Mgongano wa CHADEMA ni manufaa kwa Taifa

Mwafrika wa Kike

JF-Expert Member
Jul 5, 2007
5,185
56
Ninataka niamini kuwa ni kweli kuwa CHADEMA kuna mgongano kuhusu uteuzi wa zitto kwenye kamati/tume/jinalolote ya JK ya madini. Kama hizi habari ni kweli, basi hii ni dalili nzuri sasa kuwa watanzania wamegundua kuwa kabla ya kukubali au kupitisha jambo lolote kubwa na lenye kugusa maslahi ya watu wengi nchini ni lazima kuwepo na mjadala na mchanganuo wa kutosha.

Ninashawishika pia kusema kuwa kama chama tawala, bunge, halmashauri zetu zingefanya maamuzi kwa msingi wa kuruhusu mawazo ya wengi yasikilizwe ikiwemo wale wanaopinga kabla ya kupitisha vitu haraka haraka Tanzania ingekuwa bila IPTL, Kiwira na maovu mengi yaliyopitishwa na watu wachache sana kwa manufaa yao binafsi.

Hii ni nafasi kwenu viongozi wa CHADEMA kuonyesha nchi hii kuwa mko tayari kutunza demokrasia na kuruhusu utofauti wa nia na mawazo ndani na nje kwa nia ya kujenga kitu kikubwa na chenye manufaa kwa watanzania wa leo na wajukuu zao.

Fanyeni mjadala wazi na kila kitu kiweke pamoja ili mwishoni ikiamuliwa nini kifanyike kunusuru taifa na mafisadi wanaouza nchi, kila mtanzania azidi kujenga imani kwenu na kwa watanzania wote ndani na nje ya serikali waliochoshwa na uozo unaondelea.

Zitto ameshafanya uamuzi wa kuingia katika kamati/? hii na mie naona kuwa ni vyema aingie huko kama hivyo ndivyo anashawishika kufanya. Zitto ameahidi kuwa ataendeleza kulinda maslahi ta Tz kwa hiyo ni vyema apewe nafasi kufanya na kuthibitisha hilo. OK Zitto, kafanye mambo huko ila ukisalimu amri afadhali uombe kazi huko ikulu or something. Kwa sasa GOOD LUCK - NENDA KAFANYE KAZI
 
Ninataka niamini kuwa ni kweli kuwa CHADEMA kuna mgongano kuhusu uteuzi wa zitto kwenye kamati/tume/jinalolote ya JK ya madini. Kama hizi habari ni kweli, basi hii ni dalili nzuri sasa kuwa watanzania wamegundua kuwa kabla ya kukubali au kupitisha jambo lolote kubwa na lenye kugusa maslahi ya watu wengi nchini ni lazima kuwepo na mjadala na mchanganuo wa kutosha.

Ninashawishika pia kusema kuwa kama chama tawala, bunge, halmashauri zetu zingefanya maamuzi kwa msingi wa kuruhusu mawazo ya wengi yasikilizwe ikiwemo wale wanaopinga kabla ya kupitisha vitu haraka haraka Tanzania ingekuwa bila IPTL, Kiwira na maovu mengi yaliyopitishwa na watu wachache sana kwa manufaa yao binafsi.

Hii ni nafasi kwenu viongozi wa CHADEMA kuonyesha nchi hii kuwa mko tayari kutunza demokrasia na kuruhusu utofauti wa nia na mawazo ndani na nje kwa nia ya kujenga kitu kikubwa na chenye manufaa kwa watanzania wa leo na wajukuu zao.

Fanyeni mjadala wazi na kila kitu kiweke pamoja ili mwishoni ikiamuliwa nini kifanyike kunusuru taifa na mafisadi wanaouza nchi, kila mtanzania azidi kujenga imani kwenu na kwa watanzania wote ndani na nje ya serikali waliochoshwa na uozo unaondelea.

Zitto ameshafanya uamuzi wa kuingia katika kamati/? hii na mie naona kuwa ni vyema aingie huko kama hivyo ndivyo anashawishika kufanya. Zitto ameahidi kuwa ataendeleza kulinda maslahi ta Tz kwa hiyo ni vyema apewe nafasi kufanya na kuthibitisha hilo. OK Zitto, kafanye mambo huko ila ukisalimu amri afadhali uombe kazi huko ikulu or something. Kwa sasa GOOD LUCK - NENDA KAFANYE KAZI
Mwafrika wa Kike,

Flip flopping, when did you change your mind on this? I thought you were against the idea of Zitto joining the committee.
 
Mwafrika wa Kike,

Flip flopping, when did you change your mind on this? I thought you were against the idea of Zitto joining the committee.

Pliz, read my thread. I am against the idea of Zitto joining the committee. I also can not and will never decide for the guy on what he should do/not do.

He has decided to join, so let him join. There is nothing I can do here. CHADEMA is not CCM. Zitto is not gonna be kicked out or kolimbalized by the party for being himself. This is why I am for democracy in CHADEMA here.

Zitto has made up his mind, so let him join. I however promise a rough ride here if he fails to protect Tanzanians' interests.
 
from my opinion
labda tusikilizei matokeo ya kamati ya chadema itakayakoaa na ktoa msimamo.
ila kwa mini ningeafiki kama tume hii ingeundwa na bunge letu ili kuondoa utata wa kuficha ripoti kama kamati za awali zilizoundwa nje ya bunge. je kuna nini kinafichwa hapa??
 
Kwa maoni yangu, hiki inachoitwa mgogoro wa Chadema kuhusiana na Zitto ni ukomavu wa kisiasa na kama Chadema kitaonyesha kuwa na viongozi makini na wakomavu, watakuwa wamefanikiwa sana kuchota hisia za watu wakiwamo CCM na vyombo vyao vya habari na hivyo kujikuta wakifanikiwa sana kisiasa kwa kutumia mwanya huu. Tena unakuta sasa hii kamati badala ya kuitwa Kamati ya Bomani inaitwa Kamati ya Zito ama Kamati ya Buzwagi, kwa kweli haya ni mafanikio makubwa ambayo Chadema wanapaswa kutumia utaalamu wa hali ya juu kucheza karata ya kisiasa na kuweza kupasua mawimbi.

Pamoja na kuwa suala la madini linahusu maslahi ya taifa, katika kutetea maslahi ya taifa ni lazima uwe na nguvu ya kisiasa na kukubalika kisiasa. Upinzani waliweza kuwafanya wananchi wawaamini, hasa baada ya suala la Buzwagi. Waendelee kutumia karata hii ya Zitto kuendelea kuvuta hisia na imani ya wananchi na si kuwakatisha tamaa njiani. Kosa moja litawafanya wananchi wapoteze imani, na wakipoteza imani wataendelea kutumiwa na kuburuzwa na CCM na mafisadi ndani na nje ya CCM.

Watatanua kwa kuwa hawatakua na waku wakemea, na hata wakiwapo wananchi, hawatawaamini. Mbowe, Zitto, Slaa, Kimesera, Mnyika, Chacha, na wengineo, mujue ama zao ama zenu katika hili. Hili si suala la ubinafsi tena, hapa ni utaifa mbele. Wananchi wanafuata, halafu ndio Chadema inafuata, kabla ya watu binafsi kufuatia. Acheni ubinafsi. Angalieni mbele.
 
Mwafika wa kike,sasa kama Zitto akiteuliwa kuwa Waziri mtakakataa wanachama wa Chadema? Mie naona mnacheza cheusi chekundu i mean karata 3 Zitto kuwa pale ni kwa maslahi ya taifa au Chadema?? na Chadema ni kwa ajili yenu akina Mtei na Mbowe au ya Taifa?

Hebu acheni siasa za ajabu muacheni afanye kazi kama kweli alikuwa against na mikataba mibovu ya madini atasema nakama akikubaliana na hali ile nae atakuwa wale wale tu
 
mwafika wa kike,sasa kama Zitto akiteuliwa kuwa Waziri mtakakataa wanachama wa Chadema? Mie naona mnacheza cheusi chekundu i mean karata 3 Zitto kuwa pale ni kwa maslahi ya taifa au Chadema?? na Chadema ni kwa ajili yenu akina Mtei na Mbowe au ya Taifa?
Hebu acheni siasa za ajabu muacheni afanye kazi kama kweli alikuwa against na mikataba mibovu ya madini atasema nakama akikubaliana na hali ile nae atakuwa wale wale tu

Kitu ambacho wana ccm mmeshindwa kujua hapa ni kuwa tatizo sio zitto anapata nini binafsi hapa. Issue hapa ni maslahi ya taifa na demokrasia ndani ya CHADEMA.

Tofauti na huko ccm ambako kila kinachoamriwa na wakubwa ndicho kinafanyika, huku nje mambo ni tofauti. Watu wanajadili na kutoa madukuduku yao kabla ya kufikia maamuzi.

Kila mtu anasikilizwa kwanza na anajibiwa kwa hoja baada ya kuwa amesikilizwa - kama unaona debate yangu na Kitila kwenye ile thread nyingine. Hakuna mambo ya kufukuza watu uanachama au kukolimba watu hapa. Kila wasiwasi lazima ufanyiwe kazi na hii ndio demokrasia ya CHADEMA.

Zitto ana uhuru binafsi wa kufanya anachopenda na nakuhakikishia kuwa hatalazimishwa na mimi au yeyote mwenye akili cha kufanya.

Yeye ameamua kuingia kwenye kamati na that's ok. CHADEMA wao watakaa na kupanga mkakati kuhakikisha kuwa matokea ya hii tume sio kama zile mia tano zilizopita na pia kuwa Zitto anapata kila ushauri unaohitajika. Mimi napinga hii tume lakini sina uwezo wa kumuamulia zitto cha kufanya.

Sina tabia ya kujibu hypothetical questions so sitajibu swali lako la kuhusu zitto kupewa uwaziri maana again hayo yote ni uamuzi wake. Zitto akiamua kama Lamwai aingie ccm au apewe cheo na uwaziri hiyo ni juu yake na haitakuwa mwisho wa mapambano dhidi ya wezi na mafisadi walioko serikalini right now.
 
Mtu, kama anavyosema mwafrika, inabidi tufike mahala tuelewe kuwa siasa is about fikra, ambayo inajengwa kwa kuruhusu watu kutoa mawazo tofautitofauti. Tatizo moja lililotufikisha hapa tulipo ni utamaduni wa kutosema mawazo yetu kwa uhuru. Wanasiasa wa CCM hawawezi kutoa mawazo yao hadi wajue kwanza kiongozi wao anafikiria nini ili watakapoongea waongee yale anayotaka asikie. And this way we have killed a lot of potentials in our people. We must change, and CHADEMA ia showing the way.
 
Kitu ambacho wana ccm mmeshindwa kujua hapa ni kuwa tatizo sio zitto anapata nini binafsi hapa. Issue hapa ni maslahi ya taifa na demokrasia ndani ya CHADEMA.

Mkuu Heshima mbele, the ishu ni Chadema na Zitto na kamati ya rais, sasa CCm inatokea na kuingilia wapi? Siasa sio lazima iwe kila ishu, kuna sometimes inabidi ifike mwisho na this is one of those ishus.

Maana kama ni kukomaaa kwa chama wananchi ndio wanaojua zaidi na walishaamua kwenye kura zao, hata kura za uongozi mdogo tu wa madiwani, wao wanajua ni nani aliyekomaa kidemokrasia, lets talk Zitto na kamati, the real ishu hapa!

Mkishachanganya, na sisi wananchi mnatuchanganya! Mkuu Kitila you are too big for this!
 
Mkuu Heshima mbele, the ishu ni Chadema na Zitto na kamati ya rais, sasa CCm inatokea na kuingilia wapi? Siasa sio lazima iwe kila ishu, kuna sometimes inabidi ifike mwisho na this is one of those ishus.

Maana kama ni kukomaaa kwa chama wananchi ndio wanaojua zaidi na walishaamua kwenye kura zao, hata kura za uongozi mdogo tu wa madiwani, wao wanajua ni nani aliyekomaa kidemokrasia, lets talk Zitto na kamati, the real ishu hapa!

Mkishachanganya, na sisi wananchi mnatuchanganya! Mkuu Kitila you are too big for this!

Mkulu FMES,

Wewe ukianza kuleta mambo ya uchaguzi wa madiwani hapa ndio sasa unataka the whole thing ichanganywe kabisaa. Mimi nimejibu swali la mtu (ambaye ni mwanaccm) kuhusu debate inayoendelea CHADEMA.

Ukweli upo wazi, bungeni wanachama wa ccm wanaungana kupitisha mambo ya ajabu (likiwemo la kufukuzwa zitto) bila kuweka debate ya nguvu na kuhoji maamuzi ya hoja za viongozi wao. Hii debate ya CHADEMA inaoenyesha demokrasia ndani ya chama na mimi ndicho ninaongelea hapa kwa kuweka utofauti kati ya ccm na CHADEMA.

Ukitaka tuanze kuongelea uchaguzi wa madiwani, niko more than willing kufanya hivyo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom