Mh Mnyika, ARE you serious? ni serikali ipi unaiongelea

Bongolander

JF-Expert Member
Jul 10, 2007
5,067
2,197
[h=2]wana JF kuna wakati naona huwa tunatumia vibaya uhuru wa kuongea tulio nao. NI mejaribu kuosma hii excerpt kutoka kwenye gazeti la Guardian Online version la tarehe 23 Januari. Mh mbunge John Mnyika anajaribu kutoa maoni kuhusu hali ya uchumi, hebu soma kidogo......

"Serikali ilete mpango wa kunusuru uchumi: Mnyika"[/h]
Mnyika ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Nishati na Madini, aliitaka Serikali kupeleka mpango wa dharura wa kuimarisha uchumi na kupunguza gharama za maisha kwa wananchi katika vikao vya kamati ya bunge vinavyoendelea kabla ya kuwasilisha katika mkutano wa bunge unaotarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu.

Mnyika aliitaka Serikali kuongeza uzalishaji na usambazaji wa vyakula katika soko la ndani pamoja na kuwawezesha wazalishaji wadogo na wa kati katika kilimo na viwanda ili kuongeza mauzo nje ya nchi.

“Serikali inapaswa kuharakisha matumizi ya gesi asilia na utekelezaji wa mpango wa dharura wa umeme…itekeleze mkakati wa kupunguza manunuzi yake ya nje kwa bidhaa na huduma ambazo zinapatikana nchini,” alisema Mnyika.


Hivi kweli anayoongea Mh Mnyika ni realistic? Nani atamsikiliza? Ni kweli serikali yetu kupitia waziri wa fedha Mustafa Mkullo ina uwezo wa kuja na plan ambayo inayoweza kurescue uchumi wetu? NI kweli serikali inaweza kuongeza uzalishaji na usambazaji wa chakula katika soko la ndani? Ni wapi serikali inakozalisha chakula? Au ndio yale ya kuongea jukwaani na kuwataka wananchi walime heka mbilimbili za mahindi bila kujali uwezo wao, hali ya hewa, shughuli zai kiuchumi au hata kama wtu wenyewe wanataka kufanya hivyo au la.

Anaposema serikali "itekeleze mkakati wa kupunguza manunuzi yake ya nje kwa bidhaa na huduma ambazo zinapatikana nchini" ni manunuzi gani yanayofanywa na serikali kwa bidhaa za nje zinazopatikana nchini?

Ukiangalia kwa undani inaonekana kuwa baadhi ya hoja zinatolewa na waheshimiwa wetu bila kuwa makini. Hivi kweli kwa serikali hii tuliyonayo sasa ambayo imeshindwa kuplan hata katika wakati usio emergency, inaweza kuplan nini cha dharura? katika full article mheshimiwa pia ameongelea issue ya umeme, sijui kama kweli anaelewa ni nini kinaendelea serikalini kuhusu issue nzima ya umeme. Serikali imeshindwa ku deal na suala la umeme toka day one, hivi kweli anaamini kuwa serikali hii inaweza kudeal na tatizo la umeme?

My point here is naona mheshimiwa anaongea vitu ambavyo ni unrealistic. Mh Mnyika najua unasoma hii post naamini utaifanyia kazi.
 
kaka fikiria wewe ni kaimu mkuu wa shirika,mkuu analiendesha kwa hasara na ufisadi na hafuati ushauri wako leo anaumwa hoi kitandani unatakiwa kumpa ushauri ili akipona aufuate.
na una uhakika ugojwa alionao ni mungu tu.
 
