Mgongano wa Kimaslahi (Conflict of Interest)

pappilon

JF-Expert Member
Jan 27, 2015
3,192
3,556
Wana jukwaa habarini za jioni.

Mimi ni mgeni kabisa katika hili jukwaa la sheria na limefika hapa baada ya kutatizwa na hii kitu inayojulikana kama mgongano wa kimaslahi au conflict of interest kwa kimombo. Naomba niende kwenye mada moja kwa moja.

Kuna makubaliano ya uchimbaji wa Madini ya Dhahabu nataka kuingia na Jamaa Fulani hivi, basi katika mkataba huo wakaweka sehemu ya mgongano wa kimaslahi. Katika vipengele vyake kikawepo kimoja ambacho ndo kinanyima Amani Kabisa. Kinasema "Mbia Namba moja (ambaye ndo Mimi) hataruhusiwa kuchimba Dhahabu katika eneo la masumbe au kuwa na hisa ya uchimbaji na mtu yoyote katika eneo hili, pia hatatakiwa kuchimba wala kuwekeza katika uchimbaji katika Wilaya ya KAHAMA kwa kipindi chote cha mkataba huu". Jambo la kusikitisha sana ni kwamba hawataki niwe Mwanachama katika maduara yao ila nina gawio la 10% katika faida itakayopatikana kutokana na uchimbaji tunaofanya.

Sasa wakuu kitu ninachoomba kujua Kutoka kwa wanasheri, je hii kitu ya conflict of interest inatambuliwa na sheria Zetu? Na je application yake inakuweje? Je hiki hawa Jamaa zangu wanachong'ang'ania kibakubalika kisheria?

Kuna Jamaa yangu lawyer nimeongea Naye akaniambia inatakiwa tu ku-declare kwao kuwa nafanya pia Biashara inayofanana na Biashara tunayotaka Kufanya pamoja na si vinginevyo, Je hii ni kweli wakuu Wangu.

Naomba mnisaidie nguli wa sheria maana naona kama mkataba huu unaenda kunifunga pingu kwenye utafutaji Wangu maana shughuli zangu nyingi zinahusisha uchimbaji wa Dhahabu hasa hasa Kanda ya Ziwa.

Naomba msaada wenu wakuu

Kama hii mada ilishawai kuja hapa jukwaani basi naomba radhi kwa kuirudia ila nisaidieni tu wakuu

Jioni njema.
 
Wana jukwaa habarini za jioni.

Mimi ni mgeni kabisa katika hili jukwaa la sheria na limefika hapa baada ya kutatizwa na hii kitu inayojulikana kama mgongano wa kimaslahi au conflict of interest kwa kimombo. Naomba niende kwenye mada moja kwa moja.

Kuna makubaliano ya uchimbaji wa Madini ya Dhahabu nataka kuingia na Jamaa Fulani hivi, basi katika mkataba huo wakaweka sehemu ya mgongano wa kimaslahi. Katika vipengele vyake kikawepo kimoja ambacho ndo kinanyima Amani Kabisa. Kinasema "Mbia Namba moja (ambaye ndo Mimi) hataruhusiwa kuchimba Dhahabu katika eneo la masumbe au kuwa na hisa ya uchimbaji na mtu yoyote katika eneo hili, pia hatatakiwa kuchimba wala kuwekeza katika uchimbaji katika Wilaya ya KAHAMA kwa kipindi chote cha mkataba huu". Jambo la kusikitisha sana ni kwamba hawataki niwe Mwanachama katika maduara yao ila nina gawio la 10% katika faida itakayopatikana kutokana na uchimbaji tunaofanya.

Sasa wakuu kitu ninachoomba kujua Kutoka kwa wanasheri, je hii kitu ya conflict of interest inatambuliwa na sheria Zetu? Na je application yake inakuweje? Je hiki hawa Jamaa zangu wanachong'ang'ania kibakubalika kisheria?

Kuna Jamaa yangu lawyer nimeongea Naye akaniambia inatakiwa tu ku-declare kwao kuwa nafanya pia Biashara inayofanana na Biashara tunayotaka Kufanya pamoja na si vinginevyo, Je hii ni kweli wakuu Wangu.

Naomba mnisaidie nguli wa sheria maana naona kama mkataba huu unaenda kunifunga pingu kwenye utafutaji Wangu maana shughuli zangu nyingi zinahusisha uchimbaji wa Dhahabu hasa hasa Kanda ya Ziwa.

Naomba msaada wenu wakuu

Kama hii mada ilishawai kuja hapa jukwaani basi naomba radhi kwa kuirudia ila nisaidieni tu wakuu

Jioni njema.
Kwani umesha saini huo mkataba????

