Mh. Magufuli anarudisha mfumo wa chama kimoja kupitia dirishani

TL. Marandu

JF-Expert Member
Jul 12, 2015
3,625
5,807
Naendelea Kushitushwa, Na kauli, Teuzi, Na mambo mbalimbali ya anayofanya Rais Magufuli Kisiasa huku akisema ati kusiwepo na Shughuli za Kisiasa hadi hapo 2020. Lakini Kwa Kasi na Kwa Makusudi Kabisa, Magufuli anapambana na Mfumo wa Demokrasia Uliokuwepo.
1)Anazuia Matangazo ya Moja Kwa Moja ya Bunge tena Kwa Visingizio vya Uwongo
2)Kama alivyo ahidi anawapa Ukurugenzi wa Vilaya na Miji Makada wa ccm pekee tena wale ambao waligombea Ubunge na eidha kukosa tiketi au Kushidwa Uchaguzi.
3)Anawaagiza Polisi wapige Marufuku Shughuli za Kisiasa za Vyama Vingine, Ikiwa Ni Pamoja na Sherehe, Mikutano, Maandamano, Na Masikini hata Kuzika wafu wao (Alfonzo Mawazo)
4)Kupeleka Askari Bungeni Kupiga wabunge ili Kuwatisha.
5)Kukamata Viongozi wa Upinzani ovyo kwa vile tu wanatoa Mawazo yao.
6)Kutuma Polisi Kuwinda Wanasiasa na Viongozi wa Jamii kwa Kupingana na Rais.
7)Kila anayemteua hata Kwenye Nafasi za Kitaalamu lazima awe CCM. Imebakia tu waalimu na Madaktari wote wawe ni CCM. Labda Ndio Maana akafukuzilia wale watoto 7000 Mitaani, ili apate nafasi ya Kuwarudisha wale ambao ni CCM, Ili Kizazi Kijacho Kiwe Na waalimu ambao Ni CCM Tu.

Bila Unafiki, Kwa Mtu anayefikiri na Anayekubali Ukweli, Huko Ndiko Magufuli anaipeleka Tanzania Yetu. Nani anaweza Kuniambia Kuwa Ni Jambo Jema? Hata kwa CCM sio Jambo Jema. Ni sawa na Bondia Unaenda Ulingoni Kwenye Pambano na Bondia Mwingine, Halafu Unashangaa Wanatokea Mapolisi na Mabaunsa wanamkamaata Mpinzani wako, Wanamfunga Kwa Minyororo Mikono Na Miguu kisha Wanapiga Filimbi na Kukuambia Uanze Kupigana Naye! Ukiwa Mnyama Utafanya hivyo, Ukiwa na Utu, Na Anayetunza heshima yake. Utavua Gloves na Kushuka Ulingoni, huku Ukiwaambia, "Ninyi Mna Wazimu, Not Me!"

Sasa Kama Katika Michezo Tu Hili swala halifai, litafaaje Kwenye Maisha halisi ya Watu wa Nchi, Bila Ushabiki wa Kisiasa Tujiulize! Huko Tunakondelea aipoacha "ujancha huu uchwara" Atalitumbukiza Taifa Katika Civil War. Na Sichochei Kitu chochote Nyinyi Wanafiki Mnayembatiza Kila anayetabiri Kwa Kuangalia Mwenendo Ni Mchochezi, Basi Kama Mimi Ni Mchochozi kwa Kutabiri yanayoweza Kutokea, Na Mwalimu Naye alichochea aliposema tukiendeleza kubaguana, Hatutabaki wamoja, "tutachinjana"



Uteuzi wa wakurugenzi 187 wazua hofu

Video Niliyosema Haya Yatatokea. Ilikuwa Ni Kabla ya Uchaguzi.
 
Meku TL Marandu punguza kulia lia tu,unataka ateue chadema halafu waamriwe na mwenyekiti wao kugoma?
Angalia mameya tu wa ukawa wote marufuku kuhudhuria sherehe za serikali,je kungekuwa na ma Rc na ma Dc wa ukawa?
Mliambiwa mtaisoma namba ndio hivi,tufanye kazi tu,mie najua unalia akina meku wamepigwa chini,wengi walikuwa wapigaji tu
 
Meku TL Marandu punguza kulia lia tu,unataka ateue chadema halafu waamriwe na mwenyekiti wao kugoma?
Angalia mameya tu wa ukawa wote marufuku kuhudhuria sherehe za serikali,je kungekuwa na ma Rc na ma Dc wa ukawa?
Mliambiwa mtaisoma namba ndio hivi,tufanye kazi tu,mie najua unalia akina meku wamepigwa chini,wengi walikuwa wapigaji tu
Hapana Nafasi za Kisiasa Kv. Uwaziri zinajulikana, Lakini Nafasi za Utendaji Kama Wakurugenzi wa Majiji, Makatibu wakuu wa Wizara, Maktibu tawala wa Mikoa na Wilaya, Majaji, Mawakili wa Serikali, Mahakimu, Wakuu wa Majeshi etc, Humwangalii Mtu chama. Ni hatari sana! Pia Nalozungumzia hapa Ni Mazingira anayotengeneza ya Mfumo wa Chama Kimoja Kwa Mlango wa Nyuma. Anayeshabikia Kitu hii ajitafakari sana!
 
