Mikael Aweda
JF-Expert Member
- Dec 17, 2010
- 2,973
- 3,901
Mwasisi wa Chadema, M/kiti wa Chadema Taifa, na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni heshima yako. Leo naomba nikusumbue kidogo kuhusu salamu mpya ya kitaifa.
Hoja yangu;
Nchi yetu haina salamu rasmi ya kitaifa inayoweza kutumiwa ktk mikutano ya hadhara inayoshirikisha wananchi wa makundi yote (rika, vyama na dini)
Kuna salamu za makundi ya kijamii kama vyama kisiasa, Makundi ya kidini, rika nk, lakini hatuna salamu za kitaifa. Nitafafanua kwa kwa mfano;
Ukiwa kama M/kiti wa tume ya katiba Ukisimama mbele ya mkutano mkubwa wa hadhara wa watanzania wa mkundi yote, Jaji Joseph S. Warioba atatumia salamu gani kati salamu zilizoko hapo chini au atatumia zote kwa kuwa makundi yote yatawakilishwa ktk mikutano yake?
A)1 3 hapo juu ni za vyama, Warioba hajaenda kwa niaba ya chama cho chote.
B)3 4 ni inawakilisha makundi ya kidini Hakuna dini iliyomtuma
C) 5- 8 ni makundi ya rika yote yatakuwepo ktk mikutano. Je, anaweza kusema Shikamoni, habari, mambo vipi! Hamjambo nk.
Kwa maoni yangu hakuna salamu yo yote itakayomfaa Jaji warioba kati zote hizo zilizopo hapo juu. Vinginevyo, atalazimika kutumia zote - upotevu wa muda.
Ndiyo maana Rais mstaafu ndugu B.W.Mkapa nimemsikia mara kadhaa akiwa madarakani akizitumia salamu zote mpaka inachosha. Salam aleikum, bwana asifiwe, Tumsifu yesu kristo, vijana mambo! Wakubwa shikamoni, wanarika wenzangu habari nk.
Nimesikia pia John Mnyika mbunge wa Ubungo akijaribu mara nyingi kushirikisha makundi yote kama afanyavyo mzee Mkapa.
Jambo hili pia naona aliliona Mh Edward Ngoyai Lowasa pale alipoanzisha salamu za Hongera kwa kazi sikumbuki alipendekeza nini iwe mwitikio wake. Ila kabla hajaachia ngazi nimemsikia akilishikia bango.
Mapendekezo yangu.
Kwa kuwa makundi ya wanasisa na wananchi wote wanapenda amani, na
Kwa kuwa makundi ya dini za kikristo na kiislamu ndani ya salamu zao kuna neno amani, mfano wakristo (shalom = amani) waislamu ( Salaam aleikum = inahusisha amani)
Hivyo, basi napendekeza salamu za Taifa letu ktk mikutano inayohusisha watz wote bila kujali makundi ya kijami
iwe Nawatakia Amani, kiitikio cha wengi Ahsante nawe pia. ili tumrahisishie mzee Warioba kazi yake.Salamu hizi zitakuwa zinalenga kudumisha amani na umoja ktk nchi yetu.
Ni kwa sababu hii nimeamua kumtumia Kamanda wa Ukweli Freeman Aikaeli Mbowe apeleke hoja binafsi bungeni ili wabunge waijadili na kuipitisha. Si lazima wakubaliane na pendekezo langu, jambo la muhimu ni wao kuja na Salamu za kitaifa itakayowaunganisha watz wote. Najua tume ya katiba imeanza kazi ila mimi sidhani kama jambo hili linahitaji kusubiri katiba mpya. Vazi la Taifa limechukua miaka mingi, hata salamu za kitaifa linatushinda?
Ikumbukwe kuwa baadhi ya wanasiasa wanaotumia salamu hizi wanaposahau kundi mojawapo kutokana na uwepo wa makundi mengi labda kwa bahati mbaya inaleta hisia za ubaguzi kwa kundi lilisahauliwa. Jambo hili si jema.
Mwisho naomba nikupongeze Mh Mbowe kwa jinsi unavyoongoza chadema kwa mafanikio makubwa na ubunifu wa hali ya juu ikiwepo kauli mbio zenye kuleta tija ya M4C na vua gamba, vaa gwanda. Naamini hoja hii haitakataliwa na speaker.
Great thinkers naomba maoni yenu. Mbowe kazi kwako.
