treni la Mwakyembe lishaanza kuboa wateja hasa wa maeneo ya kariakoo na maeneo jirani maana linatoka posta limejaa pomoni na kutuaacha 'wananchi' macho kodo. Dereva wa treni alikua anatoa mkono kama wafanyavyo madereva wa daladala kuashiria 'nyomi' kwamba watu wamejaa. Mheshimiwa hebu tena waambie na uwaagize TRL nini cha kufanya maana akili zao ziliishia kwenye lile agizo lako la mwisho, pia mvua zaja, stend za hili daladala treni halina pa kujikinga patakuwa hapatoshi mkuu!