Ili uwe kiongozi haihitaji kuwa na elimu kubwa.
Uongozi ni karama.
 
Hapana Nafasi za Kisiasa Kv. Uwaziri zinajulikana, Lakini Nafasi za Utendaji Kama Wakurugenzi wa Majiji, Makatibu wakuu wa Wizara, Maktibu tawala wa Mikoa na Wilaya, Majaji, Mawakili wa Serikali, Mahakimu, Wakuu wa Majeshi etc, Humwangalii Mtu chama. Ni hatari sana! Pia Nalozungumzia hapa Ni Mazingira anayotengeneza ya Mfumo wa Chama Kimoja Kwa Mlango wa Nyuma. Anayeshabikia Kitu hii ajitafakari sana!
Nyinyi mumlaumu mwenyekiti wenu ambae amegeuza sasa siasa kuwa uadui na serikali,JPM hakuwa hivyo, JPM alitaka kufanya kazi na nyinyi lakini mwenyekiti wenu anawaza zaidi uchaguzi 2020 kuliko maendeleo ya watanzania, ana siasa za kishindani ambazo hazina msingi, na JPM anaona anaamua sasa kubadili uelekeo, ndio hapo vijana mnaotegemea JPM awakumbuke wakati mpo chumba cha pili mnalalamika, mjaribu kumcontrol mwenyekiti wenu, au mumuombe akasomee ata kadiploma ka political science labda anaweza kubadilika, ona sasa anavyowafungia milango vijana wake, ata ningekuwa mimi nachagua wa karibu yangu, nyie wengine mnaweza kuwa mamluki wa kusambaza siri za serikali kwa Mbowe.
 
Hapana Nafasi za Kisiasa Kv. Uwaziri zinajulikana, Lakini Nafasi za Utendaji Kama Wakurugenzi wa Majiji, Makatibu wakuu wa Wizara, Maktibu tawala wa Mikoa na Wilaya, Majaji, Mawakili wa Serikali, Mahakimu, Wakuu wa Majeshi etc, Humwangalii Mtu chama. Ni hatari sana! Pia Nalozungumzia hapa Ni Mazingira anayotengeneza ya Mfumo wa Chama Kimoja Kwa Mlango wa Nyuma. Anayeshabikia Kitu hii ajitafakari sana!
Lol! Wachaga bana
 
si mlisema hamumtambui raisi pamoja na serikali yake?? sasa mnalialia nn?? kama serikali hamuitambui, mnafatilia hizi teuzi ili iweje?? hebu kojoa ukalale
 
si mlisema hamumtambui raisi pamoja na serikali yake?? sasa mnalialia nn?? kama serikali hamuitambui, mnafatilia hizi teuzi ili iweje?? hebu kojoa ukalale
Umeshawahi Kutulia Dakika tano kufikiri Kabla ya Kuongea au Ukamsikiliza Mtu na Kuelewa anasema Nini Kabla ya Kumtukana?
 
Naendelea Kushitushwa, Na kauli, Teuzi, Na mambo mbalimbali ya anayofanya Rais Magufuli Kisiasa huku akisema ati kusiwepo na Shughuli za Kisiasa hadi hapo 2020. Lakini Kwa Kasi na Kwa Makusudi Kabisa, Magufuli anapambana na Mfumo wa Demokrasia Uliokuwepo.
1)Anazuia Matangazo ya Moja Kwa Moja ya Bunge tena Kwa Visingizio vya Uwongo
2)Kama alivyo ahidi anawapa Ukurugenzi wa Vilaya na Miji Makada wa ccm pekee tena wale ambao waligombea Ubunge na eidha kukosa tiketi au Kushidwa Uchaguzi.
3)Anawaagiza Polisi wapige Marufuku Shughuli za Kisiasa za Vyama Vingine, Ikiwa Ni Pamoja na Sherehe, Mikutano, Maandamano, Na Masikini hata Kuzika wafu wao (Alfonzo Mawazo)
4)Kupeleka Askari Bungeni Kupiga wabunge ili Kuwatisha.
5)Kukamata Viongozi wa Upinzani ovyo kwa vile tu wanatoa Mawazo yao.
6)Kutuma Polisi Kuwinda Wanasiasa na Viongozi wa Jamii kwa Kupingana na Rais.
7)Kila anayemteua hata Kwenye Nafasi za Kitaalamu lazima awe CCM. Imebakia tu waalimu na Madaktari wote wawe ni CCM. Labda Ndio Maana akafukuzilia wale watoto 7000 Mitaani, ili apate nafasi ya Kuwarudisha wale ambao ni CCM, Ili Kizazi Kijacho Kiwe Na waalimu ambao Ni CCM Tu.

Bila Unafiki, Kwa Mtu anayefikiri na Anayekubali Ukweli, Huko Ndiko Magufuli anaipeleka Tanzania Yetu. Nani anaweza Kuniambia Kuwa Ni Jambo Jema? Hata kwa CCM sio Jambo Jema. Ni sawa na Bondia Unaenda Ulingoni Kwenye Pambano na Bondia Mwingine, Halafu Unashangaa Wanatokea Mapolisi na Mabaunsa wanamkamaata Mpinzani wako, Wanamfunga Kwa Minyororo Mikono Na Miguu kisha Wanapiga Filimbi na Kukuambia Uanze Kupigana Naye! Ukiwa Mnyama Utafanya hivyo, Ukiwa na Utu, Na Anayetunza heshima yake. Utavua Gloves na Kushuka Ulingoni, huku Ukiwaambia, "Ninyi Mna Wazimu, Not Me!"

Sasa Kama Katika Michezo Tu Hili swala halifai, litafaaje Kwenye Maisha halisi ya Watu wa Nchi, Bila Ushabiki wa Kisiasa Tujiulize! Huko Tunakondelea aipoacha "ujancha huu uchwara" Atalitumbukiza Taifa Katika Civil War. Na Sichochei Kitu chochote Nyinyi Wanafiki Mnayembatiza Kila anayetabiri Kwa Kuangalia Mwenendo Ni Mchochezi, Basi Kama Mimi Ni Mchochozi kwa Kutabiri yanayoweza Kutokea, Na Mwalimu Naye alichochea aliposema tukiendeleza kubaguana, Hatutabaki wamoja, "tutachinjana"



Uteuzi wa wakurugenzi 187 wazua hofu

Video Niliyosema Haya Yatatokea. Ilikuwa Ni Kabla ya Uchaguzi.

Rais anafanya sahihi,anaweka watu anaoweza kuwatuma na wakafanya kazi,ukiwa kiongozi lakini subordinates wako huwezi kuwatuna na wakatekeleza basi uongozi wako hautakuwa na mwendo mzuri,mpe muda muheshimiwa kitu cha msingi ni kuangalia kama kweli ana dhamira ya kweli ya kuitoa Tanzania hatua moja kwenda nyingine ama la,bila dhamira hiyo hata akieneza maprofesa katika kila nyanja we are doomed b4 the start.
 
jibu swali: mlisema hamumtambui raisi, sasa ivi mmeanza kumtambua??
Kama Jibu Unalolitaka Ni Kuwa Magufuli alishinda Kihalali Jibu NI NO, Hata Yeye anajua, Lakini Kwa Africa Hilo la Watu kuingia kwenye Madaraka Kwa Njia ya Kupiga "Fatuma" sio geni. Lakini Rais akishatangazwa Kwa Mfumo uliopo ni Kuwa Huwezi Kwenda Kupinga Mahakamani. Wapinzani waliingia Uchaguzi wakiwa Na mentality Kuwa Something is Better than Nothing. Lakini the truth is CCM hawapo Tayari Kushindwa Kwenye Urais.
Kama Magufuli alishinda Kihalali, Kwanini Kwenda Kuvamia Vituo na Kunyang'anya Kompyuta. Kwa Nini hii Mikakati ya sasa ya Kuua Demokrasia Kama anajua alichaguliwa Kihalali hofu ni nini.

N second of All siombi Magufuli amchague Mchadema au MuAct kwenye Teuzi, Ila Kisheria na Kikatiba Na kwa Maslahi ya Umoja na Amani ya Taifa Kuna Nafasi za Utumishi serikalini ambazo sisi za Kisiasa. Ukiingiza Siasa Katika Nafasi Hizo Unaitakia Nchi Matatizo. Sasa Kama Ninyi CCM Hamwoni hayo mimi siwezi kukusaidia au Kupasua kichwa chako kuingiza ninayoamini ni ya Msingi, Siku ukiamka ukafunguka macho utajua nachokisema, hofu yangu isiwekuwa too late kurudi nyuma.
 
