Mgomo wa nchi nzima

Matata

Member
Mar 28, 2006
23
10
Nani zaidi? Wananchi au Mafisadi? Watanzania ndugu zangu, tumeonewa kiasi cha kutosha, tumeibiwa kiasi cha kutosha, tumedanganywa kiasi cha kutosha, tumedhulumiwa kiasi chakutosha. Sasa tumechoka na ufisadi huu, upole wetu umetuponza, kinachotakiwa sasa ni sisi wananachi kushika hatamu ya nchi yetu wenyewe. Tutakuwa wajinga kuendelea kuongozwa na mafisadi. Natoa wito wa mugomo nchi nzima, tuandamane kwa amani kuonyesha mshikamano. Kuanzia kwa vyama vya wafanyakazi, wanafunzi, vikosi vyote vya ulinzi, wakulima, wafanyakazi nk. tuandamane mpaka hao Mafisadi wa achie ngazi. Inabidi wananchi tuwe na mshikamano, tuachilie tofauti zetu za kichama ilitukomboe nchi yetu inayouzwa na mafisadi. Naomba polisi, JWTZ, Usalama wa Taifa, tuwe kitu kimoja wachie raia wakomboe nchi yao, isitoshe nanyie ni nchi yenu.
Mungu ibariki Tanzania
 
Naunga mkono,nadhani kuna taratibu zinaandaliwa,huo mgomo na msukosuko upo unakuja tu.
 
Kwa ushauri tu hawa wanaoandaa huo mgomo wajaribu kuangalia namna wanasiasa wa Bolivia walivyoweza kuwashirikisha wakulima na jamii masikini katika kufanikisha maandamano na mogomo ya amani iliyoleta mabadiliko ya katiba nk huko Bolivia. Haitakiwi kuwaambia tu wananchi waje kushiriki ila wanatakiwa kwanza wahakikishe wananchi wanafeel kwa dhati kuwa wao ni part of the solution.Vinginevyo watafeil.
 
Maandamano ya nguvu yanahitajika.Ila kujipanga kuzuri tu na kuyaambatanisha na HOJA NZITO,kung'ang'ana kwa nguvu zote na kwa Amani.Mimi nadhani hata Polisi na jeshi la wananchi nao ni ndugu zetu na wamepigika vilevile.Tuungane kwa nguvu zote hata bunge livunjwe kupitia njia sahihi ya nguvu ya umma.Inawezekana kama Bolivia,Burma,Yugoslavia etc.
 
wazo zuri sana na kama likitekelezwa kwa mikakati mizuri ya kuwakataa mafisadi na kudai sheria za mikataba na mabadiliko ya sheria za kikandamizaji basi tafanikiwa sana.
 
Hili wazo ni zuri sana, na nadhani muda umefika wa sisi Watanzania kuamka kutoka kwenye usingizi wa miaka nenda miaka rudi! huu ufisadi wa viongozi wetu umezidi kiasi...yaani wanatufanya sisi wote ni maf_ _ _ _!

Kikwete kama hawezi kuwashughulikia hao maswahiba wake, basi aachie ngazi! Manake kila kitu kina mwanzo bwana....Rais Nixon alipigwa presha enzi zake baada ya ma-scandal na anakijiuzulu, Rais Clinton pia aliaibishwa baada ya ufuska wake kuanikwa nje! Nusu ajiuzulu! Sasa basi, kwa nini viongozi wetu wasiletewe kasheshe hizo hizo? Tunaogopa nini? Hivi tunakaa tu kimya tukiangalia eti "Mama JK amechaguliwa kwenye kamati ya upuuzi gani sijui...," na "Mtoto wa JK amechaguliwa kwenye kamati ya upuuzi ule....." Hivi jamani mnategemea mama JK au mtoto wake, au hata shangazi yake akigomea ujumbe wa kitu fulani hatachaguliwa? Lazima atachaguliwa tu, kwa sababu ya rushwa, kujulikana na kujipendekeza kwetu tu! Na kwa nini hawa watu wajihusishe kwenye politics? Hivi hizi nyadhifa ni za "KIFALME", yaani zinarithishwa???? Mama JK anatakiwa ajitolee muda wake ahudumie watoto yatima au something useful! Na hawa watoto wa viongozi wasijitajirishe kwa migongo yetu!!!! ENOUGH IS ENOUGH!Huu ni wakati wa uwazi bwana!

Na huu upuuzi kwamba eti Rais mstaafu hawezi kushitakiwa, ni upumbavu kabisa, maana kwa namna hii basi kila rais anayekuja atafanya madhambi, akitegemea kwamba hataguswa! Kumbukeni Rais Mobutu wa Zaire, alijilimbikizia mali kibao wakati wananchi wake wanakufa na njaa! Sasa basi, Mkapa afikishwe mbele ya vyombo vya dola, ajibu mashtaka, na anyang'anywe mali zake alizopata kwa kutuibia watanzania! Wakati ndio huu.....wakati umefika sasa, tuamke na tuungane! Tuache ujinga, na kujibweteka!!!!!!
 
Mwanzo wa mwisho umefika kwa CCM!! Nani alijua Ukuta wa Berlin utaangushwa na wananchi? Nana alijua kuwa Soviet Union ingeporomoka? Wananchi wameishajua janja ya nyani, hawana tena imani na viongozi wa CCM na Baraza la mawaziri. Bahati nzuri tumeishapata watu wa kumfunga paka kengere, sasa tunangoja nini? Inatia uchungu kuona nchi inaliwa na kuuzwa wakati wenye nchi wanakufa kwa njaa. Wakati wa Ukombozi ni sasa. "It can be done, play your part"
 
natuige mfano wa MYANMAR, maandamano ya amani yaliyoshirikisha matabaka yote ya watu
 
Mimi nadhani ya kuwa maandamano yoyote lazima yawe na msingi. Mnaandamana kuomba nini au kwa malengo gani? Mfano wa Myanmar ni mzuri, kwani waliandamana wakapigwa na kufungwa jela na jeshi bado linaendelea kutawala! No results. Tujifunze kutoka Ukraine kwa mfano, you must have a point. Je mnaandamana kubadili mkataba? Au mnasema tu mmechoka? Mnataka kupindua nchi!!? You have to walk a thin line, it's dangerous. Kumbukeni jeshi letu linaweza kuona kuwa srikali imeshindwa ikatake over - God Forbid!
Nadhani kuna wanasheria wengi ambao watakuwa tayari kuangalia nini kinawezekana kikatiba. Kwanza nadhani mfano wa Nixon ni mzuri you start with the executive power kama bunge litashindwa kum-impeach au rais akivunja bunge (I beleive he has that kind of power), than other demands have to be placed. But I think that it's important to think everything through! I welcome input from legal experts.
 
natuige mfano wa MYANMAR, maandamano ya amani yaliyoshirikisha matabaka yote ya watu

..ukisema matabaka yote unamaanisha nini?matajiri,wafanyakazi,wafanyabiashara,wakulima,?au?

..maana kimsingi,matabaka ni nadra kushirikiana!na hapa kwetu ndo kabisaa!

..huu mgomo sijui utakuwa-pulled vipi,...
 
Back
Top Bottom