Endeleaaa
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 1,485
- 738
Leo nimeshangazwa sana kudaiwa ada ya kupaki gari katika fukwe za kokobeach maeneo ya oysterbay. Mkusanya ada huyo ni mfanyakazi wa kampuni ya ulinzi ya oysterbay guard. Baada ya kumhoji sana uhalali wa kulipa ada hiyo aliniacha akaondoka na hivyo nikapaki bila kulipa hadi nikaondoka.
Kilichonishangaza watu wote wanaokuja na magari yao kupunga upepo pale beach wakidaiwa hiyo ada wanalipa tu bila hata kuhoji ipasavyo uhalali wa ada hiyo. Ada yenyewe ni shs 1000 kwa saa.
Kulingana na mlinzi huyo hiyo ada ni makusanyo ya serikali ya mtaa oysterbay. nilimuomba namba ya BOSS wake niongee nae kabla sijalipoa hiyo ada lakini aligoma na kuamua kuondoka na kuniacha niendelee na starehe zangu hapo beach.
Mheshimiwa Mdee wewe kama Mbunge wetu eneo hilo tuambie kwanini tunatozwa kodi maeneo ya kujipumzisha kama hayo? Na hiyo kodi ni kulingana na kifungu gani cha sheria? Kwanini halijawekwa bango la serikali linalotoa tamko kuwa kokobichi linalipiwa ada za kuengesha magari? kwanini tudaiwe ada na askari? toka lini askari wakawa wakusanya kodi?
Nijuavyo mimi kokobichi ni eneo la wazi la watanzania kupumzika bure. tungekuwa na hela sana tungeenda commercial beaches mbona ziko nyingi tu.
Tafadhali Mheshimiwa Mdee liangalie hili isije kuwa ni aina nyingine ya ufisadi.
Asante
Kilichonishangaza watu wote wanaokuja na magari yao kupunga upepo pale beach wakidaiwa hiyo ada wanalipa tu bila hata kuhoji ipasavyo uhalali wa ada hiyo. Ada yenyewe ni shs 1000 kwa saa.
Kulingana na mlinzi huyo hiyo ada ni makusanyo ya serikali ya mtaa oysterbay. nilimuomba namba ya BOSS wake niongee nae kabla sijalipoa hiyo ada lakini aligoma na kuamua kuondoka na kuniacha niendelee na starehe zangu hapo beach.
Mheshimiwa Mdee wewe kama Mbunge wetu eneo hilo tuambie kwanini tunatozwa kodi maeneo ya kujipumzisha kama hayo? Na hiyo kodi ni kulingana na kifungu gani cha sheria? Kwanini halijawekwa bango la serikali linalotoa tamko kuwa kokobichi linalipiwa ada za kuengesha magari? kwanini tudaiwe ada na askari? toka lini askari wakawa wakusanya kodi?
Nijuavyo mimi kokobichi ni eneo la wazi la watanzania kupumzika bure. tungekuwa na hela sana tungeenda commercial beaches mbona ziko nyingi tu.
Tafadhali Mheshimiwa Mdee liangalie hili isije kuwa ni aina nyingine ya ufisadi.
Asante