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huo mkataba wenyewe ni wa Kipuuzi ,samahani kwa neno hilo.
atleast ungekuwa unapewa 30% ndio wangeweza kuweka hizo clause.
Kinyume na hapo. Declare then endelea kama competitor wao.
 
Kwani umesha saini huo mkataba????

Sent using Jamii Forums mobile app

Sikusain mkuu..wakati tunaendelea kulumbana kuhusu vipengele nikatengenezewaa zengwe....soma hapa chini na ikiwezekana unipe ushauri wako mkuu

Wakuu poleni na majukumu, naombeni msaada wenu mawakili wasomi, na wadau wengine Kwenye jukwaa hili. niende moja kwa moja kwenye mada.

Mwaka 2017 nilikutanishwa na Jamaa fulani hivi ambao walikuwa wamejiingiza Kwenye shughuli za Utafiti na uchimbaji wa madini ya Dhahabu.

Walinitaka tufanye kazi pamoja kama mtaalamu wao na mimi nikawaweka bayana kiasi ambacho huwa nalipwa kwa shughuli za Utafiti na uchimbaji wa Dhahabu. (Kiasi XX).

Kiasi kile kwao walisema hawana uwezo wa kunilipa na kimsingi wakasema kuwa hawana kabisa uwezo wa kunilipa ila wakaja na pendekezo kuwa watanipa share katika miradi yote ya Utafiti au Uchimbaji wa madini ya Dhahabu watakayoanzisha au tutakayoanzisha pamoja.

Ila tukakubaliana kuwa wakati nafanya hzo kazi watakuwa wananipa hela ya kujikimu na hata nikitaka pesa zaidi watanipa kwa makubaliano kuwa pesa nitakayochukua nje ya hela ya kujikimu itakuja katwa Kwenye gawio langu.

Basi nikawataka kuwepo na makubaliano rasmi kati yetu na wao, hawakupinga ila kimsingi walitaka tu tufanye kazi kirafiki (gentlemen agreement) ila mm niliwakatalia kuwa haitawezekana.

Kwa hiyo tukakubaliana kuwa waandae makubaliano na kuyatuma kwangu ili na mimi niyapitie.

Ghafla ikatokea kazi ambayo ilinifanya niende field Mara moja, nikaondoka ila nikawataka waandae hayo makubaliano na kuyatuma kwangu kwa email.(hapo nilienda Kufanya Utafiti Kwenye LESENI zao)

Basi tukawa tunaendelea Kufanya Utafiti huku na kule ila kwa Bahati mbaya LESENI zote walizokuwa nazo hazikuwa na majibu mazuri ya Kufanya kuanza uchimbaji au kuziuza kwa mwekezaji.

Kwa kutumia connections zangu nikapata ushirika fulani hv ambao walikuwa na leseni zao ila hawakuwa na mtu wa kuwawezesha mambo Fulani Fulani.

Basi nikawa nimewajulisha Jamaa zangu tukatembelea huo ushirika na tukakubaliana kuwa tutafanya kazi pamoja. Kwa hyo ikabidi mimi nibaki field nikiandaa miundombinu ya kazi na kuanzisha maduara/mashimo ya uchimbaji wa Dhahabu.

Wakati nikiendelea kuandaa miundombinu ya kazi nikaanda makubaliano ya Kufanya kazi kati yangu na hao jamaa. Nilifanya hivi baada ya kusubiri makubaliano Kutoka kwako kama ambavyo tulikubaliana lakini hawakuandaa.

Baada ya kuwatumia yale makubaliano walianza kwa kuomba samahani kuwa walisahau kama ndio walitakiwa kuandaa makubaliano.

Kimsingi walikubaliana na baadhi ya vipengele nilivyoweka Kwenye makubaliano na vingine walivikataa na kuongeza Vya kwako.

Hawakukubaliana na kipengele cha mimi kuwa sehemu ya mmiliki wa maduara (kwa lugha rahisi Mgodi) tutakayoanzisha kwa madai kwamba endapo ubia kati yangu na wao utavunjika basi mimi nitakuwa nawapelekesha kwa vile ni mmoja ya mmiliki wa maduara.

Hiki kipengele sikukubaliana nacho na hata tulipopata wasaa wa Kufanya mazungumzo kwa simu walishindwa kutetea kipengele hiki na wakawa kama wananishawishi tu nukubaliane nao ila hawakuwa na sababu zinazojutosheleza.

