Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,770
- 2,544
Nakumbuka sana mwaka 2005 jk alipohutubia bunge kwa mara ya kwanza kwa hotuba yake ya kutoa denda. Saa zima na ushee jk alituimbisha, huku tabasam likimtanda usoni. Alianza kwa kusema kuwa safari hii kura zimetosha. Mwanzo mwisho wabunge walitabasam. Sie tulijawa matumaini. Mwisho wa siku wabunge wakihojiwa, Cheyo alisema tena kwa bashasha, "baada ya miaka 10 tumepata rais anayeongea na watu." labda hakukosea. Jk anaongea kweli. Mh. Bado una imani ile? Bado tuna imani ile? Naomba sana kama kuna mdau anayo ile speech atubandikie hapa tuitafakari. Maisha bora kwa kila mtanzania