Kwa mfumo tunaoenda nao ipo siku unabii utatimia.. Ubakaji wa demokrasia na katiba.. Walioapa kuiliñdà katiba leo hii ndo wanaibaka....tutafika tu
 
Silent dectotorism inatokea kama hivyo utaanzisha umamluki kwenye vyama pinzan, utacontrol watumishi wasiweze paza sauti itakapowadharau, muundo wenye kukusujudia kiutendaji, kudharau mamalaka ya nje ya nchi, na kimataifa, kujitengenezea muundo wenye lengo la kujitofautisha, kuminya uhuru wa watu ili yako yaonekane kwa wingi, uteke nyoyo za watu kwa maendeleo na mipango uchwara na kweli wataitikia Kwa nguvu kwa kuwa weng ni wajinga, utaandaa vema bunge ufanye inalotaka hata kuongeza muda wa kuomgoza, kuvipa vyombo majukumu yasiyo yao Kwa maslahi yako,

Nasema tz sijui watakubali
 
Kama Jibu Unalolitaka Ni Kuwa Magufuli alishinda Kihalali Jibu NI NO, Hata Yeye anajua, Lakini Kwa Africa Hilo la Watu kuingia kwenye Madaraka Kwa Njia ya Kupiga "Fatuma" sio geni. Lakini Rais akishatangazwa Kwa Mfumo uliopo ni Kuwa Huwezi Kwenda Kupinga Mahakamani. Wapinzani waliingia Uchaguzi wakiwa Na mentality Kuwa Something is Better than Nothing. Lakini the truth is CCM hawapo Tayari Kushindwa Kwenye Urais.
Kama Magufuli alishinda Kihalali, Kwanini Kwenda Kuvamia Vituo na Kunyang'anya Kompyuta. Kwa Nini hii Mikakati ya sasa ya Kuua Demokrasia Kama anajua alichaguliwa Kihalali hofu ni nini.

N second of All siombi Magufuli amchague Mchadema au MuAct kwenye Teuzi, Ila Kisheria na Kikatiba Na kwa Maslahi ya Umoja na Amani ya Taifa Kuna Nafasi za Utumishi serikalini ambazo sisi za Kisiasa. Ukiingiza Siasa Katika Nafasi Hizo Unaitakia Nchi Matatizo. Sasa Kama Ninyi CCM Hamwoni hayo mimi siwezi kukusaidia au Kupasua kichwa chako kuingiza ninayoamini ni ya Msingi, Siku ukiamka ukafunguka macho utajua nachokisema, hofu yangu isiwekuwa too late kurudi nyuma.
Huu wimbo wa computer na tally center umeimbwa sana,hivi ni kweli kwamba bila tally centre ukawa wasingeshinda? Au tally center ndio ilikuwa strategy pekee ya kushindia,inanipa maswali ya kutaka kujua nini kilikuwa nyuma ya kituo hiki, hivi kwa mfano ukawa wangeweka picha ya ripoti za matokeo ya kila jimbo kwenye website yao si ingesaidia kuondoa huu utata,nashindwa kuelewa hiki kituo kingesaidia vipi kuleta ushindi na kufungwa kwake kumeondoaje ushindi.
 
Huu wimbo wa computer na tally center umeimbwa sana,hivi ni kweli kwamba bila tally centre ukawa wasingeshinda? Au tally center ndio ilikuwa strategy pekee ya kushindia,inanipa maswali ya kutaka kujua nini kilikuwa nyuma ya kituo hiki, hivi kwa mfano ukawa wangeweka picha ya ripoti za matokeo ya kila jimbo kwenye website yao si ingesaidia kuondoa huu utata,nashindwa kuelewa hiki kituo kingesaidia vipi kuleta ushindi na kufungwa kwake kumeondoaje ushindi.
Lengo La Kuzipora kwa Kutumia Polisi lilikuwa Ni nini? Hata Mtoto wa Darasa la Nne anaweza Kuona hiyo rafu!
 
Kwa kweli hali hii imetukatisha sana tamaa wengi
Mbaya zaidi hawa vijana huku kitaa wanatunanga sana sana kwa vyeo walivyopewa
 
Kuimalika kwa CCM ndo kunawatisha wapinzani na kweli watapotea. Hata Mkumbo alishawaambia wapinzani msipoweza kubadilika mtapotea fasta, JPM ni habari nyingine. Endeleeni kulia lia kama vichanga mawodini na wakati tayari tushaingiza gia sie.
 
Kwa kweli hali hii imetukatisha sana tamaa wengi
Mbaya zaidi hawa vijana huku kitaa wanatunanga sana sana kwa vyeo walivyopewa
Usuda tu ndo unakusumbua, na bado mpaka muisome namba yote.
 
Back
Top Bottom