Mh JK ukimaliza ziara zako,naomba uanze ziara za kukagua miradi isiyo ya maendeleo!

Calnde

JF-Expert Member
Oct 7, 2008
1,373
277
Naamini muda si mrefu utakuwa umemaliza mikoa yote na hivyo utakuwa umebakisha nchi za nje tuu unless uanze za kila wilaya! Sasa nakuomba yafuatayo! Uanze kukagua miradi isiyo ya maendeleo.
1.Uanze kukagua ujenzi wa BOT kisha ukague akaunti hadi akaunti kwa mwaka hadi mwaka!
2.Upite kila wizara kuona mapato na matumizi yao.Usisahau kukagua zile wizara ambazo zimepangisha kwa gharama kubwa ambayo ndani ya mwaka mmojawanaweza wakajenga majengo yao binafsi.
3.Usiache kupita vituo vya polisi ambavyo kila siku hawana karatasi lakini pembeni kidpgo kuna stationery ambapo wanaohitaji huduma huagizwa kununua karatasi hapo.
4.Usiache kukagua wizara ya elimu ambapo mradi wa kuvujisha mitihani na kutoa vyeti feki bila wahusika kuwajibishwa unaendelea.Pita mpaka vyuoni uone digrii feki zinzvyouzwa.
5.Ukiwa Dar usiache kupiga jicho nje ya gari lako uone mighorofa inavyoporomoshwa mita mbili toka barabani kama vile hatuna mawazo ya upanuzi wa barabara.
6.usiache kukagaua magari ya serikali yanavyobeba majani toka pugu na chanika as if kuna maradi wakufuga ng'ombe wa maziwa.Magari hayo hayo ndio yanabeba viti na maua yakupambia harusi.
7.Morogoro umejionea mwenyewe jengo la mkuu wa wilaya limegharimu over bilion Tsh,pita kila wilaya uone miradi ya namna hii ilivyo mingi.Nakuomba usiache kupita ziko sehemu nyingi natamani uzitembelee.....

Ukimaliza kukagua utakuwa na mambo mawili yakufanya 1.Uwakusanye wasaidizi wako pale ngurdoto kuwapa semina mpya elekezi au 2.Umrudishe Lowassa Madarakani mfanye fataki ya kujenga mahabusu na jela kila kata kwa msaada wa nguvu za wananchi. Usipofanya hivi 2010 itakukuta umetumia muda mwingi ukikusanya mawe na kumbe umepoteza dhahabu nyingi!
 
sawa ila asitoe taarifa akienda. akifika mfano kituo cha polisi (hasa matrafiki) wakaguliwe na wakuu wao-wataona mabulungutu ya hongo yanavyofichwa kwenye soksi.
 
sawa ila asitoe taarifa akienda. akifika mfano kituo cha polisi (hasa matrafiki) wakaguliwe na wakuu wao-wataona mabulungutu ya hongo yanavyofichwa kwenye soksi.


Bado nasisitiza afanye ziara akague miradi mingi isiyo na maendeleo? Hapo ataona umuhimu wa kuwa na mahabusu kila kata
 
Ukimaliza kukagua utakuwa na mambo mawili yakufanya 1.Uwakusanye wasaidizi wako pale ngurdoto kuwapa semina mpya elekezi au 2.Umrudishe Lowassa Madarakani mfanye fataki ya kujenga mahabusu na jela kila kata kwa msaada wa nguvu za wananchi. Usipofanya hivi 2010 itakukuta umetumia muda mwingi ukikusanya mawe na kumbe umepoteza dhahabu nyingi!

Hautahitaji feedback akimaliza hiyo kazi uliyompa?
 
Akishamaliza ziara zote hizo, mshauri pia aende karibu na Lugoba mbele kidogo tu ya Chalinze-mzee njia kuu ya lami ielekeayo Segera kijiji cha Mboga (kama sikosei, nikikosea mnisahihishe wakuu) atupe jicho upande wa kushoto aone jumba kubwa la kifahari linalojengwa bila kubandikwa kibao cha contract ya ujenzi kama sheria inavyotaka. Akishaona atuambie pia jumba hilo ni la nani.
 
Naamini muda si mrefu utakuwa umemaliza mikoa yote na hivyo utakuwa umebakisha nchi za nje tuu unless uanze za kila wilaya! Sasa nakuomba yafuatayo! Uanze kukagua miradi isiyo ya maendeleo.
1.Uanze kukagua ujenzi wa BOT kisha ukague akaunti hadi akaunti kwa mwaka hadi mwaka!
2.Upite kila wizara kuona mapato na matumizi yao.Usisahau kukagua zile wizara ambazo zimepangisha kwa gharama kubwa ambayo ndani ya mwaka mmojawanaweza wakajenga majengo yao binafsi.
3.Usiache kupita vituo vya polisi ambavyo kila siku hawana karatasi lakini pembeni kidpgo kuna stationery ambapo wanaohitaji huduma huagizwa kununua karatasi hapo.
4.Usiache kukagua wizara ya elimu ambapo mradi wa kuvujisha mitihani na kutoa vyeti feki bila wahusika kuwajibishwa unaendelea.Pita mpaka vyuoni uone digrii feki zinzvyouzwa.
5.Ukiwa Dar usiache kupiga jicho nje ya gari lako uone mighorofa inavyoporomoshwa mita mbili toka barabani kama vile hatuna mawazo ya upanuzi wa barabara.
6.usiache kukagaua magari ya serikali yanavyobeba majani toka pugu na chanika as if kuna maradi wakufuga ng'ombe wa maziwa.Magari hayo hayo ndio yanabeba viti na maua yakupambia harusi.
7.Morogoro umejionea mwenyewe jengo la mkuu wa wilaya limegharimu over bilion Tsh,pita kila wilaya uone miradi ya namna hii ilivyo mingi.Nakuomba usiache kupita ziko sehemu nyingi natamani uzitembelee.....

Ukimaliza kukagua utakuwa na mambo mawili yakufanya 1.Uwakusanye wasaidizi wako pale ngurdoto kuwapa semina mpya elekezi au 2.Umrudishe Lowassa Madarakani mfanye fataki ya kujenga mahabusu na jela kila kata kwa msaada wa nguvu za wananchi. Usipofanya hivi 2010 itakukuta umetumia muda mwingi ukikusanya mawe na kumbe umepoteza dhahabu nyingi!


Hao ambao wanashikilia nafasi za sehemu hizo wafanye nini ? yaani kuwa rais wa Tanzania ni utumwa.
 
Back
Top Bottom