Ukiwa nje ya uwanja wa mpira ni rahisi kumkosoa kocha na wachezaji lakini ukiambiwa vaa jezi ukacheze au kuwa kocha wa timu mmmmh ngoma nzito. Ukiwa nje ya uwanja unaongea hata mambo ya kufikirika yasiyotekelezeka ni haki ya Mnyika kuwa msema chochote akiwa nje ya utawala
 
Kauli nyingine ni za mashindano ya kisiasa hazina uhalali wa kuwa halisi kimatendo kwenye mazingira halisi. heshima ya mwansiasa makini ni pamoja na kukosoa mambo yanayotekelezeka......inanikumbusha sera ya mapesa kama mtanichagua kuwa Rais wenu ( John Cheyo)
 
Post nyingine hizi huwa hazina hata mantiki! Tatizo la a lot of majority kama nyie mnakunywa sana gongo na valuu asubuhi asubuhi na unajifanya upo neutral kumbe nia yako ni kumponda mnyika. Huna chako humu JF and shame on you............. 2shakustukia gamba wewe.
 
kaka fikiria wewe ni kaimu mkuu wa shirika,mkuu analiendesha kwa hasara na ufisadi na hafuati ushauri wako leo anaumwa hoi kitandani unatakiwa kumpa ushauri ili akipona aufuate.
na una uhakika ugojwa alionao ni mungu tu.

Lakini pia anayetoa ushauri anaweza kuwa ni mgonjwa wa ...........ndiyo sababu kwenye sheria/viapo inasisitizwa sana neno ' awe na akili timamu'. Huwezi kupokea ushauri eti tu kwa sababu umeshauriwa vipo vigezo. Lakini pia mpinzani wako wa kisiasa anapokushauri ni muhimu kuchuja kila neno anaweza kuwa na dhamira mbaya ya kukuangusha. Ndipo unakuta unashauriwa mambo yasiyotekelezeka
 
wana JF kuna wakati naona huwa tunatumia vibaya uhuru wa kuongea tulio nao. NI mejaribu kuosma hii excerpt kutoka kwenye gazeti la Guardian Online version la tarehe 23 Januari. Mh mbunge John Mnyika anajaribu kutoa maoni kuhusu hali ya uchumi, hebu soma kidogo......

"Serikali ilete mpango wa kunusuru uchumi: Mnyika"



Mnyika ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Nishati na Madini, aliitaka Serikali kupeleka mpango wa dharura wa kuimarisha uchumi na kupunguza gharama za maisha kwa wananchi katika vikao vya kamati ya bunge vinavyoendelea kabla ya kuwasilisha katika mkutano wa bunge unaotarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu.

Mnyika aliitaka Serikali kuongeza uzalishaji na usambazaji wa vyakula katika soko la ndani pamoja na kuwawezesha wazalishaji wadogo na wa kati katika kilimo na viwanda ili kuongeza mauzo nje ya nchi.

"Serikali inapaswa kuharakisha matumizi ya gesi asilia na utekelezaji wa mpango wa dharura wa umeme…itekeleze mkakati wa kupunguza manunuzi yake ya nje kwa bidhaa na huduma ambazo zinapatikana nchini," alisema Mnyika.


Hivi kweli anayoongea Mh Mnyika ni realistic? Nani atamsikiliza? Ni kweli serikali yetu kupitia waziri wa fedha Mustafa Mkullo ina uwezo wa kuja na plan ambayo inayoweza kurescue uchumi wetu? NI kweli serikali inaweza kuongeza uzalishaji na usambazaji wa chakula katika soko la ndani? Ni wapi serikali inakozalisha chakula? Au ndio yale ya kuongea jukwaani na kuwataka wananchi walime heka mbilimbili za mahindi bila kujali uwezo wao, hali ya hewa, shughuli zai kiuchumi au hata kama wtu wenyewe wanataka kufanya hivyo au la.

Anaposema serikali "itekeleze mkakati wa kupunguza manunuzi yake ya nje kwa bidhaa na huduma ambazo zinapatikana nchini" ni manunuzi gani yanayofanywa na serikali kwa bidhaa za nje zinazopatikana nchini?

