Mh Mbowe una kazi ya ziada kuiishi misingi ya mzee Mandela

gimmy's

JF-Expert Member
Sep 22, 2011
3,283
3,274
Kwa kipindi hiki ambacho dunia inaombeleza msiba wa tata madiba ni vema mh Mbowe akajitathimini upya.
Mbowe unapaswa kujiuliza je unaiishi misingi alioiacha Tata madiba?
Tata Madiba baada yakutoka gerezani na kushika uraisi wa Afrika ya kusini aliachia kwa hiari yake uraisi mara tu baada ya miaka mitano ya uongozi.
Udikteta wako utakiponza chama,
Mtu kutangaza nia yakuwania nafasi yako imekua nongwa?
hivi demokrasia ninini?
tambua chama si chako wala si mali ya kaskazini,
Hiki chama ni cha wanachama,
Wakati umefika kwa hiari yako uruhusu demokrasia itawale,
Naamini muhaini atakua ni yule anaegandamiza demokraisia,
Kumuondoa ZZK kimabavu ili uendelee kua mwenyekiti ni
ishara ya woga,
Tunajua ZZK kuitwa msaliti/mhaini ni kiini macho na hii ni janja ya nyani,
Hapo hujashika dola,
hemu tujiulize kwa pamoja kama CDM ingekuwa imeshika dola ie jeshi na mamlaka yote vipo chini ya CDM ZZK angepewa adhabu gani na huyu dikteta?
Tizama viongozi wako wanajiuzuru,
Tizama maandamano yakupinga udhalimu unaoufanya,
Ni vema ukamuenzi tata madiba kivitendo la sivyo siku si nying CDM itabaki kwenye vitabu vya historia!
 
Back
Top Bottom