Mh Mbowe aunga mkono kitabu cha Yericko na kushauri vijana kuonyesha uthubutu kupitia vipaji vyao

NORTHERN ROCK

Senior Member
May 2, 2012
108
124
Katika ukurasa wa Yericko amelipoti kwamba:

"Leo nimekutana na kaka mkubwa kamanda wa Anga, Mwenyekiti wa Chadema Taifa na Kiongozi wa Upinzani Bunge Mh Freeman Mbowe.

Tumezungumza mengi kwa mapana yake, lakini kubwa yakigusa mambo ya kiusalama, siasa na mengineyo... Mh Mwenyekiti ameunga mkono juhudu zangu kwa kukinunua Kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, na kusema ni furaha kwake kuona vijana aliowalea na anaoendelea kuwalea kama mimi, wanaonyesha vipawa vyao na kuthubutu.

Mh Mwenyekiti amepongeza hatua yangu ya kuandika kitabu na kulitaja kama tukio la uthubutu. Amesisitiza kwamba vijana tutumie fursa zilizopo hasa kitendo cha kuwapo ndani ya chadema, tuonyesha vipawa vyetu bila woga, na zaidi amesema ili tudumu katika misimamo yetu ya kisiasa, ni vema vijana tukahakikisha tunakuwa na shughuli za kutuingizia vipato halali, hapo hatutarubuniwa na kuhamahama vyama.

Katika eneo lingine katikati ya mazungumzo yetu, Mh Mwenyekiti amesema Chadema na washirika wetu (UKAWA) tunapigana vita vya kisayansi dhidi ya adui yetu CCM, na kwa namna tunavyosonga tumewashinda maadui zetu, 2020 tutashinda kwa kishindo.

Mwisho amenizawadia zawadi maalumu ya kitabu kiitwacho The Spycraft Manual kilichoandikwa na Barry Davies, B.EM

Na Yericko Nyerere"
IMG_20171222_003944_920.jpg
IMG_20171222_130254_449.jpg
 
Hongera Yericko umethubutu....hivi bei haijapungua bado ili na sisi tufaidi yaliyomo.
 
Kwani yeriko ni kijana? Halafu yeriko kiboko alienda CCM Lumumba akawapa kitabu chake bure kaenda Chadema kawauzia.ee makubwa.Halafu utakuta anajitapa yeye Chadema damu!!!!!!
falsafa aliyoitumia Yericko wainjilisti wa vitabu wanaijua,kwa kuwagawia ccm bure na kuwauzia chadema
 
Mimi mwakani natoa kitabu changu "Tanzania baada ya Tanzania". Kwa sasa bado naendelea kupika!
 
Kwanza Hongera sana kwa ubunifu na juhudi zako kuandika kitabu. That is very highly commended and am impressed.

The issue I wish to raise here is that being an Author you don’t have to mix politics and your authorship, the book you write should be read by everybody, and as an Author you should not have any boundaries.

Try and separate your political affiliations and your literary ones. You have every right to be part of political side but only in politics. You should not separate those who may want to follow your literary work.

I also wonder how can you call people who don’t politically agree with you as enemies, jee Jana hukuwaona Mbowe NA Zitto wakiwa wamekaa kwenye hivyo viti ulivyokaa hapo kwenye picha yako.
 
Back
Top Bottom