naninibaraka
JF-Expert Member
- Oct 13, 2011
- 910
- 668
Mh Rais nchi yetu inapita kwenye kipindi kigumu cha hali mbaya ya uchumi,maisha yamekua magumu,kibaya zaid serikali unayoiongoza haijatoa tamko lolote,wachina wajenz wa barabara wametishia kusimamisha kazi pesa hakuna.
Pesa zinazokusanywa kwa kiasi kikubwa zinatumika kuendesha serikali ikiwa ni pamoja na safari zako kila kukicha nje ya nchi ambazo hazina tija,zaid ya maslahi binafsi,rais makini hutumia muda mwingi kutatua kero za wananchi wake, kusafir nje kwa raha gani wananchi walizonazo?
Rais wa nchi kukaa kimya wakati uchumi unadorora si jambo jema hata kidogo,hakuna juhudi za dhati za serikali kutatua matatizo yanayoikabili nchi kwa sasa..
Wananchi tumechoka na maneno kila kukicha mara 'serikali yenu ni sikivu,mara serikali inafanya upembuz yakinifu' hizi zote ni blabla! Fanyeni maamuz magumu!
Pesa zinazokusanywa kwa kiasi kikubwa zinatumika kuendesha serikali ikiwa ni pamoja na safari zako kila kukicha nje ya nchi ambazo hazina tija,zaid ya maslahi binafsi,rais makini hutumia muda mwingi kutatua kero za wananchi wake, kusafir nje kwa raha gani wananchi walizonazo?
Rais wa nchi kukaa kimya wakati uchumi unadorora si jambo jema hata kidogo,hakuna juhudi za dhati za serikali kutatua matatizo yanayoikabili nchi kwa sasa..
Wananchi tumechoka na maneno kila kukicha mara 'serikali yenu ni sikivu,mara serikali inafanya upembuz yakinifu' hizi zote ni blabla! Fanyeni maamuz magumu!