Kipengele kingine ni kwamba walisema mimi sitaruhusiwa kuwa ma maduara yangu peke yangu au kuwa na ubia na mtu mwingine yoyote katika shughuli za uchimbaji kwa maeneo ambayo tulikuwepo tofauti na wao. Kipengele hiki pia sikukubaliana nacho.

Wakati tunaendelea kujadiliana Kuhusu makubaliano maduara mawili niliyokuwa nimeyaanzisha yakawa yamefika Kwenye uzalishaji.

Nikawataarifu kuwa maduara yetu yapo vizuri na kuwa kuna mawe nitasaga ili tujue yana uzalishaji kiasi gani.?? Ikumbukwe kuwa maeneo tuliyokuwa tunachimba yalikuwa chini ya ushirika Fulani na huo ushirika ulikuwa na ofisi iliyokuwa inaratibu shughuli zote za uchimbaji.

Siku tunasaga yale mawe akaja muwakilishi wao kwa hyo mawe yakasagwa na yeye akiwepo na Dhahabu kukamatishwa.

Dhahabu iliyopatikana Kwenye Yale mawe tuliyosaga ilikuwa ni ya kutisha maana kiroba kimoja cha wastani wa kilo mia kilitoa gramu 40 za Dhahabu. Yule muwakilishi wao akawa kama kapagawa vile.

Kesho yake mimi nikawa Naendelea na kazi pale mgodini ila yule muwakilishi wao akawa kama hataki kuwa karibu na mimi na muda mwingi anaongea na simu.

Jioni ya siku hyo nikapata simu Kutoka kwa wale Jamaa wakinituhumu kuwa kuna wizi wa mawe ulifanyika Kwenye duara lao na mimi nimehusika.

Na wakaniambia kuwa ofisi ina ushahidi kuhusu wizi uliokuwa unaendelea na wameshanipa onyo Mara kadhaa ila sikuacha.

Niliwajibu kifupi tu kuwa hamna wizi wowote ambao ulishafanyika na hakuna onyo lolote ambalo lilishatolewa na ofisi Kuhusu wizi.

Jamaa haraka haraka tu wakaniambia sisi hatutaki tena biashara na wewe na wakaenda Mbali zaidi wakasema afadhali tulikuwa hatujasaini makubaliano yoyote na wewe. Wakanitaka kila kitu nimkabidhi muwakilishi wao.

Mimi hatua ya kwanza niliyochukua ni kuiandikia ofisi nikawataka kukanusha kuwa kuna wizi ulishatokea na mm nikahusika.

Ofisi ilijibu barua yangu na kukana kuwa sijawahi husika Kwenye wizi wowote na wala sijawahi kupewa onyo lolote.

Baadae ofisi ikaanza Kufanya mchakato wa kunikutanisha na wale Jamaa zangu ili tuone tunamalizanaje. Jamaa zangu hawakukubali kuja site na baada ya mvutano mrefu ofisi wakanishasuri niende nikutane na Jamaa zangu tuone kama tunaweza malizana.

Nilipokutana nao hata zile tuhuma hazikuongelewa badala yake wakasema tu hawawezi kuendelea Kufanya kazi na mm kwa maana hakuna tena trust kati yetu. Mimi nikawaambia kama ndivyo basi wanilipe kile kiasi nilichotaka mwanzoni wakati nakutana na kwa kipindi chote nilichokuwa nao au nibaki na share ya 10% Kwenye ule mradi uliokuwa unaendelea ila mm nisijihusishe na kitu chochote niwepo tu kuangalia maslahi yangu.

Mapendekezo yangu hawakukubaliana nayo, nilipowauliza nyie mnatakaje Mmoja wao akaniambia we ondoka tu tuachie tuendelee na ile kazi halafu siku tukipata faida tutakufikiria, nikawaambia hilo halitawezekana. Tukaachana bila muafaka wowote.

Baadae kupitia kwa mtu fulani wakasema watanipa 30m ili tuachane, baadae ile 30m ikapungua tena ikawa 20m, hata hyo 20m hawakutoa wakawa wanapiga chenga tu.

Sasa hapa nilipo ninataka kwenda mahakamani ili niwafungulie hawa Jamaa kesi ya madai.

Ombi langu kwa mawakili wasomi na wadau wengine yenye uzoefu na kesi za madai, Ni utaratibu/jinsi Gani naweza kuwafungulia hawa Jamaa kesi ya madai.

Au kutokana na Maelezo yangu hapo juu ni utaratibu Gani wa kisheria au kimahakama natakiwa kufuata ili niweze kupata haki yangu.

Nitashukuru sana kwa msaada wenu wakuu
 
Back
Top Bottom