Mgonjwa wa akili aua wenzake wodini Muhimbili, ajeruhi watano

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
Date::8/12/2008
Mgonjwa wa akili aua wenzake wodini Muhimbili, ajeruhi watano
Na Waandishi Wetu
Mwananchi

IMANI ya watu wengi kwamba hospitalini ni mahali pa kukimbilia kuokoa maisha kwa mgonjwa, imeshindikana kuthibitika baada ya mgonjwa wa akili kuwashambulia wenzake saba wodini na kuua wawili kati yao.

Tukio hilo la kuhuzunisha na la kwanza kutokea katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), lilitokea usiku wa kuamkia juzi baada ya mgonjwa wa akili, David Denge (21) aliyelazwa katika wodi ya wagonjwa kuwashambulia wenzake wakiwa wamelala usingizini.

Habari ambazo zimethibitishwa na Mkurugenzi Mkuu wa MNH, Profesa Leonard Lema pamoja na polisi, Denge anadaiwa kucharuka usiku na kuwashambulia wenzake kwa kuwaponda kichwani kwa chuma cha kuwekea maji ya dripu.

Profesa Lema alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa 1:30 usiku katika wodi ya wagonjwa wa akili.

Alisema Denge aliyekuwa katika hospitali hiyo tangu Julai 28 mwaka huu, alikuwa katika wodi ya wagonjwa wa akili waliopitiliza walioko chini ya uangalizi maalum.

Kwa mujibu wa Profesa Lema, mgonjwa huyo aliamka ghafla kutoka usingizini na kuchukua chuma wanachowekea wagonjwa maji ya dripu na kuwaponda wenzake.

"Polisi walijulishwa tukio hilo jana (juzi), walifika Muhimbili na wanaendelea na uchunguzi wao. Pia uongozi wa hospitali umewasiliana na viongozi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa hatua zaidi," alisema Profesa Lema.

Alisema wagonjwa wawili walifariki dunia kwa kuumia vibaya kichwani huku wengine wanne wakipelekwa chumba cha upasuaji na hali ya wagonjwa wawili kati ya hao wanne sio nzuri.

Profesa Lema alisema uchunguzi wa tukio hilo unaendelea kubaini sababu za tukio hilo na kujua endapo kulikuwa na uzembe kwa upande wa wauguzi katika kuwaangalia wagonjwa.

''Kinachoonekana katika suala hili ni kwamba mgonjwa huyo hakupewa dawa mapema kwani dawa wanazotumia zinawafanya wakose nguvu za kufanya fujo,'' chanzo cha habari kilidokeza.

Habari zingine zinasema hospitali ya Muhimbili pia ina tatizo la dawa za wagonjwa wa akili na upungufu wa madaktari na wauguzi.

Katika hatua nyingine, Jeshi la polisi nchini limesema kuwa lina wasiwasi kuwa muuaji wa wagojwa wawili katika wodi ya vichaa Muhimbili alizinduka mapema na kuwaua wenzake wakati wakiwa usingizini.

Wagonjwa wa aina hiyo, huchomwa sindano za usingizi ili walale na polisi ilisema kuwa huenda muuaji alizinduka mapema baada ya dawa walizochomwa kuisha nguvu na kufanya mauaji hayo.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Aibula Tanda, alitaja waliouawa na Denge ambaye ni mchoma mkaa wa Kongowe ni Paul Maganga (30) na Abdallah Abeid (20).

Tanda alisema kwa mujibu wa muuguzi wa daraja la pili wa wodi hiyo, Kokumula Severine (26), muuaji huyo alitumia chuma kinachotumika kama ‘stedi dripu’ na kuwashambulia wagonjwa wenzake wakiwa wamelala.

“Kwa kuwa wagonjwa hao huchomwa sindano yenye dawa ili kupunguza makali yao, tunasadiki kuwa dawa aliyochomwa muuaji iliisha nguvu mapema na ndipo alipoamka na kuwashambulia wenzake na wawili kati ya tisa wamefariki na wengine ni majeruhi,” alifafanua Tanda.

Alisema tukio hilo ni la kusikitisha kwa kuwa wagonjwa hao, walikuwa wamelala wakati muuaji akiwashambulia.

Kamanda Tanda aliwataja wagonjwa wengine, Hamis Mohammed (41), Athuman Abdallah (23), Peter Joseph (Milanzi) na Maurice Oyala (20) ambao walijeruhiwa vibaya maeneo ya kichwani na kulazwa katika hospitali hiyo na kwamba hali zao si nzuri.

“Kwa mujibu wa taarifa kutoka Muhimbili, mgonjwa Jumbe Said amepata majeraha ya kawaida na anaendelea vizuri wakati mgonjwa Bela Mosha hakushambuliwa kabisa,” alisema Kamanda Tanda.

Aliongeza kuwa muuaji amekamatwa na polisi na anatarajiwa kufikishwa mahakamani ili kujibu tuhuma zinazomkabili.

''…Kwa sheria lazima afikishwe mahakamani na wataalamu watampima ili kuchunguza mgonjwa huyo wa akili alipata wapi nguvu za kufanya matukio hayo wakati wenzake walikuwa wamelala,'' alisema Tanda.

Hili ni tukio la kwanza kutokea katika hospitali hiyo tangu kuanzishwa kwake mwaka 1956, hivyo kutoa changamoto kwa uongozi kuweka mikakati ya kukabiliana na tatizo hilo katika siku za usoni.

Habari hii imeandaliwa na Kuruthum Ahmed, Jackson Odoyo na Festo Polea
 
Aisee hii habari mbona inatisha? Ina maana kama angefanikiwa huyu mgonjwa kutoroka angeweza hata kuingia wodini kwa watoto au akina mama na kuwaponda vichwa, au sio? Duh! It send chills down my spine!
 
Huu ni uzembe au tuseme ndio mgomo baridi wa madaktari wetu unaosababishwa na serikali kupitia wizara husika.
 
Yaani inasikitisha but why vitu vya hatari viwekwe katika chumba hicho cha wagonjwa wa akili? Hawa waangalizi hawajui kuwa lolote laweza kutokea kichaa akicharuka? au ndo huo mgomo baridi?... Mimi hata sielewi nini maana ya kuwa katika wodi ya UANGALIZI MAALUMU wakati vifaa hatari vipo humo?... nani mwenye kichaa kati ya huyo mgonjwa na waangalizi.!!
 
Yaani inasikitisha but why vitu vya hatari viwekwe katika chumba hicho cha wagonjwa wa akili? Hawa waangalizi hawajui kuwa lolote laweza kutokea kichaa akicharuka? au ndo huo mgomo baridi?... Mimi hata sielewi nini maana ya kuwa katika wodi ya UANGALIZI MAALUMU wakati vifaa hatari vipo humo?... nani mwenye kichaa kati ya huyo mgonjwa na waangalizi.!!

Kwanza hawa manesi walikuwa wapi?Cha ajabu Prof Lema na Yule Mkuu wa Polisi wanasema yule Kichaa atafunguliwa mashtaka nadhani hata mwanafunzi aliyegraduate jana law school anaweza kumtetea huyo kichaa maana Insanity is a defence weapon already!

Refer to the Penal Code Cap 16 R.E 2002 Section 13 whereby a person will not be liable for an act if his mind is affected by disease at the time of commiting the offence that he was incapable of undrstanding the nature of the crime,incapable of appreciating that he ought not to do the act or omission and does not have control of the act or omission.

I thought Muhimbili wana strong room kwa ajili ya acute patients?Wakufungulia mashtaka hapo ni muuguzi msimamizi na uongozi they will be vicarious liable!Maana this was a negligence committed in the course of the emplyment of the nurse in charge!Sasa hawa akina Lema na wenzake wasishift blame to other people eboo..........!
 
Kwanza hawa manesi walikuwa wapi?Cha ajabu Prof Lema na Yule Mkuu wa Polisi wanasema yule Kichaa atafunguliwa mashtaka nadhani hata mwanafunzi aliyegraduate jana law school anaweza kumtetea huyo kichaa maana Insanity is a defence weapon already!

Refer to the Penal Code Cap 16 R.E 2002 Section 13 whereby a person will not be liable for an act if his mind is affected by disease at the time of commiting the offence that he was incapable of undrstanding the nature of the crime,incapable of appreciating that he ought not to do the act or omission and does not have control of the act or omission.

I thought Muhimbili wana strong room kwa ajili ya acute patients?Wakufungulia mashtaka hapo ni muuguzi msimamizi na uongozi they will be vicarious liable!Maana this was a negligence committed in the course of the emplyment of the nurse in charge!Sasa hawa akina Lema na wenzake wasishift blame to other people eboo..........!
I couldnt say more ......... You have said it all.

Eti mgonjwa atafunguliwa mashtaka yaaani hawa........... wakubwa!!
 
yaani nimesikitika sana chumba cha ungalizi maalum huyo muangalizi alikuwa wapi? au nae alikimbia nini??? not serious !!!!!!!!!!
 
The M'Naghten Rule provides as follows: "Every man is to be presumed to be sane, and ... that to establish a defense on the ground of insanity, it must be clearly proved that, at the time of the committing of the act, the party accused was laboring under such a defect of reason, from disease of mind, and not to know the nature and quality of the act he was doing; or if he did know it, that he did not know he was doing what was wrong.

Upon being taken to jury accused of murder they have to prove his mens rea (evil mind) and actus reus (evil act) but in this case there was an evil act but the evil mind was not there as the act itself of him being admitted on a psychiatric ward proves that he was insane and there is no need of proving his insanity, therefore he will not be liable of murder but manslaughter and the punishment for his act is to admit him on a psychiatric ward which will be nonsense that is taking him out of the ward and return him to the same place it will be a circle of which is undefined to be done with reasonable people. I think it is nonsense to bring the man to court.
 
Kweli nci hii inakwenda kama mtumbwi fata upepo!! maana jamaa kuweza amka na kujerui wenzake na hata kuuwa je wasimamizi walikua wapi? au yanini kuchangaya wagonjwa kama hawa tena wenye matatizo ya akili pamoja mana hawa hakuna cha anapata afadhali wala nini ni lazima watenganishwe au wafungwe kiasi kwamba hawawezi dhuru wengine,ina maana hapa hata ndugu zake ndio wangekua wamekwenda kumwangalia basi lazima angewashughulikia....kwakeli hapa lazima kitu kifanyike tusifanye vitu kienyeji.
 
Back
Top Bottom