Mh. Lissu naomba ukishinda uikuze elimu yetu angalau mtu akifika chuo kikuu aongee Kiingereza kwa ufasaha

James Martin

JF-Expert Member
Apr 2, 2016
1,206
1,509
Mh. Lissu naamini kuna haja ya kupitia mfumo wa elimu yetu hapa Tanzania.

Nimetumia mfano wa lugha ya Kiingereza kama kipimo kwasababu tunawasikia watu wakijaribu wakikiongea. Inawezekana yako masomo mengine pia yanayotakiwa yakuzwe lakini kwa sasa hatujui.

Wapo watakaosema mbona Urusi na China hawaongei Kiingereza. Tofauti ni kwamba wao sio omba omba kama sisi. Sisi bado tunatakiwa kuiongea lugha ya "kibeberu" kwa ufasaha ili kuweza kuomba mikopo!

Najua Mh. Lissu utanielewa kwasababu unaipenda lugha ya Kiingereza. Halafu pia Kiingereza chako ni kizuri kuliko changu, I can't reach you! (sikufikii wewe)
 
Mh. Lissu naamini kuna haja ya kupitia mfumo wa elimu yetu hapa Tanzania.

Nimetumia mfano wa lugha ya Kiingereza kama kipimo kwasababu tunawasikia watu wakijaribu wakikiongea. Inawezekana yako masomo mengine pia yanayotakiwa yakuzwe lakini kwa sasa hatujui.

Najua Mh. Lissu utanielewa kwasababu unaipenda lugha ya Kiingereza. Halafu pia Kiingereza chako ni kizuri kuliko changu, I can't reach you! (sikufikii wewe)

Kwa kuongea yeye mwenyewe Lissu bado ni tatizo, wenye uelewa wa kuzungumza kiingereza humu ndani watakwambia.
 
Kwa kuongea yeye mwenyewe Lissu bado ni tatizo, wenye uelewa wa kuzungumza kiingereza humu ndani watakwambia.
Naunga mkono hoja Lissu Kidhungu hakijui isipokuwa ana bwabwaja Ili aonekane anaflow hakuna Gramma anayotumia ibebaki kuunga vi sentensi vya kisheria ambavyo alifundishwa na wale Maprofesa anaowaita wametokea Majalalani ni maajabu kuona Tumbili anazaa Gorilla
 
Mh. Lissu naamini kuna haja ya kupitia mfumo wa elimu yetu hapa Tanzania.

Nimetumia mfano wa lugha ya Kiingereza kama kipimo kwasababu tunawasikia watu wakijaribu wakikiongea. Inawezekana yako masomo mengine pia yanayotakiwa yakuzwe lakini kwa sasa hatujui.

Najua Mh. Lissu utanielewa kwasababu unaipenda lugha ya Kiingereza. Halafu pia Kiingereza chako ni kizuri kuliko changu, I can't reach you! (sikufikii wewe)
Lugha ni muhimu sn, tuna kuwa na kiongozi mkubwa wa nchi hawezi kutunga sentensi moja ya kiingereza
 
... kama kuna eneo la kufumua haswa basi ni mfumo wa elimu wa nchi hii! Ni aibu medium of instruction ni English lakini baadhi ya PhD's yet haziwezi kunyoosha tungo moja ya Kiingereza ikaeleweka mbele ya audience.

Pia kuna tatizo la wahitimu kutojiamini; we need more Tundu Lissu's in all fields; akisimama graduate wa sheria aonekane ni mwanasheria kweli; akisimama mhandisi ni mhandisi kweli; akisimama mhasibu ni mhasibu kweli, etc.
 
Naunga mkono hoja Lissu Kidhungu hakijui isipokuwa ana bwabwaja Ili aonekane anaflow hakuna Gramma anayotumia ibebaki kuunga vi sentensi vya kisheria ambavyo alifundishwa na wale Maprofesa anaowaita wametokea Majalalani ni maajabu kuona Tumbili anazaa Gorilla
Lissu huwezi kumfananisha na maprofesa wa majalalani. Alipata Masters yake Warwick University, ni moja ya chuo kinachoheshimika huko Uingereza!
 
Kama hoja ni kiingereza basi nadhani mwanajf mwenzetu Nyani Ngabu ndio anafaa kuwa raisi
 
... kama kuna eneo la kufumua haswa basi ni mfumo wa elimu wa nchi hii! Ni aibu medium of instruction ni English lakini baadhi ya PhD's yet haziwezi kunyoosha tungo moja ya Kiingereza ikaeleweka mbele ya audience.

Pia kuna tatizo la wahitimu kutojiamini; we need more Tundu Lissu's in all fields; akisimama graduate wa sheria aonekane ni mwanasheria kweli; akisimama mhandisi ni mhandisi kweli; akisimama mhasibu ni mhasibu kweli, etc.

Ujasiri ni hulka na huanza kutengenezwa bado ukiwa mdogo, lakini ujasiri hauwezi kureplace uelewa bobezi.

Ila kama una ujasiri na una mapungufu , mapungufu yako yatakuwa wazi sana na kwa haraka, kwa kuwa utatumia ujasiri huo huo kuonyesha ulivyo kiuhalisia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom