Mgomo wa waalimu nchi nzima waja

Mpaka Kieleweke

JF-Expert Member
Feb 27, 2007
4,132
1,571
Chama cha waalimu kinaendelea na zoezi la kujaza fomu kwa ajili ya kuitisha mgomo wa waalimu nchi nzima kushinikiza wao kulipwa haki zao pamoja na madeni yao ambayo serikali inadaiwa.

Wamesema kuwa watatangaza aina ya mgomo soon, na wakati huo huo TUICO nayo inasema kuwa mgomo wao uko pale pale kwani mjadala umekuwa wa muda mrefu sana sasa wanasema kuwa azima ya mgomo iko pale pale.

Nchi inakokwenda sijui kwani kila mahali moto...
 
Haya sasa yangu macho!I wish kungekuwa na mgomo wa kumlazimisha JK ajiuzulu kama ule wa Victor Yanukovich na Victor Yuschenko the so called ORANGE REVOLUTION ningekuwa Frontline kwa kweli!
 
Tangazo hilo limetolewa na Rais wa chama cha waalimu, na amewataka waalimu wote nchini kujaza fomu za mgomo na hatimaye wataiandikia serikali rasmi kuhusu mgomo huo.

L a TUICO kasema Ngulla mwenyekiti wao.
 
Kwa mujibu wa TBC ni kuwa mkoani morogoro waalimu 600 kati ya waalimu 760 tayari wamehudhuria kikao leo na wamejaza fomu zao kuwa wanakubaliana na mgomo.

Walikuwa kwenye kikao leo.
 
Wanagoma kiwongowongo hao wakiambiwa watayarishe maandamano kwenda kwenye kampeni za CCM wanakuwa wa mwanzo na kama mwanafunzi hakuhudhuria basi wanaweza hata kumufkuza shule, huo ndio utawala wa CCM baba.Si mshaambiwa mvumilie sasa maandamano ya nini ?
 
Wanagoma kiwongowongo hao wakiambiwa watayarishe maandamano kwenda kwenye kampeni za CCM wanakuwa wa mwanzo na kama mwanafunzi hakuhudhuria basi wanaweza hata kumufkuza shule, huo ndio utawala wa CCM baba.Si mshaambiwa mvumilie sasa maandamano ya nini ?
Ni kweli walimu ni kati ya watu walioshabikia sana kuchaguliwa kwa JK. Sijui kwa kuwa ni shemeji yao?
Wao ni wepesi kudanganywa wakakubali. Na ni hao hao ambao uchaguliwa kuendesha chaguzi bila hata kupewa soda, na wakijua wanalo rungu mkononi la kuweza kuwashawishi wapiga kura kuinyima ccm kura wameshindwa kuitumia.
Sasa wacha waipate ili next time wajue kitumbua si keki.
 
Kuna mgomo baridi unaendelea bandarini kitengo cha container tangu tarehe 05/08/08.
Jamaa hawalipwi mishahara mizuri,pia kuna ufisadi wa manunuzi ya crane mbovu.
 
Theopista Nsanzugwanko
Daily News; Friday,August 08, 2008 @00:03

Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA) limeahirisha mgomo wa watumishi wa Umma nchi nzima uliokuwa uanze kesho. Mgomo huo wa wafanyakazi uliokuwa uambatane na kufanya maandamano katika wilaya na mikoa wakipinga serikali kuwanyanyasa, kuwanyima nyongeza na malimbikizo ya mishahara ulitolewa taarifa kwa Baraza la Kazi Uchumi na Masuala ya Jamii (LESCO).
Akitangaza uamuzi huo mbele ya waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa TUCTA Nestory Ngulla, alisema shirikisho hilo litatoa taarifa rasmi ya siku ya kuanza mgomo wa watumishi wa umma Jumatatu.

Ngula ambaye alikuwa ameandamana na viongozi wa vyama vyote vya wafanyakazi vinavyounda shirikisho hilo, aliwataka wanachama wote wa vyama vya wafanyakazi na wafanyakazi kwa ujumla kuwa wavumilivu kusubiri tamko la kuanza mgomo huo.

Mwezi uliopita, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA) lilitangaza nia yake ya kutangaza mgomo wa wafanyakazi wote nchini na kufanya maandamano katika wilaya na mikoa wakipinga serikali kuwanyanyasa, kuwanyima nyongeza na malimbikizo ya mishahara.
 
Ni kweli walimu ni kati ya watu walioshabikia sana kuchaguliwa kwa JK. Sijui kwa kuwa ni shemeji yao?
Wao ni wepesi kudanganywa wakakubali. Na ni hao hao ambao uchaguliwa kuendesha chaguzi bila hata kupewa soda, na wakijua wanalo rungu mkononi la kuweza kuwashawishi wapiga kura kuinyima ccm kura wameshindwa kuitumia.
Sasa wacha waipate ili next time wajue kitumbua si keki.[/B]


sasa hapa ninachojiuliza inakuwaje ukipita mitaani watu wanashabikia serikali kuwa imetenda mambo kibao na kusaidia maisha bora, wakati inaelekea makundi ya watu wote yako kwenye maandamano na migomo

na hapo hapo utasikia ukifika uchaguzi hawa niliowataja hapo juu wao ndio wa kwanza kabisa, tena aibu ni kwamba kama wanachuo wao walinunuliwa kwa kubebwa na mabasi ya scandinavia, kofia na vijitishert, na wengineo ndio huko,
Huku tukiendelea kuimba na kukisifia chama cha Mafisadi moto tunauoa, endeleeni kugoma na wakati mkiichagua CCM ambayo inaongozwa na mafisadi na watu wenye upeo mdogo sijui kama mtapata majibu ya maandamano zaidi ya mabomu tuu



Mi naona nyie mwapanda mbegu mbovu; I think you are just frustrated - but so is everybody!!
Sioni shida mtu akilalamika, ila tusipotoshe tafadhali, ...tafadhali! Wanafunzi 10 kati ya 200 wakivishwa kofia sio sahihi kuwatwika lawama wanafunzi wote 200.

Kuhusu waalimu, mimi ni shuhuda. Ipo shule tena yenye wanafunzi wengi tu, mkuu wa shule na wenzie wawili ni makada wa SISIEMU. Matendo yao yako dhahiri kabisa nisingependa kusema mengi nisijefichua identity yangu. Waalimu katika shule hiyo ya serikali hawafanani kabisa na mnayosema hapo juu isipokuwa hao watatu.

Nitatoa mfano mmoja na sio zaidi.
Mkuu huyu wa shule alibadilisha ratiba ya kuifunga shule kusudi wanafunzi wawe makwao siku ya kupiga kura 2005. Kumbuka sheria inasema ni lazima ukapige kura katika kituo ulichojiandikisha na hawa wanafunzi walijiandikisha shuleni (boarding school). Bahati nzuri mwaka 2005 uchaguzi uliahirishwa, kwa hiyo wananafunzi walipiga kura.
Msiwatupie lawama waalimu kwa kitu msichokuwa na hakika nacho. Don't make it look like majority of teachers are like that. Waalimu wasaliti wanahesabika na mifano tunayo.

Ikiwa waalimu walio wengi hawataitikia wito wa mgomo, tujiulize kwanini badala ya kulaumu.




.
 
ili Kuandamana lazima mjaze fomu?....uwoga au strategy....? Hivi maandamano yote yangesubiri watu wajaze fomu, sijui kama kungefanyika maandamano...WALIMU AMKENI...KTK WATU MNAOWEZA KUFANYA MABADILIKO KTK NCHI HII NI NYINYI....

Msingi wa maandamano ni kujua legality ya ya kile mnachotaka kukigomea. Nakumbuka walimu waligoma wakati wa Mzee Ruksa, Wakati wa Mkapa, Mkapa akataka waandamane kwa vifijo kwa style Povu lake la kupambana na RUSHWA!!!

Ushauri wangu naomba tufungue thread Mzima juu ya Madai ya Walim wetu, then tujadili kwa kina hapa JF, najua wengi wa walimu wetu access ya Mtandao ni ngumu, lkn wale wa karibu au wenye access tuchukue nyeti ili tuwasaidie wenzetu, Najua matatizo ya Nchi yetu ni Mengi, lkn for me Waalim ni tool kubwa sana juu ya mabadiliko tunayoyazungumzia hapa JF
 
Tangazo hilo limetolewa na Rais wa chama cha waalimu, na amewataka waalimu wote nchini kujaza fomu za mgomo na hatimaye wataiandikia serikali rasmi kuhusu mgomo huo.

L a TUICO kasema Ngulla mwenyekiti wao.

Wamuongezee ulinzi au ajifiche kabis au ahamie pale ofisini kwao na ulinzi mkali wamuwekeee, maana nijuavyo watu wasio julikana huyu lazima apotee soon.
 
ili Kuandamana lazima mjaze fomu?....uwoga au strategy....? Hivi maandamano yote yangesubiri watu wajaze fomu, sijui kama kungefanyika maandamano...WALIMU AMKENI...KTK WATU MNAOWEZA KUFANYA MABADILIKO KTK NCHI HII NI NYINYI....

Msingi wa maandamano ni kujua legality ya ya kile mnachotaka kukigomea. Nakumbuka walimu waligoma wakati wa Mzee Ruksa, Wakati wa Mkapa, Mkapa akataka waandamane kwa vifijo kwa style Povu lake la kupambana na RUSHWA!!!

Ushauri wangu naomba tufungue thread Mzima juu ya Madai ya Walim wetu, then tujadili kwa kina hapa JF, najua wengi wa walimu wetu access ya Mtandao ni ngumu, lkn wale wa karibu au wenye access tuchukue nyeti ili tuwasaidie wenzetu, Najua matatizo ya Nchi yetu ni Mengi, lkn for me Waalim ni tool kubwa sana juu ya mabadiliko tunayoyazungumzia hapa JF


NI kugoma na sio kuandamana na iyo ipo kisheria.
 
Theopista Nsanzugwanko
Daily News; Friday,August 08, 2008 @00:03

Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA) limeahirisha mgomo wa watumishi wa Umma nchi nzima uliokuwa uanze kesho. Mgomo huo wa wafanyakazi uliokuwa uambatane na kufanya maandamano katika wilaya na mikoa wakipinga serikali kuwanyanyasa, kuwanyima nyongeza na malimbikizo ya mishahara ulitolewa taarifa kwa Baraza la Kazi Uchumi na Masuala ya Jamii (LESCO).
Akitangaza uamuzi huo mbele ya waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa TUCTA Nestory Ngulla, alisema shirikisho hilo litatoa taarifa rasmi ya siku ya kuanza mgomo wa watumishi wa umma Jumatatu.

Ngula ambaye alikuwa ameandamana na viongozi wa vyama vyote vya wafanyakazi vinavyounda shirikisho hilo, aliwataka wanachama wote wa vyama vya wafanyakazi na wafanyakazi kwa ujumla kuwa wavumilivu kusubiri tamko la kuanza mgomo huo.

Mwezi uliopita, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA) lilitangaza nia yake ya kutangaza mgomo wa wafanyakazi wote nchini na kufanya maandamano katika wilaya na mikoa wakipinga serikali kuwanyanyasa, kuwanyima nyongeza na malimbikizo ya mishahara.
Wajinga nyinyi ikifika wakati wa uchaguzi mnanunuliwa mnawasaliti wananchi..kwa Sasa tunaisoma namba mnaanza ujinga wenu kwendaaa ntaenda kazini...kila mtu apambane na Hali yake...
 






Mi naona nyie mwapanda mbegu mbovu; I think you are just frustrated - but so is everybody!!
Sioni shida mtu akilalamika, ila tusipotoshe tafadhali, ...tafadhali! Wanafunzi 10 kati ya 200 wakivishwa kofia sio sahihi kuwatwika lawama wanafunzi wote 200.

Kuhusu waalimu, mimi ni shuhuda. Ipo shule tena yenye wanafunzi wengi tu, mkuu wa shule na wenzie wawili ni makada wa SISIEMU. Matendo yao yako dhahiri kabisa nisingependa kusema mengi nisijefichua identity yangu. Waalimu katika shule hiyo ya serikali hawafanani kabisa na mnayosema hapo juu isipokuwa hao watatu.

Nitatoa mfano mmoja na sio zaidi.
Mkuu huyu wa shule alibadilisha ratiba ya kuifunga shule kusudi wanafunzi wawe makwao siku ya kupiga kura 2005. Kumbuka sheria inasema ni lazima ukapige kura katika kituo ulichojiandikisha na hawa wanafunzi walijiandikisha shuleni (boarding school). Bahati nzuri mwaka 2005 uchaguzi uliahirishwa, kwa hiyo wananafunzi walipiga kura.
Msiwatupie lawama waalimu kwa kitu msichokuwa na hakika nacho. Don't make it look like majority of teachers are like that. Waalimu wasaliti wanahesabika na mifano tunayo.

Ikiwa waalimu walio wengi hawataitikia wito wa mgomo, tujiulize kwanini badala ya kulaumu.




.
Wakati wa uchaguzi wanahongwa vijihela wanasaliti wananchi wanaongoza oparesheni za kuiba kura za wapinzani....
 
Back
Top Bottom