Ukiangalia kwa undani inaonekana kuwa baadhi ya hoja zinatolewa na waheshimiwa wetu bila kuwa makini. Hivi kweli kwa serikali hii tuliyonayo sasa ambayo imeshindwa kuplan hata katika wakati usio emergency, inaweza kuplan nini cha dharura? katika full article mheshimiwa pia ameongelea issue ya umeme, sijui kama kweli anaelewa ni nini kinaendelea serikalini kuhusu issue nzima ya umeme. Serikali imeshindwa ku deal na suala la umeme toka day one, hivi kweli anaamini kuwa serikali hii inaweza kudeal na tatizo la umeme?

My point here is naona mheshimiwa anaongea vitu ambavyo ni unrealistic. Mh Mnyika najua unasoma hii post naamini utaifanyia kazi.

:A S embarassed:
 
Post nyingine hizi huwa hazina hata mantiki! Tatizo la a lot of majority kama nyie mnakunywa sana gongo na valuu asubuhi asubuhi na unajifanya upo neutral kumbe nia yako ni kumponda mnyika. Huna chako humu JF and shame on you............. 2shakustukia gamba wewe.

wewe mwenye matusi ndiye unaonekana umekunywa gongo kama ningepewa kazi ya kuwapima nyinyi wawili. matusi ya nini? sisi wote tuna akili timamu hata bila kutukana tutakuelewa. Jenga hoja kaka siasa sio matusi.
 
Wewe unataka asemaje?
aendelee kulalamika kila siku kama wewe na bila kufanya kazi.
Grow up
OTIS
 
wana JF kuna wakati naona huwa tunatumia vibaya uhuru wa kuongea tulio nao. NI mejaribu kuosma hii excerpt kutoka kwenye gazeti la Guardian Online version la tarehe 23 Januari. Mh mbunge John Mnyika anajaribu kutoa maoni kuhusu hali ya uchumi, hebu soma kidogo......

"Serikali ilete mpango wa kunusuru uchumi: Mnyika"



Mnyika ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Nishati na Madini, aliitaka Serikali kupeleka mpango wa dharura wa kuimarisha uchumi na kupunguza gharama za maisha kwa wananchi katika vikao vya kamati ya bunge vinavyoendelea kabla ya kuwasilisha katika mkutano wa bunge unaotarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu.

Mnyika aliitaka Serikali kuongeza uzalishaji na usambazaji wa vyakula katika soko la ndani pamoja na kuwawezesha wazalishaji wadogo na wa kati katika kilimo na viwanda ili kuongeza mauzo nje ya nchi.

“Serikali inapaswa kuharakisha matumizi ya gesi asilia na utekelezaji wa mpango wa dharura wa umeme…itekeleze mkakati wa kupunguza manunuzi yake ya nje kwa bidhaa na huduma ambazo zinapatikana nchini,” alisema Mnyika.


Hivi kweli anayoongea Mh Mnyika ni realistic? Nani atamsikiliza? Ni kweli serikali yetu kupitia waziri wa fedha Mustafa Mkullo ina uwezo wa kuja na plan ambayo inayoweza kurescue uchumi wetu? NI kweli serikali inaweza kuongeza uzalishaji na usambazaji wa chakula katika soko la ndani? Ni wapi serikali inakozalisha chakula? Au ndio yale ya kuongea jukwaani na kuwataka wananchi walime heka mbilimbili za mahindi bila kujali uwezo wao, hali ya hewa, shughuli zai kiuchumi au hata kama wtu wenyewe wanataka kufanya hivyo au la.

Anaposema serikali "itekeleze mkakati wa kupunguza manunuzi yake ya nje kwa bidhaa na huduma ambazo zinapatikana nchini" ni manunuzi gani yanayofanywa na serikali kwa bidhaa za nje zinazopatikana nchini?

Ukiangalia kwa undani inaonekana kuwa baadhi ya hoja zinatolewa na waheshimiwa wetu bila kuwa makini. Hivi kweli kwa serikali hii tuliyonayo sasa ambayo imeshindwa kuplan hata katika wakati usio emergency, inaweza kuplan nini cha dharura? katika full article mheshimiwa pia ameongelea issue ya umeme, sijui kama kweli anaelewa ni nini kinaendelea serikalini kuhusu issue nzima ya umeme. Serikali imeshindwa ku deal na suala la umeme toka day one, hivi kweli anaamini kuwa serikali hii inaweza kudeal na tatizo la umeme?

