Hii ni sehemu ndogo tu ya wodi mojawapo za Muhimbili. Kama hapa ndo Hospitali ya Taifa, huko kwingine kukoje?
Kama ilivyo katika sehemu nyingi zinazotoa huduma za afya hapa nchini na hospitali ya taifa Muhimbili kwa ujumla, hali ya utoaji wa huduma za afya ni mbaya.
Haya ni baadhi ya mapungufu utakayoshuhudia ukienda Muhimbili kulazwa!
1. Msongamano wa wagonjwa wodini
Msongamano ni wa hali ya juu sana hadi kupelekea wagonjwa wengi wenye maradhi mbalimbali na mengi ya kuambukiza kama kifua kikuu na hepatitis kurundikana wodi moja.
Mfano wodi moja ina uwezo wa kulaza wagonjwa/vitanda 33. Lakini wagonjwa kwa siku ni 40 hadi 100 katika wodi moja. Hii hupelekea wagonjwa kulala chini kuambukizana magonjwa na utoaji wa huduma uko chini ya kiwango.
2. Uhaba wa manesi
Kwa kawaida wastani wa nesi kwa mgonjwa unatakiwa kuwa 1:6
Lakini kwa sasa kila shifti wanaingia manesi wawili tu. Yaani ratio ni 2:40-100(1:20-50)
Imeadhiri sana utoaji wa huduma. Wagonjwa hawapati dawa kwa wakati na wakati mwingine hukosa kabisa.
Kwa sababu hiyo wagonjwa wanakaa sana wodini na wengine wanakufa bila uangalizi (unattended deaths). Yaani unaweza kupita raundi na kufanya kazi ya kugundua maiti za watu waliokufa bila taarifa!! Unyama gani huu kwa binadamu. Na hili linahitaji mahakama ya kazi?!!
3. Uhaba wa madawa
- Kuna uhaba mkubwa wa madawa ya dharura kama Junior ASA, Lasix, Clopidogrel, aldactone na nyingine nyingi kwa ajili ya dharura za magonjwa ya moyo na mapafu.
- Uhba wa dawa za kutibu magonjwa nyemelezi kwa wenye Ukimwi kama fluconazole nk.
- Madawa mengine mengi muhimu hayapo mf. Tramadol, lactulose, madawa ya magonjwa ya mishipa ya fahamu nk.
Madawa muhimu kwa magonjwa hatari ya mapafu kama nebulizers na steroids mara nyingi hakuna. Wagonjwa hufa bila sababu.
4. Uhaba wa vitendea kazi
Mashuka- Yanatakiwa mashuka 8 kwa kila kitanda kwa siku. Lakini Muhimbili inatoa shuka moja tu kwa kila kitanda kwa siku. Hii hupelekea uchafu na kuambukizana maradhi
Vifaa vingine kama infusion pumps, nebulizing machines (kwa wagonjwa wa
pumu hatarishi) nk hakuna
Hakuna hata mipira na mifuko ya mikojo haipo. Kila kitu hakuna. Wananchi wanateseka.
Kukosekana kwa vitendea kazi clinic kama BP machine, stethoscope nk.nk
5. Ukosekanaji na ucheleweshaji wa vipimo muhimu
- Mfano CT scan ambayo tangu mwaka jana haifanyi kazi
- OGD tangu mwaka jana November haifanyi kazi
- Vipimo huchukua muda mrefu hivyo wagonjwa hufa au huondoka hospitali bila magonjwa yao kufahamika. Mfano USS booking hadi wiki mbili (sababu hakuna mashine na wataalamu wa kutosha kufanya vipimo), ECHO n.k,
6. Magonjwa ya kuambukizwa na chanjo
- Madaktari na manesi wako katika hatari kubwa ya kuambukizwa magonjwa hatari kama ukimwi, Hepatitis, nk.
- Pamoja na hatari hii, hakuna motisha wala chanjo inayotolewa kuwakinga na wala hakuna fidia inayoeleweka
Matatizo yaliyotajwa ni machache. Yapo mengi mengine ambayo yanahitaji pia kutatuliwa kwa haraka.
Madaktari wetu wameshasema. Serikali inakimbilia propaganda za posho na mishahara kwenye vyombo vya habari! Mazingira mazuri ya kazi, wagonjwa kupona ndiyo ahueni(satisfaction) ya daktari.
Kama ilivyo katika sehemu nyingi zinazotoa huduma za afya hapa nchini na hospitali ya taifa Muhimbili kwa ujumla, hali ya utoaji wa huduma za afya ni mbaya.
Haya ni baadhi ya mapungufu utakayoshuhudia ukienda Muhimbili kulazwa!
1. Msongamano wa wagonjwa wodini
Msongamano ni wa hali ya juu sana hadi kupelekea wagonjwa wengi wenye maradhi mbalimbali na mengi ya kuambukiza kama kifua kikuu na hepatitis kurundikana wodi moja.
Mfano wodi moja ina uwezo wa kulaza wagonjwa/vitanda 33. Lakini wagonjwa kwa siku ni 40 hadi 100 katika wodi moja. Hii hupelekea wagonjwa kulala chini kuambukizana magonjwa na utoaji wa huduma uko chini ya kiwango.
2. Uhaba wa manesi
Kwa kawaida wastani wa nesi kwa mgonjwa unatakiwa kuwa 1:6
Lakini kwa sasa kila shifti wanaingia manesi wawili tu. Yaani ratio ni 2:40-100(1:20-50)
Imeadhiri sana utoaji wa huduma. Wagonjwa hawapati dawa kwa wakati na wakati mwingine hukosa kabisa.
Kwa sababu hiyo wagonjwa wanakaa sana wodini na wengine wanakufa bila uangalizi (unattended deaths). Yaani unaweza kupita raundi na kufanya kazi ya kugundua maiti za watu waliokufa bila taarifa!! Unyama gani huu kwa binadamu. Na hili linahitaji mahakama ya kazi?!!
3. Uhaba wa madawa
- Kuna uhaba mkubwa wa madawa ya dharura kama Junior ASA, Lasix, Clopidogrel, aldactone na nyingine nyingi kwa ajili ya dharura za magonjwa ya moyo na mapafu.
- Uhba wa dawa za kutibu magonjwa nyemelezi kwa wenye Ukimwi kama fluconazole nk.
- Madawa mengine mengi muhimu hayapo mf. Tramadol, lactulose, madawa ya magonjwa ya mishipa ya fahamu nk.
Madawa muhimu kwa magonjwa hatari ya mapafu kama nebulizers na steroids mara nyingi hakuna. Wagonjwa hufa bila sababu.
4. Uhaba wa vitendea kazi
Mashuka- Yanatakiwa mashuka 8 kwa kila kitanda kwa siku. Lakini Muhimbili inatoa shuka moja tu kwa kila kitanda kwa siku. Hii hupelekea uchafu na kuambukizana maradhi
Vifaa vingine kama infusion pumps, nebulizing machines (kwa wagonjwa wa
pumu hatarishi) nk hakuna
Hakuna hata mipira na mifuko ya mikojo haipo. Kila kitu hakuna. Wananchi wanateseka.
Kukosekana kwa vitendea kazi clinic kama BP machine, stethoscope nk.nk
5. Ukosekanaji na ucheleweshaji wa vipimo muhimu
- Mfano CT scan ambayo tangu mwaka jana haifanyi kazi
- OGD tangu mwaka jana November haifanyi kazi
- Vipimo huchukua muda mrefu hivyo wagonjwa hufa au huondoka hospitali bila magonjwa yao kufahamika. Mfano USS booking hadi wiki mbili (sababu hakuna mashine na wataalamu wa kutosha kufanya vipimo), ECHO n.k,
6. Magonjwa ya kuambukizwa na chanjo
- Madaktari na manesi wako katika hatari kubwa ya kuambukizwa magonjwa hatari kama ukimwi, Hepatitis, nk.
- Pamoja na hatari hii, hakuna motisha wala chanjo inayotolewa kuwakinga na wala hakuna fidia inayoeleweka
Matatizo yaliyotajwa ni machache. Yapo mengi mengine ambayo yanahitaji pia kutatuliwa kwa haraka.
Madaktari wetu wameshasema. Serikali inakimbilia propaganda za posho na mishahara kwenye vyombo vya habari! Mazingira mazuri ya kazi, wagonjwa kupona ndiyo ahueni(satisfaction) ya daktari.