Mh Mbowe atunukiwa cheti cha heshima na jamii ya waislamu

Majighu2015

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
2,924
3,904
MBUNGE wa Jimbo la Hai na Kiongozi wa Kambi rasmi Bungeni,Mh ,Freeman Mbowe ametunukiwa cheti cha heshima na jamii ya Waislamu katika wilaya ya Hai kutokana na jitihada zake zisizo na ukomo katika kuleta umoja katika Dini na Madhehebu mbalimbali.

“Tunaamini katka Uhuru wa kuabudu na kujieleza ,malumbano ya hoja na mijadala ,Kuvumiliana na kusamehe, Vitisho ,ugandamizaji na uonevu wa aina yoyote vinaweza kuendelea lakini havitaweza kushinda jamii yetu. Uhuru ni tunu ya sili tuliyopewa na Mwenyezi Mungu Mtukufu” yalieleza maeno yaliyopo katika Cheti hiycho.

Mh Mbowe alikabidhiwa cheti hicho na Mjumbe wa Baraza Kuu la Waisalmu (BAKWATA) Alhaji Habib Nasiwa , katika msikiti wa Lambo uliopo Machame wilayani muda mfupi baada ya kumalizika kwa hafla ya kushiriki futari iliyoandaliwa na mbunge huyo katika misikiti minne tofauti ya Modio ,Rundugai,Kibaoni na Lambo.

Cheti hicho kilichosainiwa na Sheakh Mkuu wa wilaya ya Hai,Sheakh ,Omary Mahmoud ambaye pia ni katibu wa msikiti wa Kibaboni Bomangombe kimetolewa ikiwa ni ni ishara ya kutambua mchango mkubwa unatolewa na Mbunge huo kwa Waislamu.
 
Kwanza mwenyekiti gani ambaye hataki kujiuzulu,wakati ni dhahiri chama kimemshinda,na katibu wake aliyemsimika kwa mkwara mzito ameflop vibaya.
 
JF kuna miujiza! Wale wanaokojoa hovyo kando ya barabara eti wanamshauri mkulima wa kisasa anayelima ndani ya banda (greenhouse) kuwa asichafue mazingira kama vile wanayajua!
We hujui mkojo wa bia ulivyo na protini.
 
MBUNGE wa Jimbo la Hai na Kiongozi wa Kambi rasmi Bungeni,Mh ,Freeman Mbowe ametunukiwa cheti cha heshima na jamii ya Waislamu katika wilaya ya Hai kutokana na jitihada zake zisizo na ukomo katika kuleta umoja katika Dini na Madhehebu mbalimbali.

“Tunaamini katka Uhuru wa kuabudu na kujieleza ,malumbano ya hoja na mijadala ,Kuvumiliana na kusamehe, Vitisho ,ugandamizaji na uonevu wa aina yoyote vinaweza kuendelea lakini havitaweza kushinda jamii yetu. Uhuru ni tunu ya sili tuliyopewa na Mwenyezi Mungu Mtukufu” yalieleza maeno yaliyopo katika Cheti hiycho.

Mh Mbowe alikabidhiwa cheti hicho na Mjumbe wa Baraza Kuu la Waisalmu (BAKWATA) Alhaji Habib Nasiwa , katika msikiti wa Lambo uliopo Machame wilayani muda mfupi baada ya kumalizika kwa hafla ya kushiriki futari iliyoandaliwa na mbunge huyo katika misikiti minne tofauti ya Modio ,Rundugai,Kibaoni na Lambo.

Cheti hicho kilichosainiwa na Sheakh Mkuu wa wilaya ya Hai,Sheakh ,Omary Mahmoud ambaye pia ni katibu wa msikiti wa Kibaboni Bomangombe kimetolewa ikiwa ni ni ishara ya kutambua mchango mkubwa unatolewa na Mbunge huo kwa Waislamu.
Hahahaha, hii Kali
 
Kwanza mwenyekiti gani ambaye hataki kujiuzulu,wakati ni dhahiri chama kimemshinda,na katibu wake aliyemsimika kwa mkwara mzito ameflop vibaya.
Wewe unanipa mashaka uelewa wako, Mbowe hakujipa tuzo yeye bali amepewa na viongozi wa dini, ingekuwa wewe kwa ufinyu wa uelewa wako labda na ukosefu wa heshima ugewakatalia. Lakini ulichokiandika hakihusiki na mada hii.
 
Wewe unanipa mashaka uelewa wako, Mbowe hakujipa tuzo yeye bali amepewa na viongozi wa dini, ingekuwa wewe kwa ufinyu wa uelewa wako labda na ukosefu wa heshima ugewakatalia. Lakini ulichokiandika hakihusiki na mada hii.
Mimi nina mashaka na hao waliomtunukia cheti labda ni umoja wa wachoma mkaa wa kiisilamu.
 
Back
Top Bottom