Jacobus
JF-Expert Member
- Mar 29, 2011
- 4,681
- 1,698
Juma Mgunda, sasa hivi ni kocha wa klabu ya Simba. Tokea ajiunge na klabu hii pana watu wanajitahidi kumpamba kuwa ni kocha mzawa mzuri mno, wakitaka kututoa katika kumbukumbu kuwa katokea timu ya Coastal Union iliyopo Ligi Kuu kama timu ya Simba.
Mimi, naamini kuwa kufanya vizuri kwa timu ya Simba sasa hivi ni kwa juhudi za wachezaji, klabu iliyowasajiri na si usajiri alioufanya kocha Mgunda. Hivyo namtahadharisha kocha huyo kujiandaa kisaikolojia kuwa wanaomsifia sasa hivi kwa timu kufanya vizuri kimichezo ndiyo hao hao watakao mzomea kesho pindi timu ikianza kufanya vibaya.
Sasa hivi kelele za kumtaka kocha Matola wala hazisikiki na ndiyo muda mzuri kwake kuondoka hapo.
Mimi, naamini kuwa kufanya vizuri kwa timu ya Simba sasa hivi ni kwa juhudi za wachezaji, klabu iliyowasajiri na si usajiri alioufanya kocha Mgunda. Hivyo namtahadharisha kocha huyo kujiandaa kisaikolojia kuwa wanaomsifia sasa hivi kwa timu kufanya vizuri kimichezo ndiyo hao hao watakao mzomea kesho pindi timu ikianza kufanya vibaya.
Sasa hivi kelele za kumtaka kocha Matola wala hazisikiki na ndiyo muda mzuri kwake kuondoka hapo.