Mh Makamu wa Rais na Waziri Lukuvi tunaomba msaada wenu wa haraka tunakufa

Hakikwanza

JF-Expert Member
Dec 11, 2010
4,034
1,003
Mh Makamu wa Rais na mbunge wa jimbo la Ismani kwanza pole na majukumu yenu ya kila siku katika kulijenga taifa letu. Tunaungana moja kwa moja nanyi na serikali yetu katika kulisukuma gurudumu la maendeleo katika taifa hili na utekelezaji wa kauli mbiu ya Mh Rais ya HAPA KAZI TU . Kilio chetu ni huu utekelezaji wa sera ya mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Raisi Mazingira umekuwa mkali mno na hauja zingatia uhalisia uliopo kwa wakazi waishio pembezoni mwa mto Ruaha (ndogo).

Tumepokea ujumbe toka kwa uongozi wa vijiji vya tarafa ya Pawaga . Taarifa hiyo imesemwa kwa mdomo toka kwa viongozi wa vijiji vyetu inasema:-

-Tunatakiwa kutojihusisha na kilimo cha aina yeyote ile ndani ya mita sitini toka kwenye kingo za mto huu.
-Tunatakiwa kutovuta maji toka mtoni kwa kutumia mashine za kupampu maji.

Wakulima wamelikubali sharti la kwanza la kuachana na kilimo ndani ya mita sitini toka kingo za mto na kulitunza eneo hilo ikiwemo kupanda miti ya kuukinga mto kwa manufaa ya kizazi hiki na kijacho kwa moyo mkunjufu. Ila pendekezo la pili wamelipokea kwa masikitiko makubwa sana, simanzi na huzuni kubwa sana, kwani litaathiri maisha ya kila siku ya watu wote wa bonde hili la Pawaga. Ikumbukwe eneo hili linapata mvua kidogo sana kwa mwaka ambazo kwa kiasi kikubwa huwa hazisaidii kuivisha mazao mengine ukiacha mashamba ya mpunga unaolimwa chini ya mradi wa umwagiliaji.

Hivyo wakulima hulima bustani ndogo ndogo bondeni kwa kutumia mashine za kuvuta maji mtoni kustawisha mbogamboga kama nyanya, vitunguu, hoho, pilipili nk . Mzao haya husaidia kuboresha lishe za wakazi wa Pawaga na kutoa ajira kwa ujumla wake

Hivyo tunaomba swala hili liangaliwe upya kwani litatupa mateso makubwa ikiwepo utapiamulo na magonjwa mengine kwa ukosefu wa matumizi ya mboga mboga na dhana ya kila mtu afanye kazi litakuwa ndoto huku. Pia ajira itakuwa ni tatizo kwani kazi za kufanya zitakuwa hakuna na hivyo kuchochea uhalifu.

Baadhi ya picha za bustani ambazo toka sasa hazitapata maji na hatimaye kukauka na wakulima wake wamekopa mikopo kwa watu binafsi na taasisi za kifedha.
IMG_20170427_093547.jpg

IMG_20170427_094116.jpg

Mmiliki wa hii bustani hadi sasa ni mgonjwa BP ipo juu na ukimwona amejaa simanzi na huzuni kuu sana. Kwani hii bustani ni tegemeo lake kuendesha maisha
IMG_20170427_094645.jpg

Hii ni bustani ya mboga mboga ya mzee mwenye umri miaka 75 ipo hatarini kukauka kutokana na katazo la kutotumia maji ya Ruaha
IMG_20170427_092352.jpg

Hiyo ni mbegu ya vitunguu ambayo imemgharimu mwenye hilo shamba TSH 700,000/= hadi sasa na hatakiwi kuimwagia maji na ipo nje ya mita sitini
IMG_20170427_091622.jpg

Huyu ni mkulima wa nyanya na matikiti mpaka hapo ametumia zaidi ya TSH 800,000/= anatakiwa kuacha kumwagilia hadi hayo mazao yafe
 
Kwani hayo maji wanataka yafanyie kitu gani? Au wanataka yawe metered wawauzie?
Hatujajua kwani tumejeribu kwenda kwa mamlaka ya bonde wanakataa kutoa vibali na wametupa wiki moja kutofanya shughuli yoyote ile wakati watu bado wanamazao machanga
 
Piga chini ccm 2020 lakini kama imekutendea mema naomba muichague tena kwa kishindo 2020
Mkuu hali hii imeleta hasira kubwa kwa wananchi kwani wengi wamewekeza kwa kupanda mazao kama vitunguu hivyo wanatakiwa kushuhudia vikikauka kwa macho yao. Inasikitisha sana
 