My point here is naona mheshimiwa anaongea vitu ambavyo ni unrealistic. Mh Mnyika najua unasoma hii post naamini utaifanyia kazi.

Halafu hapa utasikia Pro-CDM wakisifia kuwa thread nzuri , kumbe jamaa ameongea upupu mtupu. Ndio huwa nasema siku zote Mnyika kichwani hamna kitu, mtabisha tu ila ndio ukweli.

 
Mimi hapa sijaelewa,unamulaumu Mnyika juu ya huo ushauri tarajiwa juu ya serikali au unailaumu serikali kwamba siyo sikivu kuwa haiwezi kutekeleza mapendekezo yake??!!
 
Mimi hapa sijaelewa,unamulaumu Mnyika juu ya huo ushauri tarajiwa juu ya serikali au unailaumu serikali kwamba siyo sikivu kuwa haiwezi kutekeleza mapendekezo yake??!!

Mkuu unajua ni kweli Mh Mnyika ana haki ya kutoa maoni yake. Lakini maoni anayotakiwa kutoa yanatakiwa kuwa maoni ambayo ni realistic, yeye ni mbunge kijana ambaye tumeweka hopes kwake. Mimi si pro Gamba, Gwanda au Ganda, mimi ni Pro Tanzania, na vijana kama Mnyika wenye uchungu na nchi ndio tegemei la Tanzania, bila kujali yeye ni Gwanda, Gamba au Ganda. Si mlaumu Mnyika kwa kutoka maoni, ila kinachoonekana ni kuwa maoni yake ni kama ya kinjozi njozi na kusadikika. Yanafanana ya yale ya demagogue politicians ambao wanaongea tu kwa kuwa wanaplatforms za kuongea.

'Kwa serikali isiyosikivu kama ya sasa ni vizuri unapoongea usiwape nafasi ya kusema "mnasikia wapinzani wanayoongea?", that ais my worry with Mnyika statements. Ingekuwa vema kama angeendelea kutoa sauti kubwa kuonyesha uozu uozu uozo, kuwafanya magamaba wajue kuwa wananchi tunaona wanachofanya ni pumba, ili wajitahidi kufanya la maana.
 
mnyika mdogo wangu jimbo lako la ubungo naona litakuwa gumu kulitetea.

hakuna ugumu kwa cdm zaidi 2015 mateso ni kwa magamba maana ninauhakika dar kama dar majimbo yote yatakwenda upinzani na baada ya hapo ccm ndio itaitwa chama cha upinzani dar
 
Ukiwa nje ya uwanja wa mpira ni rahisi kumkosoa kocha na wachezaji lakini ukiambiwa vaa jezi ukacheze au kuwa kocha wa timu mmmmh ngoma nzito. Ukiwa nje ya uwanja unaongea hata mambo ya kufikirika yasiyotekelezeka ni haki ya Mnyika kuwa msema chochote akiwa nje ya utawala

we kweli ni porojo tu, tushaona serikali hii imeshindwa tena sio hii tu hata ya nyuma na ya nyuma yake labda ya nyuma yake na hii!ilijitahidi sana na mungu amlinde na kumtunza mtangulizi wake na shujaa wetu, ipo siku tutapata wa kuvaa viatu vyake, hawa waliobaki tumwachie mungu atupe mbinu!tutawashinda na ulafi wake na mipango yao ya majukwaani tu!
 
Kuongeza uzalishaji si lazima serikali iwe inalima....hata kwa kuwapa wakulima mbegu bora na zinazokidhi mahitaji ya wakulima, na pia sasa badala ya kuwa wanatoa mbegu za aina moja,wanaweza toa mbegu za mazao ya chakula tofauti tofauti....na dawa za kudhibiti magonjwa yanayowafanya wakulima kushindwa kuzalisha chakula cha kutosha.

Kuhusu usambazaji,bado hii ni changamoto kubwa kwa wakulima wetu,kuna baadhi ya mazao yanaozea ndani kwenye maghala ya wakulima,hawana uwezo wa kusafirisha au pengine hata ule ufahamu wa namna ya kuuza mazao yao. Serikali inao wajibu wa kuhakikisha inawasaidia wakulimba kuuza mazao yao sehemu mbalimbali za Tanzania au hata nje ya Tanzania kama taifa liko vizuri.

Kuhusu ununuzi wa bidhaa za nje, mimi nimeshuhudia furniture nyingi za maofisini na baadhi za nyumba za viongozi zikiagizwa nje ya nchi kwa gharama kubwa sana na wala ubora wake si wa kiwango kikubwa. Tunao watanzania wenye uwezo mzur wakutengeneza baadhi ya bidhaa kama furniture japo si kwa wingi sana kumudu mahitaji lakini, wakiwezeshwa wanaweza au wakipewa order mapema,wanaweza hata kukaa kwa vkundi kutengeneza. Ni mfano tu.

Kuhusu kuzalisha gesi asilia, kuna makampuni mengi sasa yanataka kuwekeza kwenye uzalishwaji wa gesi asilia kwa matumizi ya nyumbani na viwandani. Ni juzi tu nimeona kampuni moja ya Renewable Projects Africa wakipita kukusanya taarifa kutoka kwa wakulima,kuweza kujua ni kiasi gani cha mbolea ya mifugo wanaweza pata ili kuzalisha gesi hiyo kwa wingi hapa Tanzania na walikuwa na wakifanya utafiti huo kushirikiana na afisa mifugo wa serikali.

Anayosema Mnyika yanawezekana,aungwe mkono kusukuma hawa viongozi wetu wazito kufanya kazi.
 
Anachokisema Mnyika ni realistik, we washawishi wenzako waiondoe CCM madarakani ndio utathibitisha kauli za mnyika kama ni realistic au la.
 
Binafsi natofautiana na mtoa hoja anaye mkosoa kwa nguvu Mh.Mnyika nachokiona hapa ni kwamba yy kawajibika kusema ambayo ndo kazi yake na pia kwa jinsi anavyoona sio kwamba haiwezekana ni kwa vile serikali ya ccm imeamua kuwasusa wapiga kura na kujilimbikizia mali.Hapa nn kikubwa sana ambacho hakiwezekani kama watu ni wawajibikaji?bongolander
 
wana JF kuna wakati naona huwa tunatumia vibaya uhuru wa kuongea tulio nao. NI mejaribu kuosma hii excerpt kutoka kwenye gazeti la Guardian Online version la tarehe 23 Januari. Mh mbunge John Mnyika anajaribu kutoa maoni kuhusu hali ya uchumi, hebu soma kidogo......

"Serikali ilete mpango wa kunusuru uchumi: Mnyika"



Mnyika ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Nishati na Madini, aliitaka Serikali kupeleka mpango wa dharura wa kuimarisha uchumi na kupunguza gharama za maisha kwa wananchi katika vikao vya kamati ya bunge vinavyoendelea kabla ya kuwasilisha katika mkutano wa bunge unaotarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu.

Mnyika aliitaka Serikali kuongeza uzalishaji na usambazaji wa vyakula katika soko la ndani pamoja na kuwawezesha wazalishaji wadogo na wa kati katika kilimo na viwanda ili kuongeza mauzo nje ya nchi.

“Serikali inapaswa kuharakisha matumizi ya gesi asilia na utekelezaji wa mpango wa dharura wa umeme…itekeleze mkakati wa kupunguza manunuzi yake ya nje kwa bidhaa na huduma ambazo zinapatikana nchini,” alisema Mnyika.


Hivi kweli anayoongea Mh Mnyika ni realistic? Nani atamsikiliza? Ni kweli serikali yetu kupitia waziri wa fedha Mustafa Mkullo ina uwezo wa kuja na plan ambayo inayoweza kurescue uchumi wetu? NI kweli serikali inaweza kuongeza uzalishaji na usambazaji wa chakula katika soko la ndani? Ni wapi serikali inakozalisha chakula? Au ndio yale ya kuongea jukwaani na kuwataka wananchi walime heka mbilimbili za mahindi bila kujali uwezo wao, hali ya hewa, shughuli zai kiuchumi au hata kama wtu wenyewe wanataka kufanya hivyo au la.

Anaposema serikali "itekeleze mkakati wa kupunguza manunuzi yake ya nje kwa bidhaa na huduma ambazo zinapatikana nchini" ni manunuzi gani yanayofanywa na serikali kwa bidhaa za nje zinazopatikana nchini?

Ukiangalia kwa undani inaonekana kuwa baadhi ya hoja zinatolewa na waheshimiwa wetu bila kuwa makini. Hivi kweli kwa serikali hii tuliyonayo sasa ambayo imeshindwa kuplan hata katika wakati usio emergency, inaweza kuplan nini cha dharura? katika full article mheshimiwa pia ameongelea issue ya umeme, sijui kama kweli anaelewa ni nini kinaendelea serikalini kuhusu issue nzima ya umeme. Serikali imeshindwa ku deal na suala la umeme toka day one, hivi kweli anaamini kuwa serikali hii inaweza kudeal na tatizo la umeme?

My point here is naona mheshimiwa anaongea vitu ambavyo ni unrealistic. Mh Mnyika najua unasoma hii post naamini utaifanyia kazi.

Bongolander,

Asante kwa maoni yako, sisi hatuongozi serikali kwa sasa kwa maana ya kuwa na Rais na mawaziri hivyo ili kutoa mchango wetu kwa taifa kusukuma maendeleo katika kipindi hiki mpaka uchaguzi mwingine utakapofanyika ni lazima tutimize vizuri wajibu wa kuisimamia hii serikali iliyopo madarakani. Ndio wajibu ambao naufanya.
Itakumbukwa kwamba Tarehe 28 na 29 Oktoba 2011 Waziri wa Fedha Mustapha Mkullo alinukuliwa na vyanzo mbalimbali akieleza kwamba mpango kabambe unatarajiwa kupitishwa na baraza la mawaziri kuboresha uchumi na kupunguza gharama za maisha. Kauli hiyo ya Waziri Mkullo aliitoa siku chache baada ya mkutano wangu na waandishi wa habari wa tarehe 23 Oktoba 2011 ambao nilitoa mwito kwa Rais Jakaya Kikwete kuitisha kikao cha dharura cha tume ya mipango na baraza la mawaziri kupanga mpango wa dharura na wa muda mrefu wa kupunguza gharama za maisha kwa wananchi kwa kudhibiti mfumuko wa bei pamoja na kuporomoka kwa shilingi ya Tanzania. Aidha, nilitoa mwito pia kwa bunge kuingilia kati kupitia kamati zake za kisekta na hatimaye kwa serikali kuwasilisha bungeni mpango wa kukabiliana na matatizo husika ya kiuchumi ambayo ni hatari kwa usalama wa nchi na maisha ya wananchi.

Miezi zaidi ya miwili imepita toka Waziri wa Fedha Mustapha Mkullo atoe ahadi kwa niaba ya serikali kuwa mpango kabambe unatarajiwa kupitishwa kuboresha uchumi na kupunguza gharama za maisha; ndio maana nimeendelea kuibana serikali ieleze mpango huo umefikia wapi ili kunusuru maisha ya wananchi.

Ikishindikana kwa njia za kawaida za kibunge itabidi tuelekee katika hatua za kuunganisha nguvu ya umma, ndio kazi mliyotutuma ya kuwawakilisha na kuwatumikia.

JJ
 
Back
Top Bottom