Mh. John Momose Cheyo unakumbuka?

Raia Fulani

JF-Expert Member
Mar 12, 2009
10,770
2,544
Nakumbuka sana mwaka 2005 jk alipohutubia bunge kwa mara ya kwanza kwa hotuba yake ya kutoa denda. Saa zima na ushee jk alituimbisha, huku tabasam likimtanda usoni. Alianza kwa kusema kuwa safari hii kura zimetosha. Mwanzo mwisho wabunge walitabasam. Sie tulijawa matumaini. Mwisho wa siku wabunge wakihojiwa, Cheyo alisema tena kwa bashasha, "baada ya miaka 10 tumepata rais anayeongea na watu." labda hakukosea. Jk anaongea kweli. Mh. Bado una imani ile? Bado tuna imani ile? Naomba sana kama kuna mdau anayo ile speech atubandikie hapa tuitafakari. Maisha bora kwa kila mtanzania
 
Hana lolote huyo JK,kazi ya msanii ni kuchekesha,Tanzania ndugu zangu hatuwezi kukombolewa na CCM.Huyo Cheyo na chama chake ni CCM B.
 
Nakushauri uachane na John Momose Cheyo, huyu siye yule wa 2005; baada ya kuhoja joto la jiwe ambapo nyumba yake ilipigwa mnada, ameamuakujihudumia yeye badala ya kuwahudumia watanzania. Matokeo yake chama chake hivi sasa tayari kimeishapoteza sifa za kuwa chama cha siasa. Kinachozuia chama hicho kufutwa ni kutokana na kulindwa kwake na utawala uliopo.
 
Nakumbuka sana mwaka 2005 jk alipohutubia bunge kwa mara ya kwanza kwa hotuba yake ya kutoa denda. Saa zima na ushee jk alituimbisha, huku tabasam likimtanda usoni. Alianza kwa kusema kuwa safari hii kura zimetosha. Mwanzo mwisho wabunge walitabasam. Sie tulijawa matumaini. Mwisho wa siku wabunge wakihojiwa, Cheyo alisema tena kwa bashasha, "baada ya miaka 10 tumepata rais anayeongea na watu." labda hakukosea. Jk anaongea kweli. Mh. Bado una imani ile? Bado tuna imani ile? Naomba sana kama kuna mdau anayo ile speech atubandikie hapa tuitafakari. Maisha bora kwa kila mtanzania

Siyo Mzee Cheyo peke yake, humu humu JF wakati inaanza 2006 ilikuwa ukimsema JK unatupiwa mawe, hata wakongwe kama Mzee Mwkjj walikuwa wanatumia kauli eti 'washauri wa raisi hawakumshauri vizuri' na leo miaka 6 baadae hatujaona mabadiliko.
Ama kweli ukipenda chongo huita kengeza!
 
Siyo Mzee Cheyo peke yake, humu humu JF wakati inaanza 2006 ilikuwa ukimsema JK unatupiwa mawe, hata wakongwe kama Mzee Mwkjj walikuwa wanatumia kauli eti 'washauri wa raisi hawakumshauri vizuri' na leo miaka 6 baadae hatujaona mabadiliko.
Ama kweli ukipenda chongo huita kengeza!

ni wengi sana tuliingizwa kingi kumbe tumeandaliwa mazingira ya kuliwa. Hata mi nakumbuka nilimtetea sana eti tumpe muda. I wish tungepata ile hotuba yake ya kwanza kabisa bungeni
 
Anyone who has never made a mistake has never tried anything new. Kwa hiyo mwanzoni mlikuwa na matumaini, haikuwa kosa. Lakini kosa ni kutumaini tena safari hii wakati hali halisi ni tofauti na maneno yasemwayo sokoni i.e. .. reality rarely matches the marketing.
 
Nakumbuka Mzee aliyekua anatoka MKAPA alituonya kwamba "Najua ntaonekana sifai ila ipo siku Tanzania Itanikumbuka" Personaly sikujuaga alimaanisha nini ila kwa sasa najua alichomaanisha, na inaonekana alijua nini kitakachotokea.

Watu walipoambiwa "Nguvu mpya na Kasi mpya" Wakajua ni Mbio za maendeleo kumbeee......Teh!
 
Anyone who has never made a mistake has never tried anything new. Kwa hiyo mwanzoni mlikuwa na matumaini, haikuwa kosa. Lakini kosa ni kutumaini tena safari hii wakati hali halisi ni tofauti na maneno yasemwayo sokoni i.e. .. reality rarely matches the marketing.
Siamini kama kuna mtu kwa dhati ya moyo wake anamuamini tena kwa sasa. Kama wapo basi wana aidha maslahi binafsi ama ni wapumbavu (maana ujinga si tusi). Mpumbavu ni mtu aliyekuwa katika kiwango cha ujinga akashindwa kuondokana na ujinga pamoja na kueleweshwa. Mmojawapo Cheyo. Huyu ana maslahi binafsi
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom