Mh.Kikwete (rais) anashauriwa nani kuijenga Tanzania?

mchambakwao

Member
Dec 9, 2011
77
14
Habari wana JF!
Inatia uchungu sana kuona na kusoma humu jamvini eti rais wetu anasema kujizulu kwa mawaziri kwa ubadhirifu ni upepo tu,utapita.Hana uchungu na nchi hii?
Aliapa kutetea katiba ya JMT na sio wezi na wahujumu uchumi.
Rais anashauriwa na nai ktk kuijenga nchi yetu kama hataki kusikiliza ushauri na mawazo ya wabunge? Kwa mantiki hii inaonyesha kuwa hata wale waliojiuzulu mwaka 2008 inaonyesha yeye ndo kikwazo na sio wale waliojiuzulu.
Je tutafika kwa mchwa huu uliotamalaki serikalini na bosi wao kuwatetea? Anaacha historia gani kwa vizazi vijavyo?
Nawaomba mnaomsaidia rais tafadhali mwambieni huku mitaani na vijijini hali ni tia maji tia maji,njaa balaa na mfumuko wa bei hauongeleki na miradi mbalimbali imesimama,kazi za serikali haziendi kabisa.
 
Back
Top Bottom