GeniusBrain
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 4,315
- 306
Tunasikitishwa sana na style ya uongozi ya Mh. Mdee ( Mbunge wa kawe). Wakati anaomba kura alikuwa mnyenyekevu ila baada ya kupata ubunge amekuwa sasa malkia kwa wananchi wake badala ya kuwatumikia kama alivyo ahidi. Nakumbuka moja ya ahadi zake wakati wa kampeni ni kutengeneza barabara ya msasani ambayo ina anzia hapa Tanesco na kuzunguka eneo la msasani kwa mamwinyi ndani ya miezi mine. Ila mpaka sasa hakuna lolote na barabara ile inazidi kuharibika. Sasa Mh. Mdee mbona umeahidi kitu ambacho hukiwezi ? sie tulikuchagua ututumikie sisi au ufanye u sista duu wako ?. Tafadhali acha huo utoto wako na tekeleza ahadi zako, hatukuelewi badala ya kushughulikia kero zetu wewe kila siku uko kwenye maandamano ya cdm