Ta Muganyizi
R I P
- Oct 19, 2010
- 5,361
- 2,734
Katika hali ambayo mie siielewi ni ile ya mtu mmoja kuwa na madaraka nyeti kana kwamba yeye pekee ndo kaenda shule. Au ndo tuseme serikali inabana matumizi kwa kumneemesha mmoja tu alafu wengine wabaki bila kazi? Yeye ni mbunge kule kwao kusini, bado ni mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, bado ni waziri wa nchi Sera na Bunge why! Sasa mie ninachojua ni kuwa kwa vyeo hivi kila cheo unapewa dreva na gari. Kwa Ukuu wa Mkoa na Uwaziri Ulinzi unakuwepo. Sasa yeye ana magari mangapi ya Serikali, dreva wangapi na walinzi wangapi na ni kwa busara zipi alizonazo huyu bwana mpaka mtu mmoja afanye shughuli tatu alone? Ufanisi upo kweli hapo. Wanaojua nisaidieni Mtanzania mwenzenu.