Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Mimi sio mshabiki wa CCM, lakini napenda kumuunga mkono Mh Zungu (kwa hoja ya umoja wa kitaifa) kwa hoja yake ya serikali kudhibiti matumizi ya magari ya ghali. Kwa ufupi tu, Mh Zungu aliongea yafuatayo
- Viongozi wa serikali Tz wanatumia magari ya gharama sana, yanayoongeza matumizi yasiyo ya lazima kwa serikali
- Serikali iwe na standard ya magari, kwa mfano Kenya wanatumia Volkswagen isipokuwa kwa viongozi wakuu wa serikali.
- Mh Zungu alisisitiza sana mawaziri watumia magari yao binafsi, kwa kupewa tu posho ya mafuta, kwa safari za kawaida
Kimsingi nakubaliana na Mh. Zungu, lakini hebu tuangalie mfano wa nchi nyingine ya Rwanda. Hii ni nchi ambayo hivi majuzi tu ilikuwa katika vita kubwa ya wenyewe, lakini kwa kasi ya maendeleo waliyo nayo leo, Tanzania hatuwagusi.
Kuhusiana na magari ya serikali inasemekana (kwa niliyoambiwa na mnyarwanda mmoja aliyeko serikalini),
Serikali humpa 50% ya fedha ya kununua, na kumkopesha 50% nyingine bila riba, lakini kwa masharti ya kukata deni lake kwenye mshahara kwa kipindi kilichoamuliwa. Kila mfanyakazi anakuwa na haki hii kila baada ya miaka mitatu, tokea alipopata gari moja.
Kila kiongozi anayestahili hupewa fixed amount ya posho ya mafuta kwa mwezi. Udhibiti umewekwa kwa makampuni yanayoagiza magari kiasi kwamba bei ya gari haiwezi kuchakachuliwa kwa manufaa ya kiongozi. Kiongozi (isipokuwa hao watatu), hapewi dereva na serikali, na kama anataka kuendeshwa basi anaajiri dereva kwa hela yake.
Zimewekwa gari maalumu ambazo zinatumika kama kiongozi anakwenda kikazi katika safari ambayo inahitajika kutumiwa gari maalumu ya serikali.
Kwa Utaratibu huu serikali ya Rwanda imeweza kudhibiti sana matumizi katika magari ya serikali.
Nadhani ndg Watanzania mnajua hali ikoje hapa kwetu...
- Viongozi wa serikali Tz wanatumia magari ya gharama sana, yanayoongeza matumizi yasiyo ya lazima kwa serikali
- Serikali iwe na standard ya magari, kwa mfano Kenya wanatumia Volkswagen isipokuwa kwa viongozi wakuu wa serikali.
- Mh Zungu alisisitiza sana mawaziri watumia magari yao binafsi, kwa kupewa tu posho ya mafuta, kwa safari za kawaida
Kimsingi nakubaliana na Mh. Zungu, lakini hebu tuangalie mfano wa nchi nyingine ya Rwanda. Hii ni nchi ambayo hivi majuzi tu ilikuwa katika vita kubwa ya wenyewe, lakini kwa kasi ya maendeleo waliyo nayo leo, Tanzania hatuwagusi.
Kuhusiana na magari ya serikali inasemekana (kwa niliyoambiwa na mnyarwanda mmoja aliyeko serikalini),
- Ni viongozi watatu tu wa serikali wanaopewa magari ya kutembelea; Raisi, Jaji Mkuu na Spika wa bunge
- Viongozi wengine wote wanatumia magari yao 'binafsi' kwa utaratibu ufuatao;
Serikali humpa 50% ya fedha ya kununua, na kumkopesha 50% nyingine bila riba, lakini kwa masharti ya kukata deni lake kwenye mshahara kwa kipindi kilichoamuliwa. Kila mfanyakazi anakuwa na haki hii kila baada ya miaka mitatu, tokea alipopata gari moja.
Kila kiongozi anayestahili hupewa fixed amount ya posho ya mafuta kwa mwezi. Udhibiti umewekwa kwa makampuni yanayoagiza magari kiasi kwamba bei ya gari haiwezi kuchakachuliwa kwa manufaa ya kiongozi. Kiongozi (isipokuwa hao watatu), hapewi dereva na serikali, na kama anataka kuendeshwa basi anaajiri dereva kwa hela yake.
Zimewekwa gari maalumu ambazo zinatumika kama kiongozi anakwenda kikazi katika safari ambayo inahitajika kutumiwa gari maalumu ya serikali.
Kwa Utaratibu huu serikali ya Rwanda imeweza kudhibiti sana matumizi katika magari ya serikali.
Nadhani ndg Watanzania mnajua hali ikoje hapa kwetu...