Mkuu hali hii imeleta hasira kubwa kwa wananchi kwani wengi wamewekeza kwa kupanda mazao kama vitunguu hivyo wanatakiwa kushuhudia vikikauka kwa macho yao. Inasikitisha sana
Sirikali yetu hii hii, watu wanafanya maamuzi bila kujali wananchi wanaumia vipi na bado kuna nyumbu wanashadadia. Yaani unatamani kuwanywa supu kabisa nyumbu hao wenye mfanano na binadamu
 
Hili tatizo limekuwa ni la miongo mingi sana. Watendaji wa serikali kufanyia maamuzi ofisini wakiwa na vikombe vya kahawa ni tatizo sugu lililoota ukurutu. Kwa nin wasiwe wanakwenda kujionea moja kwa moja na kuzungumza na wahusika wanaoguswa moja kwa moja na hilo jambo! Nawaza tu kwa sauti
 
Sirikali yetu hii hii, watu wanafanya maamuzi bila kujali wananchi wanaumia vipi na bado kuna nyumbu wanashadadia. Yaani unatamani kuwanywa supu kabisa nyumbu hao wenye mfanano na binadamu
Ni kweli ndugu maamuzi yanafanyika bila kufanya tathimini ya kina ya zoezi zima kwa kuangalia faida na hasara. Ni kweli juhudi za kupanda miti rafiki wa maji ni muhimu. Mimi binafsi nimekuwa nikihimiza kupanda miti hiyo kwenye mita sitini za kingo za mto ili ututunze sisi na kizazi kijacho
 
Hili tatizo limekuwa ni la miongo mingi sana. Watendaji wa serikali kufanyia maamuzi ofisini wakiwa na vikombe vya kahawa ni tatizo sugu lililoota ukurutu. Kwa nin wasiwe wanakwenda kujionea moja kwa moja na kuzungumza na wahusika wanaoguswa moja kwa moja na hilo jambo! Nawaza tu kwa sauti
Tena naomba sauti yako isikike wasikie. Na hiyo ndiyo shida kubwa ya viongozi wetu wamekuwa wa ofisini na sio field area
 
Hakika hili la kukataza kuvuta maji toka mtoni kwa pampu (Hata kama shamba lipo mita 900 toka kingo za mto) ni pigo kwa walala hoi waliokuwa wakijipatia riziki zao kwa kilimo cha mboga mboga na mpunga. Serikali iliangalie upya suala hili.
 
Egypt kwa kutumia mto Nile tu imefanya massive irrigation schemes na imeweza kuwa agricultural producer mzuri tu. sasa huku kwetu tatizo nini?
 
Hakika hili la kukataza kuvuta maji toka mtoni kwa pampu (Hata kama shamba lipo mita 900 toka kingo za mto) ni pigo kwa walala hoi waliokuwa wakijipatia riziki zao kwa kilimo cha mboga mboga na mpunga. Serikali iliangalie upya suala hili.
Mkuu kunawanafunzi wamemaliza Chuo kikuu cha Mkwawa wamelima kitunguu ili kujikwamua na tatizo la ajira nao kitunguu chao kipo mbioni kukauka. Inasikitisha sana
 
Wanataka maji yakajaze bahari bure tu nchi hii inaviongozi pumba kabibisa wanaofikiri kwa kutumia kiungo gani cha mwili!!
 
Wanataka maji yakajaze bahari bure tu nchi hii inaviongozi pumba kabibisa wanaofikiri kwa kutumia kiungo gani cha mwili!!
Hatuja jua lengo lao hasa kwani maamuzi hayajatushirikisha wananchi wa eneo husika tulicho ambiwa ni operation. Jamani ni shida kwa kweli watu wameambiwa hakuna kutumia mashine wakati mazao yao yamepandwa kabla ya hiyo operation. Watu wamekopa fedha toka vyanzo mbali mbali ili wajikwamue kiuchumi serikali inawaangamiza Mh Lukuvu tunakuomba uokoe jahazi hili huku jimboni kwako
 
Jamani tunaomba msaada wenu kutufikishia kilio hiki kwa waheshimiwa pia walioko office ya makamu wa Rais mazingira juu ya kilio chetu kwani mitaji yetu inateketea
 
Msaada wa mawazo wakuu

Kilimo ni uwekezaji na ni biashara kubwa, mashamba yote makubwa duniani hayatumii maji ya mito bali wanachimba visima (deep boreholes), mjipange muwe vikundi na mchimbe bisima na mgawane maji, mto Ruaha umekauka kweli na soon utapotea kwenye ramani ya Dunia, ulikiwa ni mto usiokauka maji sasa umekuwa seasonal river
 
Back
Top Bottom