Hoja yangu;
Nchi yetu haina salamu rasmi ya kitaifa inayoweza kutumiwa ktk mikutano ya hadhara inayoshirikisha wananchi wa makundi yote (rika, vyama na dini)
Kuna salamu za makundi ya kijamii kama vyama kisiasa, Makundi ya kidini, rika nk, lakini hatuna salamu za kitaifa. Nitafafanua kwa kwa mfano;
Ukiwa kama M/kiti wa tume ya katiba Ukisimama mbele ya mkutano mkubwa wa hadhara wa watanzania wa mkundi yote, Jaji Joseph S. Warioba atatumia salamu gani kati salamu zilizoko hapo chini au atatumia zote kwa kuwa makundi yote yatawakilishwa ktk mikutano yake?
| Kikundi | mwanzisha salamu | Mpokea salamu | Maoni yangu |
1 | CCM | CCM HOYEE | HOYEE | Kwa wanaccm tu. |
2 | Chadema | Chadema | Vema | Wanacdm tu |
3 | CUF | Haki | Kwa wote | Wanacuf tu. |
4 | Waislamu | Asalaam Aleikum | Dini ya kiislamu | Makundi ya waislamu zaidi |
4 | Wakristo | Bwana asifiwe, tumsifu yesu kristo, shalom | Amin, tumsifu yesu kristo, shalom | Hii ni za makundi ndani ya dini ya kikristo. |
5 | Wadogo kwa wazima | Shikamoo | Marahaba. | Ina mipaka ya rika |
6 | Mkubwa kwa mdogo | Hamjambo | Hatujambo Shikamoo | Ina mipaka ya rika |
7 | Wenye umri sawa | Habari | Nzuri | Ina mipaka ya rika |
8 | Vijana kwa vijana | Mambo | Poa | Ina mipaka ya rika |
A)1 3 hapo juu ni za vyama, Warioba hajaenda kwa niaba ya chama cho chote.
B)3 4 ni inawakilisha makundi ya kidini Hakuna dini iliyomtuma
C) 5- 8 ni makundi ya rika yote yatakuwepo ktk mikutano. Je, anaweza kusema Shikamoni, habari, mambo vipi! Hamjambo nk.
Kwa maoni yangu hakuna salamu yo yote itakayomfaa Jaji warioba kati zote hizo zilizopo hapo juu. Vinginevyo, atalazimika kutumia zote - upotevu wa muda.
Ndiyo maana Rais mstaafu ndugu B.W.Mkapa nimemsikia mara kadhaa akiwa madarakani akizitumia salamu zote mpaka inachosha. Salam aleikum, bwana asifiwe, Tumsifu yesu kristo, vijana mambo! Wakubwa shikamoni, wanarika wenzangu habari nk.
Nimesikia pia John Mnyika mbunge wa Ubungo akijaribu mara nyingi kushirikisha makundi yote kama afanyavyo mzee Mkapa.
Jambo hili pia naona aliliona Mh Edward Ngoyai Lowasa pale alipoanzisha salamu za Hongera kwa kazi sikumbuki alipendekeza nini iwe mwitikio wake. Ila kabla hajaachia ngazi nimemsikia akilishikia bango.
Mapendekezo yangu.
Kwa kuwa makundi ya wanasisa na wananchi wote wanapenda amani, na
Kwa kuwa makundi ya dini za kikristo na kiislamu ndani ya salamu zao kuna neno amani, mfano wakristo (shalom = amani) waislamu ( Salaam aleikum = inahusisha amani)
Hivyo, basi napendekeza salamu za Taifa letu ktk mikutano inayohusisha watz wote bila kujali makundi ya kijami
iwe Nawatakia Amani, kiitikio cha wengi Ahsante nawe pia. ili tumrahisishie mzee Warioba kazi yake.Salamu hizi zitakuwa zinalenga kudumisha amani na umoja ktk nchi yetu.
Ni kwa sababu hii nimeamua kumtumia Kamanda wa Ukweli Freeman Aikaeli Mbowe apeleke hoja binafsi bungeni ili wabunge waijadili na kuipitisha. Si lazima wakubaliane na pendekezo langu, jambo la muhimu ni wao kuja na Salamu za kitaifa itakayowaunganisha watz wote. Najua tume ya katiba imeanza kazi ila mimi sidhani kama jambo hili linahitaji kusubiri katiba mpya. Vazi la Taifa limechukua miaka mingi, hata salamu za kitaifa linatushinda?
Ikumbukwe kuwa baadhi ya wanasiasa wanaotumia salamu hizi wanaposahau kundi mojawapo kutokana na uwepo wa makundi mengi labda kwa bahati mbaya inaleta hisia za ubaguzi kwa kundi lilisahauliwa. Jambo hili si jema.
Mwisho naomba nikupongeze Mh Mbowe kwa jinsi unavyoongoza chadema kwa mafanikio makubwa na ubunifu wa hali ya juu ikiwepo kauli mbio zenye kuleta tija ya M4C na vua gamba, vaa gwanda. Naamini hoja hii haitakataliwa na speaker.
Great thinkers naomba maoni yenu. Mbowe kazi kwako.