Mh lissu apasua jipu. Polisi wahaha (video)

Kazi kweli kweli! Hili lakuzua mikutano halijakaa sawa kabisa. Swala nikutafuta mbinu mbadala ya kuhakikisha ulinzi na usalam unaimalishwa kipindi cha hiyo mikutano.
 
Polisi wetu wakipokea amri wao wanafanya bila kuangalia sheria zinasemaje au wanajua lakini wanajaribu kutekeleza amri ya boss wao. Hii ni hatari kwa demokrasia ya kweli kwenye nchi. Hivi unawezaje kumzuia mbunge asikutane na wapiga kura wake? Mimi nafikiri mbunge hapashwi kuomba ruhusa polisi ili kufanya mkutano, anapashwa kutoa taarifa tu kwamba siku fulani nina mkutano na wapiga kura wangu tarehe fulani na mahali fulani basi!!!. Na polisi wanapashwa kutoa ulinzi basi!!! sio kutoa ruhusa!!!

Tiba
 
hizi blanket statement kutoka polisi eti............"taarifa za Ki-Intelijensia"..........ni UJINGA.........hizi sio zama za Zidumu fikra za Viongozi.........
 
Hivi kikwekte pamoja na kuiba kura na kupewa urais, baado ana hofu gani na chadema?
ccm wametumia mbinu zote chafu ktk vitabu wakati wa uchaguzi, bado hawajaridhika, na sasa wanawanyima wananchi haki ya kukukutana na kuongea na wawakilishi wao! This is going too far na inaonyesha wazi yanayosemwa kwamba , ccm wao wapo kwa ajili ya masilahi ya utawala tuu, hawajali wananchi wanataka nini! It's pathetic, wanazidi kujichimbia mashimo.
Hivi hawa watu huwa hawana watu wa kuwashauri, hii nayo ni strategy ya namna gani kama si ujinga, wanadhani watazuia hiyo mikutano hadi lini? naona nia yao ni kutaka wananchi waanzishe fujo.
 
Polisi wetu wakipokea amri wao wanafanya bila kuangalia sheria zinasemaje au wanajua lakini wanajaribu kutekeleza amri ya boss wao. Hii ni hatari kwa demokrasia ya kweli kwenye nchi. Hivi unawezaje kumzuia mbunge asikutane na wapiga kura wake? Mimi nafikiri mbunge hapashwi kuomba ruhusa polisi ili kufanya mkutano, anapashwa kutoa taarifa tu kwamba siku fulani nina mkutano na wapiga kura wangu tarehe fulani na mahali fulani basi!!!. Na polisi wanapashwa kutoa ulinzi basi!!! sio kutoa ruhusa!!!

Tiba

Tiba,

neno hapo sio "wanapashwa"..........neno sahihi ni...... "wanapaswa/hapaswi/anapaswa"...........

Kupasha maji, chai, chakula, misuli, au habari..........e.g .Tiba alipashwa habari ya maendeleo wilaya ya Bukoba vijijini

Ukiwa Mfanyakazi Inakupasa kwenda Ofisini.............na unapaswa kufanya kazi
Inawapasa Polisi kutoa ulinzi......au...Polisi wanapaswa kutoa ulinzi
 
Waandishi wa habari wa Tanzania hawana adabu (nafahamu si wote).

Kwanza asante kwa kutuwekea hii video.

Sasa kama mmealikwa na kuja wenyewe na mkifika kwenye Press Conf. mnaanza makelele na fujo kama mitoto ya Chekechea jamani? Wengine misimu inalia ovyo, wengine wanatongozana sijui, WTF????

Hamna heshima kwa aliyewaalika, maboss wenu waliowatuma kuja hapo, kwa wananchi na hata kwa taaluma yenu mnayoifanya na kuingiza kipato chenu cha kila siku. Tafadhali nyie watu mkue sasa na kufahamu kipi ukifanye na kipi usikifanye katika sehemu fulani. Mkishambuliwa kuwa ni WACHAFU, basi mnakuja juu na kuanza kulalamika kuwa wanawadharau. Je nyie wenyewe mnajiheshimu?

Ona lile jinga jingine limenyowa Kibwenzi na kusoma taarifa ya habari kwenye ITV.... Kaaazi kwelikweli!!!!
 
Tiba,

neno sio "Kupashwa"..........neno sahihi ni...... "Kupaswa/Kupasa"...........

Kupasha maji, chai, chakula, misuli, au habari..........e.g .Tiba alipashwa habari ya maendeleo wilaya ya Bukoba vijijini

Ukiwa Mfanyakazi Inakupasa kwenda Ofisini.............na unapaswa kufanya kazi
Inawapasa Polisi kutoa ulinzi......au...Polisi wanapaswa kutoa ulinzi

polepole mwalimu, tangulia mwalimu
 
Hivi kikwekte pamoja na kuiba kura na kupewa urais, baado ana hofu gani na chadema?
ccm wametumia mbinu zote chafu ktk vitabu wakati wa uchaguzi, bado hawajaridhika, na sasa wanawanyima wananchi haki ya kukukutana na kuongea na wawakilishi wao! This is going too far na inaonyesha wazi yanayosemwa kwamba , ccm wao wapo kwa ajili ya masilahi ya utawala tuu, hawajali wananchi wanataka nini! It's pathetic, wanazidi kujichimbia mashimo.
Hivi hawa watu huwa hawana watu wa kuwashauri, hii nayo ni strategy ya namna gani kama si ujinga, wanadhani watazuia hiyo mikutano hadi lini? naona nia yao ni kutaka wananchi waanzishe fujo.
Mrdennis,
Mwizi kila mara anaogopa. Hawa wanaogopa kuwa CHADEMA itaendelea kupata umaarufu kwa kufanya mikutano. Wanataka raia wasahau vuguvugu lililoanzishwa na uchaguzi wa mwaka huu na bado wana ndoto kuwa wanaweza kurudisha nyuma harakati hizi. (Si umewasikia wakisema watakomboa majimbo waliyopoteza katika uchaguzi huu?)
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom