Mh. Kikwete, Tundu hatafuti umaarufu wa kisiasa!

Kwani digrii ya sheria ya OUT ina tofauti gani na ya UDSM?

Mheshimiwa Zakumi nafikiri hujailewa mada au unataka kupotosha maana makusudi.

Mtoa mada anasema Mh. J. K. kamteua jaji anaysema degree ya sheria OUT sasa. Sheria yetu inataka Lazima jaji awe na degree ya sheria anapoteuliwa. Huyu jaji ndo anaisomea hiyo degree. Hata kama angekuwa naisomea UDSM ilimradi hajaipata asingestahili kuteuliwa kuwa jaji.

Kimsingi degree ya sheria ya UDSM na OUT zinatakiwa ziwe sawa. Mtoa mada hajasema kuwa mtu akisoma OUT hastahili kuwa jaji ila kasema mtu ambaye hajapata degree hawezi kuteuliwa kuwa jaji bila kujali chuo anachosomea.
 
Hapana twende taratibu mkuu, usiwe na haraka... Nakubaliana na hoja yako. Ila pia nataka kuelewa, kama hapa ungenisaidia ungeniambia huyo judge ni nani, hapo hapo ukanisaidia kwa kuniwekea ombi langu la kupata CV yake. Hilo linatokana na basis kuwa katika jamii yetu kuna watu wanawajibika na kufanya mambo makubwa sana lakini kwa bahati mbaya ama nzuri hawajabahatika kusoma na kufuzu darasani.

Ila unakuta ni mtu ambaye anajituma saana! Anasoma sana vitabu hasa vya idara yake, anafuatilia documentaries, anafuatilia practices na vitu mbali mbali. Siwezi support hili jambo sababu tu Lissu ame point out (as much as hoja yake ni nzito) na wala sio tu sababu kachaguliwa na JK (kwa sababu ya madhaifu mengi aliyofanya wakati wa uongozi wake).

Hivyo narudi pale pale, kama utaweza naomba tumtambue huyo judge na tuapate CV kama itawezekana... Eventually mengine yatafuata kama uko sawa ama lah.

Refer post number 34 !
 
naona wakuu mnachukua muda mwingi kujibu hoja za ZAKUMI, badala ya kujadili hoja yenyewe! huyo ZAKUMI ni mgumu kuelewa, mwepesi kusahau.
 
Ninachokisema ni kuwa huyu jaji bado anasoma degree ya sheria OUT, sasa JK anabisha nini kuwa majaji hawana sifa. Sisemi kuhusu ubora wa degree. OUT wanatoa wanasheria wazuri tu
kwa maneno mengine ni kwamba alipaswa kuwa nayo degree kabla ya kuteuliwa kuwa jaji! si ndio mkuu?
 
Kwani digrii ya sheria ya OUT ina tofauti gani na ya UDSM?

Hivi watu wengine Kweli mnatumia MASABURI kufikiri!!!

Degree ya OUT na UDSM hakuna tofauti na siyo issue kwenye mada hii. Issue ni kwamba huyo JAJI hata hiyo ya OUT HAJAISOMA NA KUIMALIZA, HANA degree yoyote bado anasoma huku akiwa JAJI ambapo ni kinyume cha sheria!!!

FIKIRI kwa kutumia mifumo sahihi.
 
Ni kweli kabisa AshaDii.
Ishu ya huyu judge ni more on "technicalities" ambazo zimewekwa na sheria zenyewe.
Judge muhusika anayo 1st degree lakini siyo ya sheria. Kisha akasomea Masters ya Sheria ilhali ili uwe judge lazima uwe na degree yab kwanza ya sheria - LLB.
Usomi wa huyu jaji hauna dosari na wala siyo kihiyo hata kidogo.

Kuna jambo ambalo sijui kama wachangiaji wa hii mada wanaelewa,Jaji anayezungumziwa ni wa Mahakama ya Rufaa! Ameteuliwa akitokea Zanzibar. Kwa wenye kumbukumbu mtakumbuka mwaka jana jinsi chama cha Mawakili wa Zanzibar walipinga vikali uteuzi holela wa watu wasiokua na sifa walivyokua wanateuliwa kuwa majaji ktk Mahakama Kuu ya Zanzibar,na walipinga vikali nyongeza ya mkataba wa Jaji Mkuu wa Zanzibar aliokuwa ameongezewa na rais Shein. Hao Majaji hawakuondolewa lakini nyongeza ya mkataba wa Jaji Mkuu ilifutwa!
 
Kuna jambo ambalo sijui kama wachangiaji wa hii mada wanaelewa,Jaji anayezungumziwa ni wa Mahakama ya Rufaa! Ameteuliwa akitokea Zanzibar. Kwa wenye kumbukumbu mtakumbuka mwaka jana jinsi chama cha Mawakili wa Zanzibar walipinga vikali uteuzi holela wa watu wasiokua na sifa walivyokua wanateuliwa kuwa majaji ktk Mahakama Kuu ya Zanzibar,na walipinga vikali nyongeza ya mkataba wa Jaji Mkuu wa Zanzibar aliokuwa ameongezewa na rais Shein. Hao Majaji hawakuondolewa lakini nyongeza ya mkataba wa Jaji Mkuu ilifutwa!

Funguka zaidi mkuu.
 
Kwani digrii ya sheria ya OUT ina tofauti gani na ya UDSM?

Tatizo hapa si degree ya OUT,tatizo ni kigezo gani walichotumia kumpelekea rais jin la jaji ambaye hana taaluma ya kutosha ya sheria na mwenendo wa kuendesha mashitaka.Hilo ndilo tatizo tujaribu kuirudia kuisoma vizuri taarifa ya ushahidi wa Lissu wakati wakiwakilisha kama utetezi wake kwa kamati ya maadili ya bunge ndipo tuseme ana tafuta umaarufu.vinginevyo kama ndiyo njia iliyo tumika kujipanga kwa CCM kujibu hoja za wapinzani ndo hizo basi wataonekana CCM vuvuzela
 
Mwambie mkuu!! Aliyeteuliwa hakuwa na Degree! Alianza OUT baada ya kuteuliwa!! This is unprofessional!!

na yeye aliona uvunjaji wa katiba alioufanya Jk ndio maana akakimbilia OUT kusoma, otherwise hana haja ya kusoma maana as a "Judge" tena wa rufaa, ana kila privileges on Tanzania earth! Kumbuka na Deodorus kamala (waziri wa Afrika mashariki), baada ya watu kumsakama na degree isiyotambulika alijisajiri Mzumbe apate PhD inayokubalika! Alijua kuwa being called a doctor without a genuine degree, inamshushia hadhi mbele ya wasomi.
 
Hoja hapa ni kwamba sheria inataka anayeteuliwa kuwa jaji awe tayari na digrii ya sheria siyo ambaye hana na anayesoma open university au UDSM wakati ni jaji tayari. Yaani ni sawa na uwe unaendesha basi la abiria wakati unasomea udereva chuo cha usafirishaji pale mabibo.QUOTE=Zakumi;5044703]Kwani digrii ya sheria ya OUT ina tofauti gani na ya UDSM?[/QUOTE]
 
Mheshimiwa JK, nimekusikia ukiwahutubia majaji na kuwaombna samahani kuwa wanasiasa wanatafuta umaarufu na wala hujamchagua jaji ambaye ni jamaa yako kutoka barabarani. Let us be scientific, jibu hoja za Tundu Lissu moja baada ya nyingine. From there we will reach a just, reasoned conclusion.

1. Je yule jaji anayesoma first degree OUT, ana degree ya sheria kama sheria inavyotaka? Toa majibu na kwa hoja zingine.
2. Umepitia hukumu za hawa majaji uliowateua na kuzisoma kama zinakidhi matakwa ya kisheria ya hukumu?- umepima lugha wanayotumia kama ni kiingereza cha kisheria?
3. etc, etc,etc, etc,............................................................................

MAJAJI: JIHUKUMUNI WENYEWE:
1. SOMA HUKUMU ZA MAJAJI WA KIKWETE MTAUONA UKWELI WA LISU
2. MAADILI YA WENZENU YAJADILI MTAUONA UKWELI WA LISU

Kama alivyosema jaji Mihayo, afadhali kuwaachia watuhumiwa 10 walioua kuliko kumnyonga mtu mmoja ambaye hakuua! The opposite is the case with JK appointed judges
Unajua watawala wengi barani Afrika hawapendi kukubali makosa na kuomba msamaha. Kikwete anaelewa wakati anaingia Ikulu,alikuta majina ya majaji wapya mezani kwake yakisubiri atangaze uteuzi rasmi. Majina yalikatwa na kwa mshangao wakatangazwa watu wengine ambao wengi walikua karibu na mtandao uliomwingiza madarakani! Bila kujali itikadi zetu na tofauti zetu,ni ukweli kwamba uteuzi wa majaji kama zilivyo nafasi nyingine za uongozi ktk nchi yetu kuna makosa mengi yanafanyika.
 
tumia kidogo busara au kaa kimya.Onyesha nawe ni great thinker na si shabiki.
haileti mantiki kusema kama huna degree usiwe hakimu wa mahakama yeyote,kwa akili yako mahakama ya mwanzo hakimu awe na degree wakati hata mawakili hawaruhusiwi.
hoja dhaifu hata haijadiliki hapa labda primary school na kukaa kimya kwa kitu usichokijua si dalili ya ujinga bali wingi wa hekima

You are the great thinker. I am not and if my post doesn't meet your criteria of greatnest, you might as well ignore it.
 
Mheshimiwa Zakumi nafikiri hujailewa mada au unataka kupotosha maana makusudi.

Mtoa mada anasema Mh. J. K. kamteua jaji anaysema degree ya sheria OUT sasa. Sheria yetu inataka Lazima jaji awe na degree ya sheria anapoteuliwa. Huyu jaji ndo anaisomea hiyo degree. Hata kama angekuwa naisomea UDSM ilimradi hajaipata asingestahili kuteuliwa kuwa jaji.

Kimsingi degree ya sheria ya UDSM na OUT zinatakiwa ziwe sawa. Mtoa mada hajasema kuwa mtu akisoma OUT hastahili kuwa jaji ila kasema mtu ambaye hajapata degree hawezi kuteuliwa kuwa jaji bila kujali chuo anachosomea.


Kuna mtu kaonyesha vipengere vya katiba hiyo hiyo vinavyosema kuwa uzoefu wa kazi unaweza kutumika kama substitute ya shule.
 
Sishangai sana maana nchi hii inaongozwa na kakundi ka watu tena hata wakistaafu wanarudishwa madarakani km wakuu wa mikoa, wilaya au kamati na bodi mbali mbali, waliobakia wote hata wawe na uwezo vipi hawafai kuongoza nchi hii.
 
Hoja hapa ni kwamba sheria inataka anayeteuliwa kuwa jaji awe tayari na digrii ya sheria siyo ambaye hana na anayesoma open university au UDSM wakati ni jaji tayari. Yaani ni sawa na uwe unaendesha basi la abiria wakati unasomea udereva chuo cha usafirishaji pale mabibo.QUOTE=Zakumi;5044703]Kwani digrii ya sheria ya OUT ina tofauti gani na ya UDSM?
[/QUOTE]

What's your problem? Why do you repeat what others have already told me? It's time to move on.
 
Back
Top Bottom