LordJustice1
JF-Expert Member
- Jan 19, 2011
- 2,263
- 530
Juzi juzi Mheshimiwa Kikwete alifanya Semina Elekezi kwa Mawaziri wake na katika Semina hiyo alidai kwamba kila Wizara ina Msemaji wa wake na ni vizuri wawe wanajibu kila hoja inayotolewa dhidi yake.
Alienda mbali kwa kusema kwamba uwongo ukiachwa kwa muda mrefu na kurudiwa mara kwa mara bila kujibiwa utageuzwa kuwa ukweli. Alidai pia kwamba kwa muda wa miaka mitano iliyopita Serikali ilikuwa haijibu hoja za Wapinzani na wananchi wamekuwa wakiwaamini kila wasemayo!
Mpaka hapo sina tatizo na Mheshimiwa Kikwete!
Hata hivyo, kama Kikwete anataka hoja zijibiwe aanze na hoja zilizoanzia wakati alipoingia madarakani mwaka 2005 na sio kujibu hoja za sasa akidhani kwamba hoja zilizopita tumezisahau! Kwa hiyo Mh Kikwete akitaka tumwelewe afanye yafuatayo:
1. Akanushe kuhusu yeye kuitwa fisadi pale ilipotajwa List of Shame!
2. Atoe maelezo kuhusu aliko Dr Balali.
3. Aeleze juu ya wizi wa Meremeta na aache visingizio kwamba eti kuna SIRI ZA JESHI!
4. Aeleze juu ya wizi wa fedha za EPA ambazo ndizo zilizomwingiza Ikulu!
5. Aombe radhi Watanzania kwa kupitisha kupitia kikao cha Baraza la Mawaziri Kampuni hewa ya Richmond ili kuja kukwapua fedha zetu!
6. Aeleze ni kwa nini alipokuwa Waziri wa Nishati na Madini alisaini mikataba tata ya IPTL na mingineyo inayotafuna uchumi wa nchi yetu mpaka sasa!
7. Aeleze juu ya wizi wa kutupwa kupitia Makampuni ya Deep Green Finance, TanGold, Mwananchi Gold, Kagoda, nk ambao mpaka sasa hakuna majibu ya kueleweka!
8. Aeleze jinsi Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira ulivyonunuliwa kwa fedha za maandazi (70m/-) na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa!
9. Aeleze jinsi alivyochakachua kura halali za Dr Willibrod Slaa na kuingia Ikulu kibabe kupitia Tume ISIYO HURU ya Uchaguzi!
10. Aeleze zilipo TSh 74bn/- ambazo zilirudishwa na wezi wa EPA ambao hakuwataja hata majina baada ya kutolewa toka Benki ya TIB!
11. n.k.
Kikwete akijibu hoja hizo kwa ukamilifu atakuwa amefanya la maana na kama ni muungwana anatakiwa ajiuzulu ili awapishe watu wenye uchungu na nchi hii waingie Ikulu!
Alienda mbali kwa kusema kwamba uwongo ukiachwa kwa muda mrefu na kurudiwa mara kwa mara bila kujibiwa utageuzwa kuwa ukweli. Alidai pia kwamba kwa muda wa miaka mitano iliyopita Serikali ilikuwa haijibu hoja za Wapinzani na wananchi wamekuwa wakiwaamini kila wasemayo!
Mpaka hapo sina tatizo na Mheshimiwa Kikwete!
Hata hivyo, kama Kikwete anataka hoja zijibiwe aanze na hoja zilizoanzia wakati alipoingia madarakani mwaka 2005 na sio kujibu hoja za sasa akidhani kwamba hoja zilizopita tumezisahau! Kwa hiyo Mh Kikwete akitaka tumwelewe afanye yafuatayo:
1. Akanushe kuhusu yeye kuitwa fisadi pale ilipotajwa List of Shame!
2. Atoe maelezo kuhusu aliko Dr Balali.
3. Aeleze juu ya wizi wa Meremeta na aache visingizio kwamba eti kuna SIRI ZA JESHI!
4. Aeleze juu ya wizi wa fedha za EPA ambazo ndizo zilizomwingiza Ikulu!
5. Aombe radhi Watanzania kwa kupitisha kupitia kikao cha Baraza la Mawaziri Kampuni hewa ya Richmond ili kuja kukwapua fedha zetu!
6. Aeleze ni kwa nini alipokuwa Waziri wa Nishati na Madini alisaini mikataba tata ya IPTL na mingineyo inayotafuna uchumi wa nchi yetu mpaka sasa!
7. Aeleze juu ya wizi wa kutupwa kupitia Makampuni ya Deep Green Finance, TanGold, Mwananchi Gold, Kagoda, nk ambao mpaka sasa hakuna majibu ya kueleweka!
8. Aeleze jinsi Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira ulivyonunuliwa kwa fedha za maandazi (70m/-) na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa!
9. Aeleze jinsi alivyochakachua kura halali za Dr Willibrod Slaa na kuingia Ikulu kibabe kupitia Tume ISIYO HURU ya Uchaguzi!
10. Aeleze zilipo TSh 74bn/- ambazo zilirudishwa na wezi wa EPA ambao hakuwataja hata majina baada ya kutolewa toka Benki ya TIB!
11. n.k.
Kikwete akijibu hoja hizo kwa ukamilifu atakuwa amefanya la maana na kama ni muungwana anatakiwa ajiuzulu ili awapishe watu wenye uchungu na nchi hii waingie Ikulu!